Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, na Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, Zanzibar, Mhandisi Hamad Masauni, amemtaka Kamanda wa Polisi Mjini Magharibi komesha kero ya wizi katika Shehia ya Kikwajuni Bondeni. Mhandisi Masauni ameyasema hayo mapema jana, Oktoba 28, 2024, wakati akihitimisha ziara yake ya siku tatu Jimboni, kwa Shehia za Mwembeni, Mwembeladu na Kikwajuni Bondeni iliyolenga kusikiliza na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi kwa utaratibu wa ‘Papo kwa Papo’.
Aidha, kwa nyakati tofauti wananchi wa Shehia ya Kikwajuni Bondeni wameomba kusaidiwa kujikwamua kiuchumi kwa kuwezeshwa katika mradi yao ya maendeleo sambamba na kutoa kero iliyohusu tatizo la wizi kwa Mhandisi Masauni ili iweze kutapatiwa ufumbuzi.
Akijibu kero hiyo Waziri Masauni amemtaka Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi kuhakikisha tatizo la wizi linakomeshwa mara moja.Vilevile, Mhandisi Masauni katika ziara hiyo atoa misaada kuwezesha vikundi vya vijana na kinamama kujikwamua kiuchumi ikiwa ni pamoja na kuwapatia mitaji, pikipiki, mashine za pampu za visima vya maji, vifaa kwaajili ya ukarabati wa majengo na ukatarabati wa Matawi ya CCM kwa Shehia hizo.