Waziri Bashe hakutakiwa kuukataa msaada wa mchele kutoka Marekani na kama alikuwa na mashaka yoyote angewatumia TBS

Waziri Bashe hakutakiwa kuukataa msaada wa mchele kutoka Marekani na kama alikuwa na mashaka yoyote angewatumia TBS

Hakuna cha tbs wala latra je uo mchele ungeletewa wewe na familia yako kilo 100 mle mwezi huu mngekula? Ok unasema huna shida sasa mbona mnawalazimishia wenzenu wamewaambia wanashida na mchele
 
Hakuna cha tbs wala latra je uo mchele ungeletewa wewe na familia yako kilo 100 mle mwezi huu mngekula? Ok unasema huna shida sasa mbona mnawalazimishia wenzenu wamewaambia wanashida na mchele
Kazi ya Serikali ni kuwalinda watu na sio kukataa tu. Kama Serikali ikinihakikishi ni salama hauna matatizo ,ninakula bila tatizo.

Huku mtaani tunakula vitu vya ovyo zaidi ,unakuta Kuna kakiwanda Cha kusaga na kukoboa mahindi kinatumia mifuko yenye nembo ya Azam kuweka bidhaa zao ,wanatumia mgongo wa jina kuuzia bidhaa zao na Bado tume survive
 
Watanzania ni wajinga sana
Wanakataa ila Ngano, Mafuta ya kupikia yote yana virutubisho
Marekani sio wajinga kutaka kuwamaliza Kwa mbinu za kishamba hivyo. Huo mchele ni salama 100% hawawezi kutumia kitu ambacho kitaacha alama mwilini mwako
 
Wewe ni mjinga. kwani tanzania ins shida ya chakula? Umeambiwa mchele upo wa kutosha si wangenunua hapa hapa kama lengo Lao lilikua msaada!

Tanzania haina njaa wangepeleka gala kwa wenye uhitaji
Aliye shiba siku hamkumbuki mwenye njaa, hapo unazungumzia ufahari wako na WA familia yako na sio maisha ya watanzania
 
Watanzania hatujui tunataka nini.

Kuna wanaosema bora mchele tukatae wengine wanasema tuukubali.

Ila mimi naishauri marekani WAACHE KUTOA MISAADA AMBAYO HAWAKUOMBWA.

laiti kama tanzania imgekuwa imeomba huu mchele basi Bashe asingeukataa.

Tatizo sio tanzania kukataa msaada hapana bali tatizo ni la wamarekani kutoa msaada ambao hawakuombwa.

Wapeleke mchele katika nchi zenye njaa na migogoro ambayo inawaletea uhaba wa chakula.
Wameamua kusaidia wanafunzi wenye njaa nyie watoto wenu wapo saints hamuwezi ona umuhimu,njaa imekatiza ndoto za wanafunzi wengi sana
 
Acha uongo Usa ajaanza leo kuipa msaada wa chkula Tza alishawahi tupa msaada wa mahindi ya kulishia ng'ombe Yale ya njano tukala Hadi kushiba.
USA ndie anaelisha chakula karibu wakimbizi wote Dunia kuanzia makambi ya kigoma hadi Afghanistan,mbona huko hawajawa mashoga.
 
Mada hii ni kuelezea mashaka makubwa niliyonayo kwa Waziri wetu wa kilimo namna maamuzi yake yanavyoweza kuharibu mahusiano ya kimataifa kama asipojirekebisha.

Kwanza kabisa nianze Kwa 'declare interest' ,Sina mahusiano ya aina yoyote na NGO iliyoleta mchele wa msaada wenye virutubisho kutoka nchini Marekani chini ya kampeni ya wizara ya kilimo ya Marekani inayoitwa "Pamoja tuwalishe" na 'interest' pekee niliyonayo ni Kwa maslahi mapana ya nchi yangu .

Siku zote mjumbe hauawi na hiyo NGO inabaki kuwa ni mjumbe tu wa wizara ya kilimo ya Marekani ,kitendo Cha Waziri kuonesha kukasirishwa na kitendo Cha mjumbe kinaleta picha isiyopendeza.

Kwa mtazamo wangu badala ya Waziri Bashe kuonesha kukasirishwa na kuletwa Kwa mchele na hiyo NGO angetumia nafasi hiyo kufanya "formal communication" na wizara ya kilimo ya Marekani juu ya mambo tunayohitaji.

Kwa kuwa mchele huo ni msaada sikuona ulazima wowote wa Waziri kusema kwamba mchele tunao ,Kwa kuwa lengo la kampeni hiyo ni zuri ,tunatakiwa kuupokea msaada huo na kushukuru na wizara ingetumia TBS kuchunguza ubora wa mchele huo kimya kimya kabla haujaanza kutumika na kama kungekuwa na mashaka yoyote Serikali ingekataa baada ya kufanyika Kwa uchunguzi na ubora na sio Kwa hoja za Waziri.

Mashaka niliyonayo kwa Waziri Bashe ni kuwa:

Kama Waziri hajui athari za kimahusiano zinazoweza kuibuka kutokana na kauli tu. Kitendo Cha Waziri Bashe kudai Kwa nini wasingeleta virutubisho wachanganye tukiwaona ,sio rafiki Kwa afya ya diplomasia. Kitendo hicho kinaweza kufikirika kama tuhuma ya usalama. Kabla ya kauli hiyo alitakiwa kuwatumia TBS kuuchunguza mchele.

Marekani ni Moja ya nchi zinazozalisha nataka ( mchele na mahindi) Kwa wingi duniani na kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa ,nchi yetu inaweza kukumbwa na baa la njaa na tukahitaji msaada wa Chakula kutoka nje. Je, tutapata wapi nguvu za kuomba msaada kutoka Marekani kama tumeamua kukataa msaada Sasa ?

Pengine kulikuwa na Cha zaidi ambacho hatukijui lakini kama ni hiki kilichopo ,ni vema Waziri Bashe angeliendea suala Hilo Kwa busara, angejiridhisha kwanza na angejua hatua Kwa busara ili tuendelee kuimarisha mahusiano na nchi nyingine.

Kila siku Rais anasisitiza mifumo kusomana ili kuepusha migogoro , na kama mifumo ingekuwa inasomana kusingekuwa na kauli za namna Ile kutoka Kwa Waziri.

Ahsante
Wazo lako zuri
 
Bashe yupo sahihi kwamba,badala ya kuleta Michele,walete hizo pesa wanunue Kwa wakulima watanzania hizo shule zipewe,mm nashangaa,kwanini wasitupe teknolojia na ujuzi wa kuzalisha huo Michele maana ardhi tunayo kama kweli Wana ni ya kutusaidia?,je,hao wamarekani watatulisha hafi lini?
Kipi walichotuanzishia tumeweza baada ya wao kuondoka,chakula nchini bei ghali sana na hakitoshi.
Ule ni msaada wa wakulima wachache TU.
Kule MTU na mkewe wake wanaweza kulima Hadi heka elf 10 wakati sisi watu elf moja hatuwezi Lima heka hizo.
 
Na hoja aliitoa Bashe kwamba,wakulima watanzania wapewe pesa maana huo Michele tunao,pia misaada ni hiari sio lazima,unaweza kukataa,au kukubali maana tupo kwenye nchi yetu
Kwanini tunalazimisha tupewe pesa?au kwa kuwa tutapata unafuu wa kuiba pesa za wafadhili
 
Namuunga mkono Bashe. Kukubali msaada wa mchele kutoka marekani ni matusi na fedheha kwa wakulima wa Tanzania.

Wakulima wapewe hizo fedha wa_supplay mchele kwenye hizo shule
Kwanini unanganaia fedha wakati na eye anawakulima hawana pakuuza chakula.Kama wewe hupeotect wakulima basi acha wenye fedha zao waprotect wakulima wao kupitia misaaada
 
mleta Uzi unadhani una akili na unayajua mambo mengi kuliko Waziri wa kilimo? acha hizo mkuu!


YESU NI BWANA NA MWOKOZI
 
Huo mchele wa Tanzania ungetolewa kama msaada au ungenunuliwa ? Unajua ugumu wa wazazi kuchangia lishe mashuleni ulivyo? Tuacheni siasa, ni jambo la heri tuwapongeze wamarekani
Wao serikali wameshindwa kuwahamasisha wananchi kuzalisha na kutia michnago ya chakula cha watoto wao lakini tuko tayari kucritise chakula kilichotolewa..Jinga sana viongozi wetu
 
Lengo la msaada likiwa zuri hakuna sababu ya kukataa msaada, dunia nzima wanaishi hivyo
Mimi nafikiri msaada tunaohitaji ni Uwezeshwaji. Tuwezeshwe kwenye technology kwakuwa ardhi ya kutosha tunayo, tutazalisha chakula chetu wenyewe kwa sasa na siku zijazo.

Waziri yuko sahihi kakataa chakula ( instant food) ili tupewe majembe tukajilimie cha kwetu wenyewe.
 
Kwanini tunalazimisha tupewe pesa?au kwa kuwa tutapata unafuu wa kuiba pesa za wafadhili
Hajalazimusha,alafu mbona mnlazimisha hicho chakula kipewe wanafunzi,au nyinyi mnataka kuuza?
 
Marekani sio wajinga kutaka kuwamaliza Kwa mbinu za kishamba hivyo. Huo mchele ni salama 100% hawawezi kutumia kitu ambacho kitaacha alama mwilini mwako
Ndo maana nasema Watz huwa hatuna hoja sisi tunarushwa kama maharagwe
 
Back
Top Bottom