Waziri Gwajima: Nawapongeza sana Mbeya kwa ujenzi wa jengo la kisasa la wajawazito, Leo nimefurahi sana!

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Waziri wa Afya Dr Gwajima ameupongeza mkoa wa Mbeya kwa ujenzi wa jengo la kisasa la wajawazito.

Dr Gwajima amesema LEO amefurahi sana.

Waziri wa Afya yuko ziarani mkoani Mbeya akikagua shughuli mbalimbali za wizara yake.

Source Upendo tv

Maendeleo hayana vyama!
 
Aiseeee nilijua atajipongeza yeye kwa kujenga barabara na ofisi za jimbo la kawe.
 
Mkoa wa mbeya umenyanyapaliwa na Awmu toka ya Mkapa na ni kwa muda mrefu.
Hakuna miradi mikubwa ya maendeleo na barabara za kuingia mjini ni masikitikao.
Pengine Awau hii ijitahidi kuondoa tatizo hilo.
 
Bi Tukinao on fleek
 
Nini jengo la kisasa la wajawazito?
 
Mkoa wa mbeya umenyanyapaliwa na Awmu toka ya Mkapa na ni kwa muda mrefu.
Hakuna miradi mikubwa ya maendeleo na barabara za kuingia mjini ni masikitikao.
Pengine Awau hii ijitahidi kuondoa tatizo hilo.
Ni ukweli mtupu yaani Mji ukiingia mpaka unasikitika, barabara zingine kama maandaki. Ukija Mbeya utdhani uko enzi za Mwinyi Tz ilivyokuwa. Sijui walikosea wapi. Wananchi wenyewe wanajitahidi bila jicho la kutoka juu,nimetembelea wilaya ya Rungwe kwakweli nimeshangaa kidogo kunamaendeleo nimeona nyumba za kisasa na kuna baadhi huwezi amini kama unaweza kutegemea kukuta vijijini nyumba kama zile kweli shemeji zangu hapo wamejitahidi sana, sikubahatika kufika mpaka kyela na Wilaya zingine bila shaka nako kuko vizuri lakini Jiji la Mbeya bado serikali inapaswa kuwapa nao keki ya Taifa.
 
Huyo mama nimemwondoa kabisa katika watu wa maana nchi hii. Aheri kumsikiliza Musukuma kuliko huyu mama.

Daktari mzima anaendekeza mambo ya nyungu, ujinga ambao hauna uthibitisho wa kisayansi, tena kwa nadharia ya kisayansi (nyungu) inaongezea tatizo la mgonjwa wa covid kujaa mapafu maji.

Siku huyu mama akiugua covid asipewe tiba yoyote, apelekwe kwenye nyungu.

Daktari mzima anaacha taaluma na kushabikia tiba za wale waganga washirikina wa usukumani wanaofuga fisi, eti ndiyo vyombo vya usafiri na viumbe vya kuwaletea nyama nyumbani.

Wanataka kuligeuza Taifa zima liache tiba za kisayansi, wageukie ushirikina.

Nadhani leo mmemsikia DC wa Nyang'wale akielezea shida kubwa ya fisi wanaofugwa na wasukuma kishirikina wanavyotishia mifugo na binadamu, na eti sasa wameomba timu ya wataalam wa jadi (maana yake wenye uchawi zaidi) toka Shinyanga, na kwamba kwa msaada wao, tayari wameua fisi 28. Huko ndiko usukumani ambako Gwajima anataka Watanzania wote watumie hizo tiba za kishirikina kutoka kwenye mazingira aliyokulia.
 
So what
 
Masikini Daktari Dorothy Gwajima, MB, na Waziri wa Afya.
Alianza vuzuri. Mbwembwe na machachari yake yakaziteka nyoyo za Watanzania.
Likaja wimbi la pili la Covid-19!
Akatepeta! Akalowa! Akageuka Mganga wa Kienyeji, Toboa Tobo! Akasahau viapo vyake vya Udaktari.
Sasa amebaki ni Mpiga debe za kisiasa na mpiga ramli za nyungu, malimau, vitunguu swaumu na tangawizi.
Sijui aliyasoma hayo mwaka wa ngapi Chuo Kikuu cha Udaktari!!!
Masikini Dk. Dorothy Gwajima!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…