Waziri Jafo amuondoa kwenye nafasi yake Meneja wa TARURA jijini Arusha kwa kushindwa kuita Wananchi kushuhudia ufunguzi wa barabara

Inaonekana mhandisi huyu alitafutwa yangu awali, bila shaka utendaji wake hauridhishi.
 
Ndo umejifunza wapi hayo???

Hivi ulikuwa unajua kazi ya tume ya mipango?? Unajua pia kuwa saivi imeamishiwa wizara ya fedha??! Unajua wanafanyaga nini??!!
Tume ya mipango haikai tu na kuota kuwa tupange nini .hAWAINUI TU VICHWA HEWANI na kuja na mawazo toka angani kuwa tupange hivi!!

Yote huanzia kwenye chama kupitia ilani ambayo Raisi hukabidhiwa na chama kama mwenyekiti wa CCM taifa.Akishakabidhiwa yeye hukabidhi kwa wataalamu wake wachote humo waende nayo kutengeneza mipango ya taifa ndipo utaanza kuona mpango wa taifa unaibuka na lazima uwe na allignment na ilani ya chama tawala na sera zake ila kwa wewe karani ofisi ya mipangio huwezi jua origin yake sababu wewe ni mtu wa chini sana kwenye utendaji wewe unatupiwa tu kuwa brain storm from here!!
 
Hii ndio sababu ya kumtoa mtu kazini.......this is Insane....Nonsense
Huo ndo ubaya mtu anahukumiwa bila hata ya kusikilizwa so sad ukweli ni kuwa haikutakiwa ifike hatua hiyo sometimes viongozi wetu inabidi wawe humble na wajue namna gani kudeal na watu ukali na maamuzi magumu hayakufanyi kuwa kiongozi bora bali itakufanya kuwa adui ya wale unaowasimamia
 
Kwa iyo kwa akili yako unadhani tume ya mipango inasubirigi ilani ya Chama na ndo inapanga mipango???

Usiku mwema mzee.
 
Akafungue nyingine aone kama sisi wananchi tutakuja.Kwanza tutakuja kufanya nini saa za kazi.Ni kweli huu ni ukatili na uonevu mbaya.Taratibu za kumsimamisha kazi mtumishi wa umma Tanzania jamani ziko wapi? Sasa hivi ni kufukuzana kazi tu bila kujali utu wa mtumishi wa Umma.

Wizara ya kazi Utumishi,mko wapi,mtumishi huyu ana haki zote za utumishi kama alivyo waziri.Kama kakosea,kuna utaratibu wa kufuata ambao Serikali ya Mh.Dr.Mwal.Julius Kambarage Nyerere aliheshimu na kuufuata kwa nguvu zake zote lakini leo hii ni ubabe tu.Hii ni Tanzania ya wapi,Uonevu mtupu.

Kwanza tunashangaa sana kilichotokea,barabara ni kodi zetu,ni haki yetu kuwa na barabara nzuri,tumeshazitumia zote,unataka tuje kuimbia barabara iliyotengenezwa kwa kodi zetu ili iweje.Uonevu huu hata Mungu hapendi.

Huyu meneja sio mwanasiasa,yeye ni mtaalamu.Kazi ya kutuita sisi wananchi sio yake.Hii ni kazi ya balozi wa nyumba kumi akishirikiana na mwenyekiti wa mtaa.Na hata kama angekuja kutuita tuone barabara ikifunguliwa tungemuuliza,kwani ilifungwa lini.Siku zote si ipo tu.Labda ifungwe kwanza kwa miezi kadhaa,halafu ije ifunguliwe ndo watuambie tukaone ile iliyofungwa inafunguliwa tungewaelewa kidogo.Lakini barabara tunapita kila siku leo corona imetuachia umaskini tuache kutafuta ada ya mtoto ya shule tuje? kuona barabara za lami.Inasikitisha sana sana.Tenda haki ili taifa liinuke.Haki huinua taifa.
 
Duh, kazi hizi ngumu sana, ingefaa huyu mtendaji wa TARURA afanye mawasiliano ya kutosha nini na nini atahitaji waziri kabla ya kufika site. Nadhani hakukuwa na mawasiliano mazuri kabla
 
Kwa iyo kwa akili yako unadhani tume ya mipango inasubirigi ilani ya Chama na ndo inapanga mipango???
siku ukiwa vyeo vikubwa utaelewa mipango huanzia wapi kwa sasa endelea na u karani tume ya mipango
 
jiji la Arusha ni busy city sio rahisi mwananchi ambaye sio mwanasiasa aache kazi zake aende kushangilia barabara labda waliowaangusha ni hao hao CCM hamkutoka kwenda kushangilua
 
Kwa nini Buhigwe ?? Kwanini Kakonko?? kwanini isiwe Kisarawe?... Hii ina maana huko anakopelekwa huyo Meneja wananchi wake hawataki maendeleo?.. Hapa,kwa maoni yangu Jafo anapaswa kuwaomba radhi wananchi wa Buhigwe na Kakonko. 🤔 😳
 
Siendi tena kusoma kwakweli
 

Unamtumbuaje mtu kisa hajaweza kuwakusanya watu waje washangae barabara, hizo ni akili au.

Anyway muda unayoyoma aendelee kuzunguka huku na kule kumsifia mwanaume mwenzake ili jamaa akiamka siku hiyo hasije akalisahau jina lake.
 
Hivi kazi ya kusomba wananchi ya nani , Mkurugenzi au meneja wa TARURA??.
Huyo meneja angepata wapi magari ya kusomba wanaCCM, Na je wananchi wangekataa kwenda ingekuwaje!!,.Kwa sababu ARUSHA watu wako bize saaana tofauti na watu wa kanda ya ziwa.
 
Kwani hao wananchi hawaoni jamani hizo barabara? Sasa barabara utaifichaje? Halafu meneja kazi yake ni kuhakikisha kazi imefanyika kwa kiwango. Siyo kukusanya wananchi. Hii serikali ya sifa, hii...! Ngoja nikazane na biashara zangu tu.
Yaani jafo huwa anaonekana ni mtu smart kumbe nae hamna kitu.
 

Meneja TARURA Biharamulo na Ngara ambako barabara kuu kwenda Ngara na Rusumo haipitiki wangali bado ofisini?
 
Kwa sasa inawezeka tunasoma upepo na iwapo utaendelea kuvuma vibaya,basi wewe ndio unaweza kushughliliwa kwa kuondolewa hapo ulipo na huyo Meneja akarudishwa katika nafasi yake mara moja tena na pengine hata akapandishwa cheo.

Kipindi hiki ni kipindi cha uchaguzi, hivyo hakuna mwanasiasa anaetaka kujiaribia au kuaribiwa kwa makosa ya mwingine.

Unaweza kuamka na kukutana na Press release mitandaoni kuwa umetenguliwa.
 
siku ukiwa vyeo vikubwa utaelewa mipango huanzia wapi kwa sasa endelea na u karani tume ya mipango
Karibu Ruvuma tufanye kilimo ingawa sera za Chama chako kimenifanya nikose hela kwa kuzuia mahindi kuuzwa nje.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…