Waziri Masauni aonya wanaodhihaki viongozi mtandaoni

Waziri Masauni aonya wanaodhihaki viongozi mtandaoni

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Ila CCM imejaa viongozi wengi wajinga, badala mtilie mkazo kwenye uadilifu, kukemea uchawa na wizi, rushwa na ufisadi, mnakuja kujitia aibu kwa ujinga kama huu! kwani nani hajui kukosolewa kwenu ni matusi? Kukosolewa kwenu ni uchochezi? Kukosolewa kwenu ni kuleta machafuko?

Yaani kama hamtoshei kwenye nafasi zenu mnataka wanachi tusiseme? Kama kichwani hamna kitu mnataka msiambiwe? Tuwape dhamana sisi halafu mkituibia na kwenda kinyume na katiba tusiseme?

Masauni ungekuwa unatoshea kwenye hiyo nafasi hata kwa robo tu usingeongea haya umeongea leo na kuhamasisha vijana wawe chawa, unatia aibu! Yaani manvuliwa nguo kila siku tena na CCM wenzenu halafu unakuja kulaumu wapinzani na wananchi, na mnaona mnafanya la maana kabisa kuja kutisha wanachi kama hivi?

Siku tutakayowakomboa chawa wote, ndio mtaelewa viongozi wengi CCM ukiwemo na wewe hakuna kitu!

#KataaUozo2025
#KataaMachawa
#KataaWajinga2025

===

"Kweli tumekuwa kimya kusemea mazuri ya Dk. Samia na Dk. Mwinyi, tujitathmini tu katika hilo, kwamba je nafanya hayo? Kwasababu kiukkweli Marais wetu hawa wawili wamefanya mambo mambo makubwa sana katika muda mfupi.

"Na bahati mbaya sana tunatoa nafasi kwa wapinzani kufikisha jitihada hizi, kwanini hamuoni kuna viclip vya kijinga jinga vvinasambaa vya wapinzani? Wanadhihaki viongozi wetu, wanadhihaki serikali.

"Sisemi kwamba lazima na wewe utoe clip ujibu lakini hata ukifanya kazi katika eneo ulipo, kama wewe ni balozi , nyumba zako 10 tafuta namna ya kuweza kufikisha ujumbe, kama ni tawi, tawi lako.

"Lakini niwapongeze sana viongozi wetu hawa, hawajatetereka, na sisi tuwe mfano wa kufuata nyayo zao. Wako watu walioona kwamba kwasababu hakuna ajenda, ilani imetekelezwa kwa kiwango kikubwa kabla hata ya wakati, hawa wapinzani wakaona labda pengine watafanya vitu vitasababisha kuteteresha mshikamano na umoja uliopo.

"Wakatishia wengine kutaka kujitoa sijui katika serikali ya umoja wa kitaifa lakini kwa busara za viongozi wetu hawa, wametulia, wanafanya mambo kwa vitendo, hawajatoka kwenye reli.

"Hayo wanafanya lengo lao si tu kututoa kwenye reli lakini vile vile kutaka tunapoelekea kwenda kutekeleza demokrasia ya kuchagua viongozi tunaowataka katika uchaguzi mkubwa unaotarajia kufanyika mwakani ili twende nchi yetu ikiwa haina amani. Jambo hilo haliwezekani.

"Nataka niwahakikishie, hiyo dhamana nimepewa mimi, mimi ndio Waziri wa Mambo ya Ndani, ninayesimamia mapolisi na vyombo vya usalama, watu watafanya uchaguzi katika nchi hii kwa usalama na amani, na mtu yoyote asijaribu kutaka kucheza na amani ya nchi hii, tutailinda amani na usalama wa nchi hii kwa gharama yoyote."


Waziri wa Mambo ya Ndani Hamad Masauni amesema hayo leo Jumapili, Julai 7, 2024 visiwani Zanzibar, kwenye hafla ya kufungua mafunzo ya uongozi wa Chama Cha Mapinduzi na jumuiya zake.
 
Usalama utakuwepo wakati wote na ile sheria waliyoipitisha msiisahau.
 
Mnatoza maKodi kibao mnanunulia LC300 ,kuwahudumia wananchi Aaaaaaah.

RAC.jpeg
 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ameonya watu wenye tabia ya kurusha video za kukejeli viongozi Wakuu wa Kitaifa huku akigusia matukio mbalimbali yanayoendelea katika mitandao ya kijamii ikiwemo kijana aliyehukumiwa kwenda jela hivi karibuni baada ya kuonekana akichoma moto picha ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Samia Suluhu Hassan ambapo pia akiwahakikishia wananchi kuwepo kwa usalama wakati wa chaguzi za serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwakani.

Ametoa kauli hiyo leo Julai 7, 2024 Visiwani Zanzibar wakati alipoalikwa kufungua Mafunzo ya Uongozi wa Chama cha Mapinduzi na Jumuiya zake huku viongozi mbalimbali pia wakitoa neno kuelekea chaguzi hizo.
 
Vipi na kuhusu wananchi wengine waaodhihakiwa huko mtandaoni! hawamhusu? Au yeye ni Waziri wa kulinda maslahi ya viongozi pekee?

Mimi nadhani angeongea kwa ujumla. Na siyo kuwa specific. Maana wananchi wote tunatakiwa kuongozwa na sheria za aina moja. Haitakiwi watu wengine waonekane ni special sana kuliko wengine.
 
Halafu Mwananchi anayepita hapo Choka mbaya hata Aibu hawaoni.

Umeona ehee,lazima wananchi wawaseme coz kodi zao zinatapakanywa,mitozo kila kona lakini huduma za jamii zero,wananchi tumepigika mlo mmoja wa bahatisha ndulute huku sirikali inanunua LC300 matumizi ya anasa.

Wapunguze mikodi ,wawahudumie wananchi vizuri uone kama watasemwa,wapunguze matumizi ya anasa,watosheke na mishahara yao ,waache upigaji ,fedha zielekezwe kwenye maendeleo.
 
😂 😂 😂 😂
Huyu Jamaa siasa huwa anajilazimisha tu bora angebaki kuwa Muhandisi tu. Sasa hizo sheria wametungiwa Wanyonge tu? Halafu kwann Viongozi watukanwe? Huwa wanajisahau sana hawa Wanasiasa hawajui sisi ndio mabosi zao?
 
Umeona ehee,lazima wananchi wawaseme coz kodi zao zinatapakanywa,mitozo kila kona lakini huduma za jamii zero,wananchi tumepigika mlo mmoja wa bahatisha ndulute huku sirikali inanunua LC300 matumizi ya anasa.

Wapunguze mikodi ,wawahudumie wananchi vizuri uone kama watasemwa,wapunguze matumizi ya anasa,watosheke na mishahara yao ,waache upigaji ,fedha zielekezwe kwenye maendeleo.
Hawa watu sijui wakoje!?Kusemwa tu ndiyo wanaugua na kulazwa hospitali?Na wenye kulala njaa,kushindwa kusomesha watoto wao,kukosa sehemu za kuegesha mafuvu yao/kulala na kupata shida nyingine wasemeje?
 
Umeona ehee,lazima wananchi wawaseme coz kodi zao zinatapakanywa,mitozo kila kona lakini huduma za jamii zero,wananchi tumepigika mlo mmoja wa bahatisha ndulute huku sirikali inanunua LC300 matumizi ya anasa.

Wapunguze mikodi ,wawahudumie wananchi vizuri uone kama watasemwa,wapunguze matumizi ya anasa,watosheke na mishahara yao ,waache upigaji ,fedha zielekezwe kwenye maendeleo.
Halafu hawataki tuongee wanataka umsifie tu Mama Abduli. Nasema hivi over my dead body...
 
Back
Top Bottom