Waziri Makamba, Uteuzi wako wa Mama Maajar kuwa mjumbe wa bodi ya TANESCO una mgongano wa maslahi

Pia katika teuzi hizohizo za wajumbe wa Bodi, Makamba kamteua mtoto wa Bakhresa ndani ya bodi ya TANESCO.
Huyu jamaa anajipanga kwa ajili ya urais ndiyo maana anawakumbatia watu wenye maslahi na mabeberu na pia Matajiri. ANATENGENEZA MTANDAO WAKE WA URAIS
Atatuuza huyu!
 
Pengine kalemani alipaswa kuondolewa. Lakini haikupaswa kuwekwa mtu kama makamba pale
 
Mkuu ni labda hujui kazi ya bodi.
Lakini pia inaweza kuwa umesahau kuwa kipindi kile Cha dowans, huyu mama Maajar ndio aliishauri Tanesco kuvunja mkataba na Dowans.
Hadi hapo hakupaswa kuteuliwa kwenye bodi,
Ila watanzania ni wasahaulifu sana
 
Nilidhani unasema Huduma zimeanza kuzorota, nilidhani unasema hela stigglers haitoki tena, nilidhani Kuna mikataba ya Tanesco wameingia kuzalisha umeme kwa mafuta!

Kumbe unapiga ramli tu!

Yaaani bodi ivinjwe kwa ramli zako?
Hayo yanaweza kuja, waswahili wanasema ngoma huanza na lele
 
Kwani hiyo bodi ambayo haikuwa na maslahi ilifanya nini cha ajabu? Nakumbuka wakati flan bodi iliiongozwa na mkuu mstaafu wa majeshi lkn ndio wakati tulikuwa na magenereta kila pahala. Mzalendo na asie na mgongano wa maslahi Ni nani Tz? Tuwape muda
Unamaanisha ikiwa huko zamani tuliwahi kuwa na watu wa hovyo kwenye bodi basi yapaswa tuendelee kuwa hivyohivyo?
 
 
Tulieni!..

Mliyaombea sana haya!

Mkalia sana, kwamba mnaonewa sana!..

Mkaomba sana mama awakomeshe sukuma gang..

Na mkafurahia sana kwamba sasa mnapumua..

Tulieni tuliiii.. Mambo ndio kwanza yanaanza
 
Huyu muheshimiwa amepewa wizara iliyo sensitive sana,ajuwe kuwa uzembe wowote atakaoufanya ita reflect kutolewa kwake kwenye uongozi kwenye awamu iliopita,sifikirii kuwa atakubali hili limtokee,ngoja tumpe muda inawezekana akafanya maajabu,na ndio maana mama kamuamini...
 
Kwani hiyo bodi ambayo haikuwa na maslahi ilifanya nini cha ajabu? Nakumbuka wakati flan bodi iliiongozwa na mkuu mstaafu wa majeshi lkn ndio wakati tulikuwa na magenereta kila pahala. Mzalendo na asie na mgongano wa maslahi Ni nani Tz? Tuwape muda
Hicho kipindi cha majenereta kilikuwa cha hao waliorudi kwenye bodi.

Wait and see
 
Mkuu ni labda hujui kazi ya bodi.
Lakini pia inaweza kuwa umesahau kuwa kipindi kile Cha dowans, huyu mama Maajar ndio aliishauri Tanesco kuvunja mkataba na Dowans.
Hadi hapo hakupaswa kuteuliwa kwenye bodi,
Ila watanzania ni wasahaulifu sana
Siku zote mimi huwa nasema shida ya tz na afrika haijawahi kuwa viongozi wao, bali upumbavu wa wananchi
 
Hii ni moja ya kazi ya TISS, wareport kwa hili swala kwa Samia, then SAMIA atoe Amri kwa January, halafu kwa nini waziri anapewa mamlaka makubwa hivi ya kuteua wajumbe katika bodi? kwa nini asipendekeze akapeleka bungeni wakajadiliwa na kama kuna mjumbe anakidhi vigezo apitishwe na bunge ambaye hakidhi vigezo aondolewe na bunge.

Unaweza kukuta Kikwete ndiye kamtumia January baadhi ya majina kwa Whatsap!
 
Watanzania mna vituko!!!...Tuache siasa kwenye Mambo ya Msingi!!..Mama Maajar ni Mtu makini sana kwenye Kazi na atatupeleka mbali kwenye sekta hii ya Umeme!!
 
Makamba ni kiongozi anajua kupanga safu za ushindi na hapa kwenye bodi ya Tanesco ndio kaanza vyema!!..Bodi hii ina watu wenye mafanikio kwenye sekta zote walizowahi kupita!!..Sasa tunategema Neema kwenye Umeme!!.. Shirika lifanye Kazi Kwa ufanisi na kuleta Faida
 
kuna mgongano wa maslahi. Mmoja wa wamiliki wa firm ya kisheria inayowakilisha kampuni inayoishtaki Tanesco amepewa ujumbe wa bodi wa hiyohiyo Tanesco, hii haina afya. kwa shirika, ni mgongano wa maslahi mtupu
 
kuna mgongano wa maslahi. Mmoja wa wamiliki wa firm ya kisheria inayowakilisha kampuni inayoishtaki Tanesco amepewa ujumbe wa bodi wa hiyohiyo Tanesco, hii haina afya. kwa shirika, ni mgongano wa maslahi mtupu
Kwenye mgongano wa kimaslahi!!!...Kila mtu ana maslahi kwenye shirika hili!!....Mama Maajar kuwa na law firm hii!!...Bado haimaanishi atakua na personal interest kwenye shirika hili!!.. Utumishi wa Umma Una miiko yake ndio maana amekubali kuteuliwa!!
 
Spot on....

Kitendo cha kumuweka January kwenye hii wizara tayari harufu ya uchafu ilianza kuhisiwa,mengineyo ni muendelezo na tutarajie zaidi.
Nani sasa anafaa?

Maana kuna waliokuwa wanasema Medard Kalemani alipwaya....

Haya, kaja Makamba, naye anaonekana ana kasoro tayari....

Je, ni nani sasa anafaa kuiongoza wizara hii?

Maana, kwa hali ilivyo, basi mimi naona kabisa kuwa hata wewe ukipata bahati ya kuiongoza wizara hii, watasema mapungufu na kasoro zako kibao tu na inaweza kuwa afadhali hata January Makamba au Medard Kalemani....!

Je, nani sasa anafaa?????
 
Kasoro iko kwenye matendo siyo sura yake
Huwezi kuteua mtu mwenye mgongano wa maslahi kuwa mjumbe wa bodi kisha hiyo ikawa na afya kwa shirika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…