Waziri Makamba: Kama hali imeboreka semeni kwamba sasa hivi ni bora kuliko ilivyokuwa, mkisema sio tunanyong'onyea

Waziri Makamba: Kama hali imeboreka semeni kwamba sasa hivi ni bora kuliko ilivyokuwa, mkisema sio tunanyong'onyea

Waziri wa Nishati, Januari Makamba amesema kazi inafanyika na dhamira nzuri ipo na anachoomba uelewa na uwepo wa subira pamoja na kutiwa moyo.

"Kazi inafanyika na dhamira nzuri ipo tunachoomba ni uelewa na subira tunaomba kutiwa moyo kama hali imeboreka semeni kwamba Sasa hivi ni bora kuliko ilivyokua mkisema sio tunanyong'onyea sababu tumetumia pesa tumetumia muda kurekebisha hii hali" amesema Makamba

Chanzo TBC

Dah sasa wanaanza kuwalazimisha watu kusema wasichokiamini!!! Hii ni Haibu SANA WACHA WATU WASEME WENYEWE.
 
Huku Dar ni mgao kwenda mbele, Kama huko ni kuboresha Basi achia ofisi wengine wafanye, makamba kazi imemshinda. Kila siku Dar lazima umeme ukatike na sio Mara moja Mara nyingi.
 
Kwa ujumla Chama changu Ccm naomba tuunde team ya kujua maisha halisi ya Mtanzania ndo tupate uhalisia ulivyo.
Na tukumbuke utulivu uliopo ni vile Mungu amelijenga hili Taifa hivyo ndo maana kila mtu amekuwa mbinafsi na chuki zisizokuwa na maana zenye ubaya na hizo chuki zinavyozidi aileti afya Kitaifa.
Ni Mwenyenzi Mungu azidi kulipigania hili Taifa kwani tuliopewa dhamana bado hatujaliona hili kwa kuwa hakuna chombo cha kufuatilia hali halisi ya maisha
 
Anazunguka tu huyu kutuzuga.

Hapa Kariakoo tunaunganisha Majenereta kwa kasi siku hizi.
 
Waziri wa Nishati, Januari Makamba amesema kazi inafanyika na dhamira nzuri ipo na anachoomba uelewa na uwepo wa subira pamoja na kutiwa moyo.

"Kazi inafanyika na dhamira nzuri ipo tunachoomba ni uelewa na subira tunaomba kutiwa moyo kama hali imeboreka semeni kwamba Sasa hivi ni bora kuliko ilivyokua mkisema sio tunanyong'onyea sababu tumetumia pesa tumetumia muda kurekebisha hii hali" amesema Makamba

Chanzo TBC



Alichokosea tangu mwanzo, badala ya kutekeleza majukumu na kazi yake. Yeye akaanza kujiona bora na muelewa kuliko waliotangulia na mawazo yao. Akaanza kusimama juu ya legacy ya nchi na kuanza kuikanyaga na kuisigina na kisigino huku akitoa maneno yenye makufuru. Hilo lilimtia doa.

Halafu pili yeye badala ya kufanya kazi yake,anawaza urais. Hilo nalo ni shida, maana yanapelea kugawanya moyo, akili, nguvu, mali na muda wake kwenye mambo mengine (ya urais) badala ya kujielekeza kwenye kutekeleza majukumu ya uwaziri.
 
Waziri wa Nishati, Januari Makamba amesema kazi inafanyika na dhamira nzuri ipo na anachoomba uelewa na uwepo wa subira pamoja na kutiwa moyo.

"Kazi inafanyika na dhamira nzuri ipo tunachoomba ni uelewa na subira tunaomba kutiwa moyo kama hali imeboreka semeni kwamba Sasa hivi ni bora kuliko ilivyokua mkisema sio tunanyong'onyea sababu tumetumia pesa tumetumia muda kurekebisha hii hali" amesema Makamba

Chanzo TBC


Mamlaka za uteuzi Msisubiri Hadi ajimalize ndo mteue mwingine.

Utamaduni wa KUJIUZULU haipo CCM, msaidieni kufanya maamuzi.

Saiz anagawa mitungi ya gas nguzo zimelala Barabarani zinaliwa mchwa.
 
Ukweli ni kuwa "kila kukicha afadhali na jana"!
Simamieni rasilimali za nchi acheni kuzitawanya kama viongozi
 
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Kwa mfano jana nimetoka nyumbani bila kupasi nguo.

Shati limejikunja kama limetafunwa na mbuzi.

Sasa sijui hali inayozungumziwa hapa ni ipi??
 
Waziri wa Nishati, Januari Makamba amesema kazi inafanyika na dhamira nzuri ipo na anachoomba uelewa na uwepo wa subira pamoja na kutiwa moyo.

"Kazi inafanyika na dhamira nzuri ipo tunachoomba ni uelewa na subira tunaomba kutiwa moyo kama hali imeboreka semeni kwamba Sasa hivi ni bora kuliko ilivyokua mkisema sio tunanyong'onyea sababu tumetumia pesa tumetumia muda kurekebisha hii hali" amesema Makamba

Chanzo TBC


Hali siyo na imekuwa mbaya kwelikweli tofauti na kipindi cha nyuma. Wewe Kigogo kamwambie huyo Chifu wenu mnayejipendekeza kwake kwa mapambio ya kinafiki,labda kuhusu hali ya hewa ni baridi na joto kwa mbaaaaali.
 
Back
Top Bottom