Waziri Kombo ashiriki maadhimisho ya miaka 107 ya uhuru wa Finland

Waziri Kombo ashiriki maadhimisho ya miaka 107 ya uhuru wa Finland

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,278
Reaction score
797
WAZIRI KOMBO ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 107 YA UHURU WA FINLAND

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (Mb) ameshiriki sherehe ya Maadhimisho ya miaka 107 ya Uhuru wa Taifa hilo iliyoandaliwa na Ubalozi wa Finland hapa nchini.

Akizungumza katika sherehe za maadhimisho hayo Waziri Kombo aliyealikwa kama Mgeni Rasmi licha ya kuipongeza Serikali ya Finland kwa kuendelea kulinda Uhuru wake na kudumisha amani na usalama pia, amepongeza hatua ya maendeleo ya kiuchumi iliyofikiwa na Taifa hilo.

Aidha, Mheshimiwa Waziri aliongeza kuwa Tanzania itaendelea kudumisha na kukuza mahusiano ya kidiplomasia yaliyodumu kwa muda mrefu baina ya mataifa haya mawili kwa manufaa ya watu wake.

Kwa upande wake Balozi wa Finland hapa nchini Mhe. Theresa Zitting amesema Serikali ya Finland itaendelea kutumia matunda ya Uhuru wake kukuza mahusiano mazuri ya Kidiplomasia yaliyopo baina yake na Mataifa mengine ulimwenguni.

Sherehe za Maadhimisho hayo ambazo zimefanyika katika Makazi ya Balozi wa Finland Masaki jijini Dar es Salaam zimehudhuriwa na Mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini.

Finland ilipata Uhuru wake Disemba 6, 1917
 

Attachments

  • mini_magick20241208-31781-hi4bo.jpg
    mini_magick20241208-31781-hi4bo.jpg
    73.3 KB · Views: 2
  • mini_magick20241208-31781-8x1pof.jpg
    mini_magick20241208-31781-8x1pof.jpg
    80.6 KB · Views: 3
  • mini_magick20241208-31781-hrn9j0.jpg
    mini_magick20241208-31781-hrn9j0.jpg
    50.5 KB · Views: 5
  • mini_magick20241208-31781-d9lzcv.jpg
    mini_magick20241208-31781-d9lzcv.jpg
    91.1 KB · Views: 3
  • mini_magick20241208-31781-hajv1v.jpg
    mini_magick20241208-31781-hajv1v.jpg
    134 KB · Views: 3
  • mini_magick20241208-31781-4z899t.jpg
    mini_magick20241208-31781-4z899t.jpg
    88.7 KB · Views: 4
  • mini_magick20241208-31781-dez2om.jpg
    mini_magick20241208-31781-dez2om.jpg
    93 KB · Views: 5
  • mini_magick20241208-31781-2eghac.jpg
    mini_magick20241208-31781-2eghac.jpg
    81.5 KB · Views: 3
  • mini_magick20241208-31781-s9inmr.jpg
    mini_magick20241208-31781-s9inmr.jpg
    91 KB · Views: 4
  • mini_magick20241208-31781-ypzv9j.jpg
    mini_magick20241208-31781-ypzv9j.jpg
    51.5 KB · Views: 4
WAZIRI KOMBO ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 107 YA UHURU WA FINLAND

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (Mb) ameshiriki sherehe ya Maadhimisho ya miaka 107 ya Uhuru wa Taifa hilo iliyoandaliwa na Ubalozi wa Finland hapa nchini.

Akizungumza katika sherehe za maadhimisho hayo Waziri Kombo aliyealikwa kama Mgeni Rasmi licha ya kuipongeza Serikali ya Finland kwa kuendelea kulinda Uhuru wake na kudumisha amani na usalama pia, amepongeza hatua ya maendeleo ya kiuchumi iliyofikiwa na Taifa hilo.

Aidha, Mheshimiwa Waziri aliongeza kuwa Tanzania itaendelea kudumisha na kukuza mahusiano ya kidiplomasia yaliyodumu kwa muda mrefu baina ya mataifa haya mawili kwa manufaa ya watu wake.

Kwa upande wake Balozi wa Finland hapa nchini Mhe. Theresa Zitting amesema Serikali ya Finland itaendelea kutumia matunda ya Uhuru wake kukuza mahusiano mazuri ya Kidiplomasia yaliyopo baina yake na Mataifa mengine ulimwenguni.

Sherehe za Maadhimisho hayo ambazo zimefanyika katika Makazi ya Balozi wa Finland Masaki jijini Dar es Salaam zimehudhuriwa na Mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini.

Finland ilipata Uhuru wake Disemba 6, 1917
Huku nchi yake haina uhuru
 
Finish her......kama motokombati
 
Waziri Kombo Amepiga Glass Ya Inueni Mioyo
 
Back
Top Bottom