Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Duh nimemiss roadtrip ila kila nikichungulia bei ya wese nakuwa mpole...full tank moja 200,000/- na trip ya kawaida nahitaji tank mbili balaa tupu!
mimi namshukuru Mungu kwa kweli, hii nchi kama kuzurula nimezurula sana na ninaendelea kuzurula.

mpaka sasa karibia mikoa yote nimefika. nimebakiza kisiwa cha pemba tu.

hii ilikuwa katika roadtrip wiki chache zilizopita nikitoka mkoa A kwenda mkoa D.

wakali wa location bila shaka mnaijua hiyo barabara, ina mkeka flani umetulia sana kwa driving.
 
Hii siyi Iringa Dodoma? Via Mtera?
Nimeona viraka 😀😀
 
Pole mkuu. Nashangaa mpaka leo hakuna mfanyabiashara aliyeweka sheli katikati humo hata mitaa ya Migori
 
Hahaha sio kama IST.. ila ile [emoji146] ya King of the Road inavuliwa..
Hizo jina ni LC200..!
Hahaha mkuu kama hao wajerumani wanaoshuka bandarini ni wale wale kina BMW 1 series na 3 series, au wale kina X series wa miaka ya 2000s, basi LC 200 ataendelea tu kuwa King of the road until further notice

Kwahiyo na wanaozitengeneza wanavyoandika neno V8 kule nyuma huwa wanakosea siyo au hazitumii V8 engines
 
Yes sio kila mjerumani atawezana na LC200.. Ila hata Bimmerz za pre 2000s zinasmoke LC200.. E36 328i na E46 330i.. Wajerumani kwenye swala la mwendo ndio speciality yao..!

V8 badge sio jina la gari.. Kuna Toyota nyingi zinatumia V8 engines ila haziitwi Vietee..! Wewe kutumia pombe haibadilishi jina lako Hadde kuwa chaPombe..!
 
Inabidi ujifunze sana juu ya magari. Neno V8 lisikubabaishe. Nimepost video ya vidude viwili, kimoja kibaenda kama 250kph halafu mwingine anapita kama kasimama figure out anaenda speed gani. Hivyo vigari ni cc2000 tu 4 cylinder hizo VX zenu hazitii pua hapo. Mwaka wa gari sio issue. Kuna 1series 130i mwaka 2007 hakuna VX bongo inatia pua hapo.
 
Kuna V8 bwege nasikia....
 
Mkuu hapa bongo ni wangapi wenye hizo bimmer ulizozitaja maana bandarini kwetu zinazoshuka ni zile zile tulizozizoea

My point was hawakosei kuiita LC V8 since inatumia V8 engine labda ungeniambia wanachokosea ni kudhani V8 ndiyo jina la gari

Engine ya V8 kutumika na gari nyingi sidhani kama ndiyo sababu ya LC kutoitwa V8 labda ungesema wawe wanaspecify ila hawakosei
 
Hahaha mkuu wala sijababaishwa na V8 engines ila hapo tunaongelea LC 200 (na siyo zote) maana kuna hata gari zenye V6 zinatimuka kuliko zenye V8

Hiyo video sijaiona ni vidude gani hivyo

Hizo 130i za 2007 hapo bandarini kwetu zinashuka ngapi kama alivyosema ndugu KndNo1 maana isije kuwa umenijibu bila kuelewa point yangu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…