Waziri Jerry Silaa, kwanini hushughuliki na maafisa ardhi? Jifunze kutoka Libya ya Gaddafi pia

Waziri Jerry Silaa, kwanini hushughuliki na maafisa ardhi? Jifunze kutoka Libya ya Gaddafi pia

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Katika muendelezo wa kile waziri wa ardhi Jerry Silaa anachokiita kliniki ya ardhi na kutatatua changamoto za ardhi ameendelea kupuuza kabisa documents/nyaraka halali za serikali na mahakama za wale wanaodaiwa kuwa ni wavamazi au wanunuzi matapeli waliojimilikisha ardhi za watu wengine. Yani mtu ana hati yake halali ya umiliki kutoka serikalini anakuaje mvamvizi au tapeli wa kiwanja?!

Kwanza, swali la kwanza ni kwa vipi serikali inaweza kutoa hati zaidi ya moja kwa watu tofauti kwa eneo lile lile?

Pili, ni kwa nini hatuoni ukiwawajibisha maafisa ardhi na kamishna wa ardhi kwa namna yeyote ile tangu umeanza harakati zako?

Tatu, kuna maana gani sasa ya kwenda mahakamani kama waziri ndiye amegeuka kuwa mgawa haki?

Waziri Silaa anapaswa kujifunza kidogo katika iliyokuwa Libya ya Gaddafi, wakati Gaddafi akitawala Libya alianzisha sera ya kwamba umiliki haki na makazi ni mojawapo ya haki za msingi za kibinadamu za raia wote wa Libya. Sera aliipeleka vibaya sana kwa misingi ya kuwapa wanyonge makazi. Aliitaabishia, kuikatisha tamaa na kuifanyia vurugu makusudi biashara ya ardhi na makazi libya mpaka biashara ya real estate ikawa kama haipo kabisa.

Kwa sababu ya serikali kutoheshimu na kutotilia maanani nyaraka Ilikuwa ni kawaida wamiliki wa nyumba kuuza au kukodisha nyumba zao halafu baadaye wanageuka wanasema wamedhulimiwa. Waliokuwa wanyonge walikuwa wanavizia watu wenye nyumba zao wanaposafiri wote wanavamia nyumba wanavunja wanaigeuza ya kwao, mkirudi mnakuta nyumba ina watu wengine na haijalishi kama mna documents za kuthibitisha umiliki wenu nyumba au kiwanja mnaweza msipate tena, wao utetezi wao ni huo wa unyonge na haki ya kuwa na makazi, zaidi sana ukiwa tajiri mwenye nyumba nyingi ndio hakuna utakachoambulia kabisa wanyonge watakapodai baadhi ya nyumba yako.

Pamoja na matatizo makubwa yaliyopo katika sekta ya ardhi na makazi nchini, Jerry Silaa anapaswa kwanza kushughulika na mambo ya msingi ambao ni mfumo wa ardhi kuruhusu document za serikali zaidi ya moja kwa watu tofauti, maafisa ardhi na wengine wa serikali wanaotoa hizo nyaraka na pia aheshimu mahakama kama mtoaji haki wa mwisho, anachoweza kufanya yeye au serikali kusaidia ni kuzifanya mahakama zitoe maamuzi kwa haraka na kuwasaidia wanasheria wananchi wanaodai kudhulimiwa.
 
UKO SAHIHI, lakini kuna mambo mengine kuyatafutia ufumbuzi ni sahihi.

Kuna kama hili hapa la tanga, tafuta clip uisikilize Mmasy kasindwa kesi high court, hataki kutoka kwenye nyumba. anasema amekata rufani, sawa lkn kukata rufani hakuzuii mshindi kupata haki yake.
Kwa ruhusa ya mwandishi nakuwekea hapa, isome , very interesting

 
UKO SAHIHI, lakini kuna mambo mengine kuyatafutia ufumbuzi ni sahihi.
Kuna kama hili hapa la tanga, tafuta clip uisikilize Mmasy kasindwa kesi high court, hataki kutoka kwenye nyumba. anasema amekata rufani, sawa lkn kukata rufani hakuzuii mshindi kupata haki yake.
Kama waziri anagawa haki kesi zikiwa mahakani, kinyume na maamuzi ya mahakama na nyaraka za serikali kwa nini yeye Mmasy aiheshimu mahakama?! Kuna kesi nyingine nayo huko Arusha ya mtu mmoja anaitwa Monaban Mollel ambapo amaeshindwa hadi mahakama ya rufaa lakini hataki kuachia kiwanja.
 
Kwanza, swali la kwanza ni kwa vipi serikali inaweza kutoa hati zaidi ya moja kwa watu tofauti kwa eneo lile lile?

Pili, ni kwa nini hatuoni ukiwawajibisha maafisa ardhi na kamishna wa ardhi kwa namna yeyote ile tangu umeanza harakati zako?
Naunga mkono hoja 100%.
Kama atawaacha makamishna wasaidizi na kamishna mkuu na watendaji wengine ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.
Kuna kesi za ardhi kwa makumi elfu. Cha muhimu ni kuondoa loopholes na kuja na mfumo bora wa umilikishwaji.
 
MAMANGU ALISHNDA KESI YAKE YA ARDHI HADI MAHAKAMA KUU.LAKINI MPAKA LEO HAJAPATA ARDHI YAKE.MAHAKAMA YA ARDHI NI UPUUZ
 
MAMANGU ALISHNDA KESI YAKE YA ARDHI HADI MAHAKAMA KUU.LAKINI MPAKA LEO HAJAPATA ARDHI YAKE.MAHAKAMA YA ARDHI NI UPUUZ
Kama mtu amejenga, muichome nyumba moto. Huwezi kushtakiwa kwa sababu unasafisha kiwanja chako.
 
Katika muendelezo wa kile waziri wa ardhi Jerry Silaa anachokiita kliniki ya ardhi na kutatatua changamoto za ardhi ameendelea kupuuza kabisa documents/nyaraka halali za serikali na mahakama za wale wanaodaiwa kuwa ni wavamazi au wanunuzi matapeli waliojimilikisha ardhi za watu wengine. Yani mtu ana hati yake halali ya umiliki kutoka serikalini anakuaje mvamvizi au tapeli wa kiwanja?!

Kwanza, swali la kwanza ni kwa vipi serikali inaweza kutoa hati zaidi ya moja kwa watu tofauti kwa eneo lile lile?

Pili, ni kwa nini hatuoni ukiwawajibisha maafisa ardhi na kamishna wa ardhi kwa namna yeyote ile tangu umeanza harakati zako?

Tatu, kuna maana gani sasa ya kwenda mahakamani kama waziri ndiye amegeuka kuwa mgawa haki?

Waziri Silaa anapaswa kujifunza kidogo katika iliyokuwa Libya ya Gaddafi, wakati Gaddafi akitawala Libya alianzisha sera ya kwamba umiliki haki na makazi ni mojawapo ya haki za msingi za kibinadamu za raia wote wa Libya. Sera aliipeleka vibaya sana kwa misingi ya kuwapa wanyonge makazi. Aliitaabishia, kuikatisha tamaa na kuifanyia vurugu makusudi biashara ya ardhi na makazi libya mpaka biashara ya real estate ikawa kama haipo kabisa.

Kwa sababu ya serikali kutoheshimu na kutotilia maanani nyaraka Ilikuwa ni kawaida wamiliki wa nyumba kuuza au kukodisha nyumba zao halafu baadaye wanageuka wanasema wamedhulimiwa. Waliokuwa wanyonge walikuwa wanavizia watu wenye nyumba zao wanaposafiri wote wanavamia nyumba wanavunja wanaigeuza ya kwao, mkirudi mnakuta nyumba ina watu wengine na haijalishi kama mna documents za kuthibitisha umiliki wenu nyumba au kiwanja mnaweza msipate tena, wao utetezi wao ni huo wa unyonge na haki ya kuwa na makazi, zaidi sana ukiwa tajiri mwenye nyumba nyingi ndio hakuna utakachoambulia kabisa wanyonge watakapodai baadhi ya nyumba yako.

Pamoja na matatizo makubwa yaliyopo katika sekta ya ardhi na makazi nchini, Jerry Silaa anapaswa kwanza kushughulika na mambo ya msingi ambao ni mfumo wa ardhi kuruhusu document za serikali zaidi ya moja kwa watu tofauti, maafisa ardhi na wengine wa serikali wanaotoa hizo nyaraka na pia aheshimu mahakama kama mtoaji haki wa mwisho, anachoweza kufanya yeye au serikali kusaidia ni kuzifanya mahakama zitoe maamuzi kwa haraka na kuwasaidia wanasheria wananchi wanaodai kudhulimiwa.
MATATIZO UNAYOHANGAIKA NAYO MENGI YAMEFANYWA NA WATENDAJI WAKO KWA KUSHIRIKIANA NA HAO MATAPELI
 
Katika muendelezo wa kile waziri wa ardhi Jerry Silaa anachokiita kliniki ya ardhi na kutatatua changamoto za ardhi ameendelea kupuuza kabisa documents/nyaraka halali za serikali na mahakama za wale wanaodaiwa kuwa ni wavamazi au wanunuzi matapeli waliojimilikisha ardhi za watu wengine. Yani mtu ana hati yake halali ya umiliki kutoka serikalini anakuaje mvamvizi au tapeli wa kiwanja?!

Kwanza, swali la kwanza ni kwa vipi serikali inaweza kutoa hati zaidi ya moja kwa watu tofauti kwa eneo lile lile?

Pili, ni kwa nini hatuoni ukiwawajibisha maafisa ardhi na kamishna wa ardhi kwa namna yeyote ile tangu umeanza harakati zako?

Tatu, kuna maana gani sasa ya kwenda mahakamani kama waziri ndiye amegeuka kuwa mgawa haki?

Waziri Silaa anapaswa kujifunza kidogo katika iliyokuwa Libya ya Gaddafi, wakati Gaddafi akitawala Libya alianzisha sera ya kwamba umiliki haki na makazi ni mojawapo ya haki za msingi za kibinadamu za raia wote wa Libya. Sera aliipeleka vibaya sana kwa misingi ya kuwapa wanyonge makazi. Aliitaabishia, kuikatisha tamaa na kuifanyia vurugu makusudi biashara ya ardhi na makazi libya mpaka biashara ya real estate ikawa kama haipo kabisa.

Kwa sababu ya serikali kutoheshimu na kutotilia maanani nyaraka Ilikuwa ni kawaida wamiliki wa nyumba kuuza au kukodisha nyumba zao halafu baadaye wanageuka wanasema wamedhulimiwa. Waliokuwa wanyonge walikuwa wanavizia watu wenye nyumba zao wanaposafiri wote wanavamia nyumba wanavunja wanaigeuza ya kwao, mkirudi mnakuta nyumba ina watu wengine na haijalishi kama mna documents za kuthibitisha umiliki wenu nyumba au kiwanja mnaweza msipate tena, wao utetezi wao ni huo wa unyonge na haki ya kuwa na makazi, zaidi sana ukiwa tajiri mwenye nyumba nyingi ndio hakuna utakachoambulia kabisa wanyonge watakapodai baadhi ya nyumba yako.

Pamoja na matatizo makubwa yaliyopo katika sekta ya ardhi na makazi nchini, Jerry Silaa anapaswa kwanza kushughulika na mambo ya msingi ambao ni mfumo wa ardhi kuruhusu document za serikali zaidi ya moja kwa watu tofauti, maafisa ardhi na wengine wa serikali wanaotoa hizo nyaraka na pia aheshimu mahakama kama mtoaji haki wa mwisho, anachoweza kufanya yeye au serikali kusaidia ni kuzifanya mahakama zitoe maamuzi kwa haraka na kuwasaidia wanasheria wananchi wanaodai kudhulimiwa.
Akishughurika nao migogoro itaisha atakosa kiki
 
Japo anakosea lakini kuna wakati ili mambo yaende lazima uachane na principles of laws maana hizi sheria zimewekwa na wanadamu zinaweza kukosewa na mhalifu akatumia hiyo loophole kunyang'anya haki ya mtu.
 
Jerry Slaa position yake ni ya kisiasa, sio mtendaji wa Wizara....ipo siku yaja utaelewa.

Anakosea ktk utendaji wake...[emoji41]
Hata kama position yake ni ya kisiasa,lakini si anakua na team nzima ya Watendaji kuanzia Commissioner wa Aridhi hadi Msajili wa Hati kwenye clinic yake!!??
 
Hata kama position yake ni ya kisiasa,lakini si anakua na team nzima ya Watendaji kuanzia Commissioner wa Aridhi hadi Msajili wa Hati kwenye clinic yake!!??
Hao wapuuzi wanaomlalamikia waziri ni kwasababu hawajawahi dhulumiwa au hawaijui Tanzania vizuri. Mtu ananunua kiwanja kina mgogoro wa urithi, anatoa ela kabisa bila kuwaona warithi wote halafu baadae anakimbilia mahakamani, kesi kama hiyo Kuna aja ya ku deal na afisa ardhi yoyote!?,si ni uzembe wa mnunuzi?
 
Japo anakosea lakini kuna wakati ili mambo yaende lazima uachane na principles of laws maana hizi sheria zimewekwa na wanadamu zinaweza kukosewa na mhalifu akatumia hiyo loophole kunyang'anya haki ya mtu.
Kama sheria zimekosewa au ni dhaifu ni vyema zikabadilishwa badala ya kufanya mambo kienyeji nje ya utawala wa sheria.
 
Hao wapuuzi wanaomlalamikia waziri ni kwasababu hawajawahi dhulumiwa au hawaijui Tanzania vizuri. Mtu ananunua kiwanja kina mgogoro wa urithi, anatoa ela kabisa bila kuwaona warithi wote halafu baadae anakimbilia mahakamani, kesi kama hiyo Kuna aja ya ku deal na afisa ardhi yoyote!?,si ni uzembe wa mnunuzi?
Hakuna sheria inayosema ukitaka kununua mali ya urithi lazima uwaone warithi wote.
 
Hakuna sheria inayosema ukitaka kununua mali ya urithi lazima uwaone warithi wote.
Hujui usemalo, ndo maana ukaanzisha thread. Waziri kaelezea hiyo sheria mara nyingi kwenye hiyo ziara yake refer Ile kesi ya ghorofa la lenye WAKFU Kariakoo. Ila ukimsikiliza ukiwa umejaa chuki hutamuelewa au pengine wewe ni moja ya matapeli wa ardhi. Ukitaka kununua ardhi ya urithi yoyote watafute warithi wote upate uhakika kama wameridhia kuuza, uki deal na kaka yao mkubwa au msimamizi wao inaweza kula kwako. By the way, toa mfano mmoja kwenye ziara za waziri alipokosea kutoa haki.
 
Hujui usemalo, ndo maana ukaanzisha thread. Waziri kaelezea hiyo sheria mara nyingi kwenye hiyo ziara yake refer Ile kesi ya ghorofa la lenye WAKFU Kariakoo. Ila ukimsikiliza ukiwa umejaa chuki hutamuelewa au pengine wewe ni moja ya matapeli wa ardhi. Ukitaka kununua ardhi ya urithi yoyote watafute warithi wote upate uhakika kama wameridhia kuuza, uki deal na kaka yao mkubwa au msimamizi wao inaweza kula kwako. By the way, toa mfano mmoja kwenye ziara za waziri alipokosea kutoa haki.
Msimamizi wa mirathi anaweza kuuza mali bila kuwashirikisha warithi wote.
 
Msimamizi wa mirathi anaweza kuuza mali bila kuwashirikisha warithi wote.
Sawa, kila mtu abakie anavyojua. Inaonekana hujawahi kuona mgogoro wowote wa nyumba ya urithi, na hujui neno tamaa,ujanja,utapeli nk. Au upo hapa kwa ajili ya ubishi tu. Hakuna tajiri mwenye akili timamu ataenda kununua nyumba ya urithi tena kwa ela nyingi bila kuwaona warithi. Aidha elimu yake ndogo, au ni mtu wa migogoro au anaamini ushirikina. Naamini hata wewe huwezi ila upo hapa kuleta ligi tu.
 
Back
Top Bottom