Waziri Mhagama aagiza utekelezwaji wa ajira mpya kuanzia Julai, 1

Waziri Mhagama aagiza utekelezwaji wa ajira mpya kuanzia Julai, 1

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2021
Posts
1,147
Reaction score
2,008
Akichangia hoja ya Utoshelevu wa Watumishi wa Umma na mifumo ya ajira nchini Bungeni leo, Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ameagiza Sekretarieti ya Ajira kutangaza vijana waliofaulu usaili wa ajira za utumishi wa Umma na Julai 1, ajira zote mpya zianze kufanya kazi.

Vile vile ameelekeza Mfumo wa usaili kuwezeshwa katika Mikoa yote nchini,ili hatua ya awali ya usaili ifanyike Mikoani na hatua nyingine kufanyika ngazi ya Kanda na hata Taifa ili kupunguza kero ya Vijana ya usafiri kufuata vituo vya usaili Jijini Dodoma.

Aidha ameagiza Sekretarieti ya Ajira kutunza kumbukumbu za wanaofaulu usaili katika nafasi zinazofanana ili vijana wasihangaike kurudia kufanya usaili na badala yake database hiyo itumike kuajiri.

 
Sekritarieti ya ajira walikuwa wanasubili tamko la kisiasa sasa naona watafanyia kazi maagizo hayo ya waziri..
 
Yani maombi ya ajira yanachukua zaidi ya mwezi,ilitakiwa wachangamke,ndani ya mwezi mmoja watu wawe wameajiriwa tayari
Sasa unasubiri siku almost 30 ndio uitwe Dom kwenye usaili unaochukua zaidi ya week
 
Back
Top Bottom