Waziri Aweso amshukuru Rais Samia kwa uwekezaji mkubwa wa fedha katika sekta ya maji katika Jiji la Mwanza

Waziri Aweso amshukuru Rais Samia kwa uwekezaji mkubwa wa fedha katika sekta ya maji katika Jiji la Mwanza

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa wa fedha katika sekta ya maji katika Jiji la Mwanza kwani miradi mingi inaendelea na ikikamilika changamoto ya maji itategemewa kubaki historia.

Waziri Aweso ameyasema hayo tarehe 21 Desemba 2024 wakati Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa alipotembelea na kukagua Mradi wa Ujenzi wa Tanki la Kuhifadhi Majisafi Kisesa- Bujora Mwanza.

Katika hatua nyingine, Waziri Aweso amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA) kwa kuondoa malalamiko ya mara kwa mara ya ukosefu na upungufu wa huduma ya maji Mwanza na viunga vyake.

Waziri Aweso amekiri kwamba kulikuwa na malalamiko makubwa kuhusu upatikanaji wa maji ila kwa sasa yamepungua tangu Mkurugenzi Nelly Msuya aanze kazi.

 
Tuna siasa za kijuha sana.
Mwanza Kuna miradi mitatu imeshakamilika kwa 100% ila kwa makusudi mazima haifunguliwi simply inasubiri mwaka wa uchaguzi 2025 ili ianze kutumika..

Mradi wa maji kwa mitaa ya Buhongwa, sawa, Kishiri na hiyo Kisesa ulishakamilika na mchina hayupo hata site.....Watu wanateseka lakini hadi mwakani ili kumtafutia Mabula kula.

Daraja la Busisi lilitakiwa likabidhiwe desemba hii 2024...
Lakini nasikia muda umesogezwa hadi 2025.

Meli mpya ya kwenda Bukoba iianza kujengwa 2017, nayo inasubiri 2025 ili ianze kuzinduliwa.....assembly ya meli hii imedumu kwa miaka 7, ulishaona wapi.

Barbara ya Buhongwa to Kishiri nayo imewekwa target ikamilike 2025 ili kumtafutia Stanslaus Mabula kura
 
Back
Top Bottom