Waziri Gwajima, kuna haki za watoto zinakiukwa wazi wazi. Hatua za kuwanusuru zinahitajika

Waziri Gwajima, kuna haki za watoto zinakiukwa wazi wazi. Hatua za kuwanusuru zinahitajika

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Mhe. Waziri mama Dkt. Gwajima D hongera kwa majukumu.

Hoja yangu ni fupi.

Katika vibanda vya kusubiria abiria wanaotumia vivuko pale Kivukoni na Kigamboni kuna Watanzania wenzetu walioamua kuwa ombaomba ili wapate pesa za kujikimu.

Pamoja na kwamba wanaomba pale kwa muda mrefu, lakini sasa wameonekana kuwatumia watoto wadogo kwenye shughuli hiyo. Jambo hilo tunaliona maeneo mbalimbali nchini

Hoja yangu ni kuhusu Haki ya Mtoto hususani kwenye malezi na elimu. Je, watoto wale wanalindwaje na jamhuri waweze kupata elimu na hata malezi kama watoto wengine?

Nafahamu ombaomba fulani pale Moroco mataa ambapo hapo zamani alikuwa mtoto anaongozana na baba yake wakiomba eneo hilo.

Ahsante
 
Kuna mama mmoja alikuwa anatega posta karibu na ofisi za ATCL. Yule alikuwa na watoto kabisa na wote wanaomba. Nilikuwa nikipita pale na kumuangalia mazingira aliyokuwa nayo, niliingiwa imani sana.

Suala la omba omba si kitu cha kukiangalia on the surface, inabidi uingie deeper. Kuna ambao wanafanya biashara kwa kuchukua watoto na walemavu vijijini na kuna wengine wanaomba kwa sababu hawana hata uhakika wa kula. Yani watoto wanaamka asubuhi wakifikiria wapi wakale au wakaombe maana nyumbani hakupikiki.

Pia watu waelimishwe zaidi kuhusu uzazi wa mpango maana huwezi zaa watoto watano kwa kuamini kila mmoja anakuja na ridhki yake . Mwisho wa siku ndio watoto wanateseka.
 
Mhe. Waziri mama Dkt. Gwajima D hongera kwa majukumu.

Hoja yangu ni fupi.
Katika vibanda vya kusubiria abiria wanaotumia vivuko pale Kivukoni na Kigamboni kuna Watanzania wenzetu walioamua kuwa ombaomba ili wapate pesa za kujikimu...
Kulikuwa na operesheni chini ya mamlaka ya mkoa husika. Tutawasiliana nao tuone maendeleo na kuongeza nguvu. Shukrani

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Kuna Hadithi naisoma "The Charismatic Charlie Wade".. ndani yake inasimulia jinsi huko China kulitokea makundi yaliyojulikana kama "Beggar Gangs" yaliyomilikiwa na watu matajiri Ili kuendelea kujitajirisha.
Fanya kushare link mkuu
 
Kulikuwa na operesheni chini ya mamlaka ya mkoa husika. Tutawasiliana nao tuone maendeleo na kuongeza nguvu. Shukrani

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Naahukuru kwa majibu yako Mhe Waziri. Nina hoja ya nyongeza.

Tumezoea kuona mamlaka za chini wakitekeleza majukumu yao kwa mzuka kuliko wajibu. Je unakubaliana nami kuwa kunahitajika uratibu mahususi kuwanasua watoto hawa kutoka kwenye janga linalowakabili la kukosa matunzo na elimu.

Pia, wataalam wako wa wizara wapo tayari kuandaa mwongozo utakaotumiwa na mamlaka zinazosimamia haki za watoto kuhusu watoto wa mitaani na ombaomba?

Wakishazoea hali hii watakuwa hawana future nzuri
 
Kuna Hadithi naisoma "The Charismatic Charlie Wade".. ndani yake inasimulia jinsi huko China kulitokea makundi yaliyojulikana kama "Beggar Gangs" yaliyomilikiwa na watu matajiri Ili kuendelea kujitajirisha.
Mm mwenyewe najipanga. Nataka nkawabebe kama sita hiv nawamwaga mbagala hapa. Kazi yangu kuwapaka masizi ya mkaa asubuhi tu
 
Naahukuru kwa majibu yako Mhe Waziri. Nina hoja ya nyongeza.

Tumezoea kuona mamlaka za chini wakitekeleza majukumu yao kwa mzuka kuliko wajibu. Je unakubaliana nami kuwa kunahitajika uratibu mahususi kuwanasua watoto hawa kutoka kwenye janga linalowakabili la kukosa matunzo na elimu.

Pia, wataalam wako wa wizara wapo tayari kuandaa mwongozo utakaotumiwa na mamlaka zinazosimamia haki za watoto kuhusu watoto wa mitaani na ombaomba?

Wakishazoea hali hii watakuwa hawana future nzuri
Tumepokea maoni yako kwa maboresho, tuko tayari kupokea maoni mbalimbali kwani, maoni ya jamii yanaakisi vema zaidi uhalisia. Ubarikiwe

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Naahukuru kwa majibu yako Mhe Waziri. Nina hoja ya nyongeza.

Tumezoea kuona mamlaka za chini wakitekeleza majukumu yao kwa mzuka kuliko wajibu. Je unakubaliana nami kuwa kunahitajika uratibu mahususi kuwanasua watoto hawa kutoka kwenye janga linalowakabili la kukosa matunzo na elimu.

Pia, wataalam wako wa wizara wapo tayari kuandaa mwongozo utakaotumiwa na mamlaka zinazosimamia haki za watoto kuhusu watoto wa mitaani na ombaomba?

Wakishazoea hali hii watakuwa hawana future nzuri
Naomba nilijibu hili kitaalamu, namuavhia waziri alijibu katika muktadha wa kiutawala (pitical will and commitment).

Naomba niutambue uwepo wa mheshimiwa Dr. Dorothi Gwajima. Mtoa mada na aliyemtag hapa hapa wamezingatia protokali.

Matatizo haya ya street begars yamefungamana na umaskin na family fragmentation. Although, ni matatizo serious sana mijini.

Kwa jitihada zilizopo na zinazoendelea nyingi Kwa sasa ni multidiverse. Znapiga engo zote mana kukomalia elimu PEKEE bila kulingalia hili la umaskin ni technical negligence. Nikiri kwamba kwa sasa yanapungua japo si kwa kasi ile inayotakiwa. Lakin pia orphanage centers zimepungua hhuku mitaan hasa huku shunty towns na hili ni moja ya suluhu kubwa sana la hii kesi


Jitihada za kila mtu katika kuchukua hatua kwa upande wake ziendelee Kwan hii ni kesi moja serious sana kama uzazi katika familia maskin haupangiki vizuri
 
Tumepokea maoni yako kwa maboresho, tuko tayari kupokea maoni mbalimbali kwani, maoni ya jamii yanaakisi vema zaidi uhalisia. Ubarikiwe

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Mheshimiwa,
Kwan Tasaf inawahesabu vipi hawa watoto na je Kuna survey yoyote imewahi kufanyika kupata ni quantile ipo hasa ya hawa watoto inatoa idadi kubwa
 
Tatizo la Tanzania ni siasa
Watu wakitaka fanya wengine watapinga na kusema haki za binadamu
Mm mkuu imeniuma sana.

Kariakoo Kuna ombaomba Doni, anaishi kimara analetwa kariakoo na pikipiki na kurudishwa na pikipiki Yani elfu kumi na mbili mara mbili. JUMLA 24000.

Mchana anakula biriyani la 6500 na juis ya miwa. Asubuhi anakula supu na chapati mbili. Sisi tunaomsaidia hatuna uchumi huu.

Kama vip miheshimiwa Dkt Gwajima wasajiliwe walipe na Kodi 😁
 
Swala la MTU kuwa omba omba lipo kiroho zaidi is about someone's spirit hii ni roho ya Kuwa ombaomba inamvaa MTU na kuanza kuomba hii IPO dunia nzima.

Kama walivyo hustler na walivyo beggars. So serikali itumie zaidi hekima kuwafanya hawa ombaomba hela wanazopata wawekeze katika kazi za kawaida na halali .


Kuna watu ni walemavu na wapo broke Ila hawawezi kuomba omba mtaani then serikali itoe zaidi elimu kuhusu wat u kujitambua.
 
Swala la MTU kuwa omba omba lipo kiroho zaidi is about someone's spirit hii ni roho ya Kuwa ombaomba inamvaa MTU na kuanza kuomba hii IPO dunia nzima.

Kama walivyo hustler na walivyo beggars. So serikali itumie zaidi hekima kuwafanya hawa ombaomba hela wanazopata wawekeze katika kazi za kawaida na halali .


Kuna watu ni walemavu na wapo broke Ila hawawezi kuomba omba mtaani then serikali itoe zaidi elimu kuhusu wat u kujitambua.
Mostly of the street beggars are homeless and street children. Kuna gepu jembamba sana kati ya kuntofautisha mtoto wa mitaani na ombaomba. Pia ombaomba imefungamana na ulemavu wa akili/ UKOSEFU WA utimamu wa akili. Although Kuna wengine wanaombaga chakula tu!.

Naungana na hoja yako mkuu, nimejaribu kuwind up our stance. Tuendeleze mjadala mana waziri yupo karibu na sisi hapa
 
Back
Top Bottom