Waziri Biteko aagiza watumishi wa TANESCO waliokuwa likizo ya pasaka warudi haraka

Hivi wafanyakazi wa TANESCO wanapata wapi ujasiri hata wa kuomba likizo?

Kwa kazi ipi wanayoifanya ilihali hata sasahivi hakuna umeme maeneo karibu yote ya kaskazini?

Kweli kwenye hii nchi tunabembelezana sana na Wananchi tunaonekana hovyo tu
 
Watu mna siri sana kumbe kuna likizo ya pasaka na hamsemi!

Namshukuru sana mama kwa kunifumbua akili.
Siku 3 karibia taasisi kubwa zote ,kila sikuu watu wanaondoka tena kama hii pasaka imekaa poa ,mtu kaondoka Alhamisi anarudi jumanne au j5 .

Tena wanapata na festival allowance package kwa taasisi kubwa ..
 
Siku 3 karibia taasisi kubwa zote ,kila sikuu watu wanaondoka tena kama hii pasaka imekaa poa ,mtu kaondoka Alhamisi anarudi jumanne au j5 .

Tena wanapata na festival allowance package kwa taasisi kubwa ..
Nchi ya maziwa na asali,watu wanaenjoy tu
 
Nilikuwa nasikiliza kipindi changu kizuri, umeme umekatika. Tanesco tumewakosea nini? Uwekezaji hasa wageni wataweza hii hali?
 
Kama mikoa 3 tu ndo inapata umeme tena baadhi ya wilaya, basi tatizo ni kubwa sana huko ilikotokea hitilafu..
 
Biteko ni kwanini tusiwe na System ya Backup Generators kila Mkoa na Wilaya?

Hawa Wawekezaji si wataikimbia hii Nchi kweli.
Hapo wakikubali hizo bei za majenereta sasa. Achatu ngoma iwe hivihivi
 
Huyo waziri aache kusumbua watu. Kama wakienda likizo au wakiwepo kazini umeme sio wa uhakika anawauta wanini?
Tena angewaongezea hata miezi mitatu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…