Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Waziri wa Maji Jumaa Aweso amefika kijiji cha Kwamsisi kilichopo katika kata ya Kwamsisi, wilayani Handeni mkoani Tanga kujionea hali ya upatikanaji wa maji katika eneo hilo na changamoto iliyobainika kutokana na video iliyochapishwa katika ukurasa wa Instagram wa mtangazaji Mbarouk Khan.
Mbarouk alichapisha video inayoonesha changamoto ya maji kwa wakazi wa eneo hilo huku akieledha adha wanayoipata kutokana na changamoto hiyo, hali iliyomgusa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye alimtaka Waziri Aweso ahakikishe changamoto ya upatikanaji wa maji safi katika eneo hilo inatatuliwa.
Mbarouk alichapisha video inayoonesha changamoto ya maji kwa wakazi wa eneo hilo huku akieledha adha wanayoipata kutokana na changamoto hiyo, hali iliyomgusa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye alimtaka Waziri Aweso ahakikishe changamoto ya upatikanaji wa maji safi katika eneo hilo inatatuliwa.