Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Waziri Kombo alisema sekta ya uchukuzi ni moja ya sekta muhimu katika maendeleo ya nchi na anaona sekta hiyo ina nafasi kubwa ya kupiga hatua kupitia ushirikiano na Czech.
Wamesisitiza umuhimu wa mataifa yao kusaini Mkataba wa anga ili kuanzisha safari za ndege za moja kwa moja baina ya nchi zao ili kuinua biashara, utalii na mwingiliano wa watu.
Waziri Kombo alipongeza pia kampuni ya Skoda Electric kwa kufunga mfumo wa umeme wa kisasa kwenye uendeshaji wa reli ya SGR nchini.