Waziri Innocent Bashungwa: Wasafi TV wanajutia kosa, wameomba msamaha na kuonesha nia ya kusimamia yasijirudie

Waziri Innocent Bashungwa: Wasafi TV wanajutia kosa, wameomba msamaha na kuonesha nia ya kusimamia yasijirudie

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
Wasafi Tv wanajutia kosa, wameomba msamaha na kuonesha nia ya kusimamia yasijirudie, Wizara inaendelea na jitihada za kuona hili linapata mwelekeo utakaolinda ajira zilizozalishwa, uwekezaji uliofanyika bila kuvunja sheria za Nchi"-Waziri wa Habari Innocent Bashungwa

Taarifa: Darmpya Blog
Hatimaye Waziri wa Habari Mh Bashungwa ameanza mchakato wa kuifungulia Wasafi TV iliyofungiwa na TCRA kwa utovu wa maadili baada ya kumruhusu anayejiita Giggy Money mtoto wa Lisalisa kucheza bila nguo kwenye tamasha lao .

Wiki iliyopita TCRA iliifungia WASAFI TV kwa miezi 6 .

Sababu za mchakato huo zilizotolewa na Bashungwa hazina mashiko kwa vile vyombo vyote vilivyofungiwa na TCRA ikiwemo Kwanza Tv , Gazeti la MwanaHalisi , Mawio na TanzaniaDaima vilikuwa vimeajiri wafanyakazi kama ilivyofanya WASAFI TV lakini vimefungiwa moja kwa moja hadi sasa .

Ni vema Waziri akaweka wazi kwamba amepokea Amri kutoka mahali pengine ili kuifungulia Wasafi TV kwa vile ni wadau wa kampeni zilizododa za ccm kwenye uchaguzi mkuu wa 2020 , ikumbukwe kwamba Diamond Platnums ndiye alikuwa anaendesha kampeni za ccm huku chama chake kikikosa sera za kuwaambia wananchi baada ya kuendelelea kuwa masikini wa kutupwa kwa miaka 60 , hii ni kwa sababu aliyeshindwa jambo kwa muda mrefu wa miaka 60 hawezi kulitatua jambo lilelile kwa miaka mitano .
 
Wasafi Tv wanajutia kosa, wameomba msamaha na kuonesha nia ya kusimamia yasijirudie, Wizara inaendelea na jitihada za kuona hili linapata mwelekeo utakaolinda ajira zilizozalishwa, uwekezaji uliofanyika bila kuvunja sheria za Nchi"-Waziri wa Habari
@innobash

Taarifa: Darmpya Blog
Mwenyekiti wao Leo utamuona na Makamera Kanisani akiuza sura. Mungu hadhihakiwi.
 
Nchi uongozwa kwa mujibu wa katiba,sheria,kanuni,hekima na busara. Nionyeshe kitabu kilichoandikwa cha hekima na busara.
Hivyo basi ni mtazamo ( hekima na busara) ya mfanya maamuzi kuona hatua anazoweza kuchukua katika jambo fulani katika muktadha husika.
Hata ingekuwa mimi kwa mchango wa Diamond katika "mambo ya msingi" ningeangalia namna ya kusaidia "empire" yake isianguke kuliko kukusikiliza wewe mtoa "povu" kuhusu chuki zako dhidi ya Serikali ya CCM.
 
Nashani tungeanzia kwenye sheria sio adhabu. Tukianzia kwenye adhabu ni kama tunampa nafasi waziri mwenye dhamana kuamua kulingana na jinsi alivyoamka siku hiyo.
Nakubaliana na wewe 100%
 
FB_IMG_1610272991837.jpg


Hatimaye Waziri wa Habari Mh Bashungwa ameanza mchakato wa kuifungulia Wasafi TV iliyofungiwa na TCRA kwa utovu wa maadili baada ya kumruhusu anayejiita Giggy Money mtoto wa Lisalisa kucheza bila nguo kwenye tamasha lao .

Wiki iliyopita TCRA iliifungia WASAFI TV kwa miezi 6 .

Sababu za mchakato huo zilizotolewa na Bashungwa hazina mashiko kwa vile vyombo vyote vilivyofungiwa na TCRA ikiwemo Kwanza Tv , Gazeti la MwanaHalisi , Mawio na TanzaniaDaima vilikuwa vimeajiri wafanyakazi kama ilivyofanya WASAFI TV lakini vimefungiwa moja kwa moja hadi sasa .

Ni vema Waziri akaweka wazi kwamba amepokea Amri kutoka mahali pengine ili kuifungulia Wasafi TV kwa vile ni wadau wa kampeni zilizododa za CCM kwenye uchaguzi mkuu wa 2020 , ikumbukwe kwamba Diamond Platnums ndiye alikuwa anaendesha kampeni za ccm huku chama chake kikikosa sera za kuwaambia wananchi baada ya kuendelelea kuwa masikini wa kutupwa kwa miaka 60 , hii ni kwa sababu aliyeshindwa jambo kwa muda mrefu wa miaka 60 hawezi kulitatua jambo lilelile kwa miaka mitano .
 
Back
Top Bottom