Wana JF naona mjadala sasa unataka kuharibika kwa dataz za kudhania vile. Naomba ieleweke kuwa kuna makundi mawili hapa tunayoyaongelea: La kwanza ni kundi la akina Mzindakaya, JK, Karume, Rwakatare n.k. Hawa wana shahada za heshima tu (honoris causa) siyo za kusomea! Chuo chochote kinaweza mtunukia mtu shahada hiyo ya heshima kwa kutambua mchango wake katika jambo fulani. Siku za nyuma hata baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Spika Adam Sapi, Salim Ahmed Salim, Kaunda na Obote walipewa heshima hiyo na vyuo mbalimbali duniani.
Kundi lenye matatizo ni lile lenye shahada feki na linadai kuzisomea shahada hizo! Kundi hili ni hatari sana maana linaharibu kabisa heshima, sifa na viwango vya elimu nchini.
Wafuatao wana vyeti feki vinavyoitia aibu Serikali na nchi kwa ujumla:
(1) Salmin Amour - Ph.D yake ni feki, ya kisiasa. Aliipata Ujerumani Mashariki enzi hizo kwa miezi mitatu tu huku akiwa na cheti cha form four tu!
(2) Pius Ng'wandu - Ph.D yake ni feki. Chuo anachodai kusoma cha Stanford, Marekani hakina kumbukumbu zake. Aliosoma nao huko Marekani, akina Prof. Baregu, wanajua kuwa ana Masters tu!
(3) Mary Nagu - Ph.D yaje ni ya kununua kwenye mtandao.
(4) Emmanuel Nchimbi - Ph.D yake ya uchumi ni ya kununua. Hana uelewa wowote wa economics kichwani mwake.
(5) Makongoro Mahanga - Ph.D yake ya ugavi ni ya kununua kama Nchimbi.
(6) Didas Masaburi - Ph.D yake ilinunuliwa pamoja na ya kaka yake Makongoro.
(7) Norman Sigallah - Ph.D yake ni ya kununua kwenye mtandao.
(8) Mafwenga - Ph.D yake sawa na ya Sigallah
(9) Nangale - Ph.D yake ni kutoka chuo kimoja bomu cha chini ya viwango, London.
(10) Mathayo David - Ph.D ya kujipachika.
(11) Mutamwega - Ph.D yake ni feki, ya kununua. Mhusika hawezi kuandika hata sentensi moja sahihi ya Kiingereza.
(12) Lukuvi - Masters yake ni feki. Kaipata akiwa na sifa za elimu ya darasa la saba na cheti cha ualimu, class C.
(13) Samuel Chitalilo - Vyeti vyake vya elimu ya juu toka Uganda vyote ni feki. Ana kesi ya kujibu mahakamani!
Nimepata taarifa mbalimbali kuhusu vyeti vya Wabunge wafuatao: Sigonda, Capt.Komba, Omari Mzeru na Savelina Mwijage. Nazifanyia kazi. Nitazianika hapa muda muafaka!
Ijabu