Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Brilliant!! we jamaa engine behaviours unazijua,!!! Kuna kamsemo ka kiufundi "No replacement for displacement "
Challenge kubwa kwa wabongo ni jinsi ya kuendesha engine kubwa na kunegotiate economy ya engine ndogo, hii kitu technically inawezekana kabisa Ila wabongo tumeamua kutojifunza .kwa uoga na hear say,
 
Na kuna wale polisi huwa wanaweka barrier.

Wanakupiga kaa kushoto, ukijidai kukimbia wanakupasua hutaamini.

Wale watii, hata wakikwambia piga jeki tukague kwenye uvungu wewe tii tu.

Aah kuwakimbia hawa jamaa wa PT naona ni risk , wakiamua kupoteza muda wao mambo yanaweza kuwa mengi sana..

Me nliwahi kuwakimbia tu wale askari wa jiji wanaokamata wrong parking, nliona hawana mawasiliano yoyote zaidi ya njaa halafu wanafanya patrol na Bajaj

Ilikua Upanga pale Regency hospital, wakaanza kunikimbiza na Bajaj, wala sikutumia nguvu nyingi, nliwazungusha mule mule tu , mara Mfaume, sijui Olympio, Mazengo, nkazunguka nkapita pale Mahakama ya Kisutu nikasimama mataa ya pale Viva Towers naona nyuma kweupe tuu
 
Umeficha namba nimeelewa, huku pembeni sasa umeficha nini?

Haahahahahahhaaahahahhaa

Ngoja nikutumie Wasap picha ambayo sijaweka kivuli utaelewa kwanini nimechora chora hapo pembeni ....!!!

Mara ya kwanza niliirusha huku nikiwa nimeficha namba tuu, baada ya kuipost nikairudi kuangalia inavoonekana weeeehhh nikaifuta fastaaa aahahaaaa

Hapo sasa ndo nikaweka mavivuli kibaooo halafu nikaituma tena 😜😜😜

Nimefurahi umepata tashwishwi ya kutaka kujua nimeficha nini zaidi ya namba ...!😊
 

Ile ilikua usiku ndomana sikuona soo mkuu, mida kama ile hata akileta makeke na boda yake nampa bodi natembea mbele... Nilishasoma mazingira ki inteligensia aisee so likitokea la kutokea nina plan B tayar [emoji16]
 
Fuel economy daah [emoji23][emoji23][emoji23]

Hizo negotiation labda highway. Ukicruise constantly kati ya 110 na 130kmph at highest gear bila kuaccelerate kwa nguvu unapata mpaka 11km/l.



Ila kwa mjini na kuendesha kwenye foleni / power driving hakuna negotiation yoyote. Zinakula wese vibaya mno.
 
Haya ndio mambo nisiyotaka, ninunue gari kubwa niendeshe kama IST! Na wengi wanaingia mkenge kwa kupewa data hizi ila in reality mjini kwenye misele ya kawaida hupati hizi figures.
 
Sioni nini cha kuficha iwapo mwenye gari kaamua kukiacha wazi.
 
Haya ndio mambo nisiyotaka, ninunue gari kubwa niendeshe kama IST! Na wengi wanaingia mkenge kwa kupewa data hizi ila in reality mjini kwenye misele ya kawaida hupati hizi figures.
Na hizi gari zikiwa 130 zinafeel kama ziko 80... yani unaona haliendi! Hakuna namna uta achieve hiyo consumption kwa muda mrefu, mwenyewe utaifinya tu.

Jana nimetoka kupiga 800km Chato to Dodoma via Kahama kwa masaa 8 nimeaverage 100kmph. Fuel consumption imeaverage 8.5kmpl nimepima kwa ku subtract distance between 2 full tanks. Gari inaonyesha 8.0kmpl so its more modest.

Sijui IST angepata average speed na consumption gani but I'm sure it wouldn't be as much fun and effortless as the mighty fuga.

Sipati picha mnaoendesha vyombo vya mjerumani mnavyopata raha. Ultimate driving machines.
 
Imagine highway unapata 8km/l mjini utapata ngapi? Kwenye kusafiri kuna machaguo mawili
1.Kuinjoi ride
2.Kuokoa mafuta
Namba moja unaendesha vile unajisikia, ila namba mbili inabidi uwe unaangalia mishale yote kwenye dashboard.
 
Mh mbona Iringa,Mbeya ni kusini lakini unapanda?! Kaskazini haina maana ni juu. Juu kunaweza kuwa upande wowote ule kaskazini,kusini,magharibi,mashariki.
Ndio maana Kusini ya Iringa, Mbeya, Njombe ni eneo la (Nyanda za Juu) hapo ndipo habari ya muinuko kutoka usawa wa bahari inapowatofautisha na kusini ya Lindi na Mtwara walio karibu na usawa wa bahari

Sent from my SM-J730F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…