Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Pale mikumi hatari sana kukatiza kwa speed zaidi ya 120

Wanyama ni wanyama tu

Unaweza kuona peupeee mara pAAAp, tembo anavuka, ama nyumbu, ama Nyati (sipati picha)
Najua mkuu...
Mara ya mwisho nimepita hapo almanusura tumvamie swala alikuwa sijui anaharakia wapi kakatiza toka upande mmoja kwenda mwingine, tulikuwa kwenye ligi na jamaa mmoja hivi...chuma ishakolea ipo kama 160kph hivi, uzuri alipita spidi sana hatua moja tu ndio aliyokanyaga lami ya pili akawa kashapotelea machakani...

Ila ndio unajua tena ukishakuwa dereva uliyozoea kuchapa lapa, kuna roho ya ujasiri unakuwa nayo...
 
Panaitwa "Chalinze" kama sikosei, katikati ya msitu huko Mpanda - Uvinza rd. Kuku choma, Nyama choma bei nafuu sana hapo! Wakimbizi walowezi kibao maeneo hayo.

Nikaliona moja ya basi ya kampuni kongwe Rukwa - Katavi - Tabora - KigomaView attachment 1800195
Nilishawahi kupita huku 2016 au 2017 hivi.

Kila unaemuuliza anakwambia utekaji upo kama kawa.

Njiani tukakutana na askari polisi wakatuambia kuna tukio limetokea dk 10 kabla hatujafika.

Toka siku hiyo hii njia naiheshimu vibaya mno.
 
Nimeshawahi kutoka tabora saa moja asubuhi, saa kumi nikawa kibaha, na hapo nilikaa kama saa nzima Dodoma kwa ajili ya kula.. lakini mpaka kupita ubungo ilikua saa tatu usiku yani ile foleni siwez kuja kuisahau.. ilikua december 2019 na mnyama crown athlete
Nilishawahi kutoka morogoro saa 12 jioni nikafika dar saa 7 usiku. Kuna lari lilizima hapo gogoni.

Juzi kati nimetoka mbezi mwisho saa 12:30 asubuhi nikapita chalinze saa 3.30 asubuhi.

Mwezi uliopita nilitoka ubungo saa 5 asubuhi, nikafika vigwaza saa 11 jioni. Walikuwa wanaweka zege maeneo ya kwa matiasi.

Sahivi hata kama naenda chalinze, nazungukia bagamoyo - msata. Morogoro road ni kichefuchefu.

Morogoro road hapana kwakweli. Hii njia imekuwa kichefuchefu.
 
[emoji4]

Mkorintho unaona balaa jingine hili, hivyo usishangae sana hiyo ya 7~8 hrs Mby-Dar...

Dom - Mwz ni kama 690 au 700km hivi, upungufu wa kama 115km tu ukilinganisha na safari ya Dar - Mby...

Hapo mtu katembea masaa 7, ina maana saa la 8 ingekuwa safari inaendelea angeweza malizia hizo 115km pengine kwa dk 40 hivi
Hiyo labelling ya 'balaa jingine hili' inathibitisha upekee wa hii makitu [emoji4][emoji4]. Difference kuu ya Dom - Mza na Dar - Mby ni high traffic, njia ya kwenda Mby huko magari mengi sana. All in all daah kuachieve hii kitu ni mguu na kibati mwanzo mwisho aisee
 
Hiyo labelling ya 'balaa jingine hili' inathibitisha upekee wa hii makitu [emoji4][emoji4]. Difference kuu ya Dom - Mza na Dar - Mby ni high traffic, njia ya kwenda Mby huko magari mengi sana. All in all daah kuachieve hii kitu ni mguu na kibati mwanzo mwisho aisee
Kwa barabara zetu kupata average speed over 100kph inabidi ukimbie sana.
 
Dar - Iringa 4.5hrs, distance 490km approx
Iringa - Mbeya 3 to 3.5hrs, distance 334km approx
Muda ni usiku, gari engine ni V6/V8 (gari nyingine hizi zenye engine za kawaida ni 9 to 9.5hrs)
Dar to Mbeya, vituo vya mafuta ni viwili (Mikumi na Makambako)
Min speed 120kph na mwendo huu ni hadi kule Iyovi, Max speed kisahani chote sehemu zinazoruhusu kama Ruaha Mbuyuni, Makambako hadi Iringa, Moro hadi Chalinze, sehemu kama Mikumi unajitoa ufahamu ile 50kph yao ya usiku unafanya kama huijui...

Sehemu speed kidogo inapungua Kitonga wakati wa kupanda approx 70 to 80kph...

Chimala hadi maeneo ya Nsonyanga Mbeya sababu ya barabara ina madimbwi na mashimo...

Mlandizi hadi pale mbele kidogo ya daraja la juu la treni, barabara ina mawimbi hatari...

Hii ilikuwa achieved wakati hapo Picha ya ndege hawajabomoa barabara, Kingolwira/Kingolwira Magereza hawajaanza chimba barabara, Iyovi hawajaanza kupanua barabara...
Dar iringa 501km
 
Mkuu Siri moja ya Nissan Patrol ukiwa off road ni comfortability. Ukiendesha L/Cruiser Hardtop, Defender au Pajero huwa hazina utulivu kama wa Nissan.

Hongera zimfikie mmiliki kwa kutunza, Nissan ni gari ya mjapani ambayo haitaki janja janja kama Toyota.
Nissan patrol ya kwaza. Kuendesha ilikuwa ya mzee fulani wa dodoma , trip ya dar to dom , gari ilikuwa auto halafu sijui kwa nini halikuwa na nguvu kabisa na ndio lilikuwa linetoka japan. toka siku hiyo nikayachukia kabisa hayo madude ,
Ila must admit, zipo comfortable sana
 
Back
Top Bottom