#COVID19 Waziri Gwajima aagiza Askofu Gwajima kukamatwa ili athibitishe kauli anazozitoa dhidi ya Serikali na viongozi kuhusu chanjo ya UVIKO-19

#COVID19 Waziri Gwajima aagiza Askofu Gwajima kukamatwa ili athibitishe kauli anazozitoa dhidi ya Serikali na viongozi kuhusu chanjo ya UVIKO-19

Mimi nilidhani ni mtu na dada yake kumbe ni mtu na shemejiye!
Mie nasubiri hio ligi vile itakavyo kuwa.
 
Hicho kichaka hakitakusaidia sana, tuambiwe, madhara (side effects) za hizo chanjo baada ya miaka mi5 ni zipi? Kwa atakayechomwa na kwa watoto atakaowazaa, ziwekwe wazi na watuambie walifanya hayo majaribio kuanzia mwaka gani hadi mwaka gani...
Google basi dogooooo
 
Jibuni hoja kwa hoja na si kuweweseka kumkamata Josepht.
Wakati wa Magufuli ni nyie hao hao mlokuwa mstari wa mbele kuungana naye kupinga chanjo.Wewe waziri wa afya ulionyesha mifano mingi na kusisitiza matumizi malimao,vitunguu,pilipili na takata nyingine nyingi,pamoja na kupiga nyungu kuwa ndo dawa za korona.Mlikwenda hata kuchukua uchafu mwingine kule Madagascar kwa ndege ya serikali.Sasa toeni proof za kisayansi kudhibitisha kwamba chanjo ni salama na si kusumbua wale wanaosema si salama kwa maana ninyi tangu mwanzo mlituaminisha hivyo.
Acheni kuwa na double standard.
Jameni mwacheni Doroth aupige mwingi.

Alishasema vita hupiganwa kwa silaha ya wakati husika.

Kinjekitile alitumia silaha ya maji, japo ilikuwa imani potofu, akajitutumua kushindana na mjerumani aloyekuwa na bunduki. Anyway, hiyo ndiyo silaha waliyoimudu wakati wao.

Enzi za mwendazake Jiwe tulipewa malimao, pilipili kichaa, tangawizi, miarobaini, nk, kwani ndiyo silaha zilizokuwepo.

Dunia imetengeneza silaha mpya (SMG) chanjo, sisi ni nani mpaka tusinunue silaha mpya tuupige mwingi?

Nasimama na Doroth...
 
Askofu Gwajima ni shemeji yangu, lakini mimi waziri wa wananchi nimekula kiapo mbele ya Rais cha kutumiakia nchi, sio kumtumikia shemeji. Mimi ndiye msemaji wa masuala ya afya nchini, nimechoka kuvurugwa naagiza akamatwe popote na akahojiwe juu ya haya madai - Dk. Gwajima
--
Butiama.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Doroth Gwajima ameliagiza Jeshi la Polisi pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini ( Takukuru) kumkamata na kumhoji mbunge wa Kawe, Josephat Gwajima ili athibitishe kauli anazozitoa dhidi ya Serikali na viongozi kuhusu chanjo ya Uviko 19.

Dk Gwajima ametoa agizo hilo leo Jumanne Agosti 17, 2021 katika kijiji cha Kyatunge wilayani Butiama akibainisha kuwa Askofu Gwajima amekuwa akitoa taarifa za kupotosha kwa makusudi jambo linaloivuruga wizara yake na Serikali katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo.

Credits: Mwananchi

Pia soma
- #COVID19 - Dkt. Mollel: Askofu Gwajima ataitwa athibitishe kauli zake, akishindwa tutamshughulikia
Najiuliza je ni kweli kwamba mwwchama wa ccm ambaye atachaguliwa ama kuteuliwa nafasi ya uongozi wa juu wa chama cha mapinduzi hafanyi kiapo cha utii kwa viongozi wao wakuu na hata kwa chama kabla ya kukabidhiwa wadhifa husika? na kama ndiyo je hawa wanaopingana na viongozi wao kwa habari ya chanjo wanapta wapi ujasiri? na chama kinawachukulia hatua gani za kwadhibiti ama kuwaadhibu kwa utovu wa nidhamu kwa chama na kwa viongozi wakuu kabla hawajasababisha madhara makubwa zaidi kwenye chama na kwa taifa?

kwa mfano kama mbunge wa chama kinachotawala anaweza kusimama hadharani akampinga mwenyekiti wake wa chama ambacho ndicho kilichompatia ridhaa ya uongozi huu ni sawa kukosa adabu na kuondokewa kwa utii kulikopitiliza na hii ni dharau sana kwa kiongozi wako mkuu wa chama chako

lakini kwa sababu mtu huyu siyo mwenye madaraka ya mwisho kwenye chama ni bora kamati kuu ya chama wakakaa kwa ajili yake na kumjadili mwisho wa siku wafikie mahali wakubali kumfuta uanachama kwenye chama jambo ambalo litakalomsababisha mtu huyo pia kukosa ama kupoteza sifa ya kuendelea na uongozi Kwenye nafasi ambazo amezipata kupitia chama ama ambazo sifa ya kuzipata ni kuwa mwanachama wa chama husika

ikiwa hivyo watu ama viongozi watakumbuka kuwaheshimu na kuwatii wakuu wao ktk madaraka.
 
Najiuliza je ni kweli kwamba mwwchama wa ccm ambaye atachaguliwa ama kuteuliwa nafasi ya uongozi wa juu wa chama cha mapinduzi hafanyi kiapo cha utii kwa viongozi wao wakuu na hata kwa chama kabla ya kukabidhiwa wadhifa husika? na kama ndiyo je hawa wanaopingana na viongozi wao kwa habari ya chanjo wanapta wapi ujasiri? na chama kinawachukulia hatua gani za kwadhibiti ama kuwaadhibu kwa utovu wa nidhamu kwa chama na kwa viongozi wakuu kabla hawajasababisha madhara makubwa zaidi kwenye chama na kwa taifa?

kwa mfano kama mbunge wa chama kinachotawala anaweza kusimama hadharani akampinga mwenyekiti wake wa chama ambacho ndicho kilichompatia ridhaa ya uongozi huu ni sawa kukosa adabu na kuondokewa kwa utii kulikopitiliza na hii ni dharau sana kwa kiongozi wako mkuu wa chama chako

lakini kwa sababu mtu huyu siyo mwenye madaraka ya mwisho kwenye chama ni bora kamati kuu ya chama wakakaa kwa ajili yake na kumjadili mwisho wa siku wafikie mahali wakubali kumfuta uanachama kwenye chama jambo ambalo litakalomsababisha mtu huyo pia kukosa ama kupoteza sifa ya kuendelea na uongozi Kwenye nafasi ambazo amezipata kupitia chama ama ambazo sifa ya kuzipata ni kuwa mwanachama wa chama husika

ikiwa hivyo watu ama viongozi watakumbuka kuwaheshimu na kuwatii wakuu wao ktk madaraka.
Moja ya AHADI ZA WANACHAMA WA CHAMA CHA MAPINDUZI Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko
 
Huyu waziri atapelekewa moto na mchungaji gwajima hadi aombe poo
Mda huu tayari Gwajima yupo busy kusaka siri zake udhaifu wake wote mapungufu yake yote apate kuyaanika kwa ile style ya kuliamsha dude
 
"Hatujapa taarifa rasmi ya maandishi ya kutakiwa kumkamata Mhe.Gwajima, lakini hata tukiipokea tutachunguza iwapo matamshi yake yanaangukia Kwenye Jinai, lakini tunaweza kuwashauri wakatatua jambo hili kwa njia za mazungumzo badala ya Polisi"-IGP Simon Sirro

226491347_128826996076898_5333616628060486514_n.jpg
 
"Hatujapa taarifa rasmi ya maandishi ya kutakiwa kumkamata Mhe.Gwajima, lakini hata tukiipokea tutachunguza iwapo matamshi yake yanaangukia Kwenye Jinai, lakini tunaweza kuwashauri wakatatua jambo hili kwa njia za mazungumzo badala ya Polisi"-IGP Simon Sirro
It's a War against two idiots.
They used to worship the same god mwendazake, but now everyone is looking for his/her own 🍞 bread
A bread is now became their god
 
Back
Top Bottom