Waziri Gwajima: Wanaume mnajitengenezea ‘stress’, punguzeni wivu

Waziri Gwajima: Wanaume mnajitengenezea ‘stress’, punguzeni wivu

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Waziri Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima amewataka baadhi ya wanaume ambao bado wana mfumo dume wa kunyanyasa wanawake kuacha tabia hiyo hasa kwenye masuala ya uchumi.

Dkt. Gwajima ameyasema hayo mjini Morogoro Wakati akizungumza kwenye Kongamano ambalo limewakutanisha wanawake Zaidi ya 150 kutoka katika mikoa tofati ambalo liliandaliwa na taasisi binafsi inayoitwa Ladies Talk.

Dkt. Gwajima amesema kumekuwa na ongezeko la wajane nchini kwa sababu wanaume wanapoteza maisha kuliko wanaume huku akieleza kuwa baadhi ya sababu hizo ni vifo vinavyotokana na wivu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa taaisisi hiyo ya Ladies Talk Salome Sengo amesema lengo la kongamano hilo ni kuwakutanisha wanawake pamoja ili waweze kutangaza biashara zao ikiwa ni pamoja na kupata elimu ya ujasiriamali.
 
Vikao kama hivyo sijui kwa nini huwa najua vikiwa vimeshapita, nikiviotea huwa natafuta bar ya karibu nakaa huku macho yote yapo kwenye lango lao la kutokea nasubiria wakati wangu nijiokotee na hao wanaharakatiharakati ndio huwa nawapenda sana.
 
Kwani hiyo seminar ilikuwa ya wababa au ya wamama? Au ana stress za home?
 
Waziri Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima amewataka baadhi ya wanaume ambao bado wana mfumo dume wa kunyanyasa wanawake kuacha tabia hiyo hasa kwenye masuala ya uchumi...
Waziri Gwajima Wewe mwenyewe una stress Hata uvaaji wako Sio rahisi handsome boy aombe Hata namba yako ya simu.
 
Demokrasia gani wakati unawabagaza wabunge wanawake kwa kuwaita covid 19? Fujo zote hizo anapiganiwa joyce mukya awe mbunge
We mjane yule mchawi kaharibu sana akili yako kiasi cha kutokuolewa tena... umechanganyikiwa hadi unaandika usichokielewa.
 
Back
Top Bottom