Uchaguzi 2020 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa apasua ngome ya Mbowe Hai

Uchaguzi 2020 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa apasua ngome ya Mbowe Hai

Wanasheria nisaidieni sielewi vizuri ,hivi mpaka mda huu bado baraza la mawziri lipo? najua kidogo rais bdo yupo may be bado na waziri mkuu akwa yupo vipi mawaziri wengine ? nauliza hivi nikimanisha majuzi nilimuona waziri flani kwenye mambo ya ajira
 
Mkuu, Mbowe huko anaitwa ni Kaka, kwa taarifa yako huyu ni mwanafamilia ktk kila kaya na anakubalika ktk kila familia. Nakuhakikishia wale wahuni wa UVCCM waje tena na fujo zao tena ktk kipindi hiki cha kampeni chini uratibu wa mkora Sabaya ndiyo CCM watatambua ukweli wa mambo.
Wanafaidika vp kwa kumkubali Mbowe au ndio yaleyale ya ushabiki wa vyama tu kama tunavyoshabikia simba na yanga? Au ndio kuwakomoa CCM?

Yani siasa za bongo Mtu unaweza ukawa na uhakika wa kuchaguliwa kila uchaguzi hata kama hufanyi maendeleo yeyote kwenye jimbo lako.
 
Yaani reli , meli, madaraja viwanja vya ndege mpeleke lake Kisha mlete treni bovu na reli mbovu K'njaro.
 
Mkuu, Mbowe huko anaitwa ni Kaka, kwa taarifa yako huyu ni mwanafamilia ktk kila kaya na anakubalika ktk kila familia. Nakuhakikishia wale wahuni wa UVCCM waje tena na fujo zao tena ktk kipindi hiki cha kampeni chini uratibu wa mkora Sabaya ndiyo CCM watatambua ukweli wa mambo.
Mbona walizomea kwenye mkutano wake mpaka polisi wakamsaidia kutoka mkutanoni? Au alikuwa Mbowe mwingine??
 
Wanasiasa bwana! Hivi Ruangwa Kuna maendeleo?

Hata barabara ya kuunganisha Ruangwa na Lindi haipo, lakini ukiwasikiliza utafikiri majimbo yote ya CCM yana maendeleo.
 
Bwashee kwa mbowe ninavyomfahamu na Hai ninavyoifahamu labda wakimbie na masanduku ya kura maana nimeishi Bomang'ombe kwa miaka 3, ninapafahamu vizuri MCC pale haitakiwi, labda kwa mbinu zile zingine za kimedani za CCM ndio watatoboa.
 
Mkuu, Mbowe huko anaitwa ni Kaka, kwa taarifa yako huyu ni mwanafamilia ktk kila kaya na anakubalika ktk kila familia. Nakuhakikishia wale wahuni wa UVCCM waje tena na fujo zao tena ktk kipindi hiki cha kampeni chini uratibu wa mkora Sabaya ndiyo CCM watatambua ukweli wa mambo.
Namwamini Mbowe katika kuendesha kampeni za Ubunge wa Hai, Lakini nitamuamini zaidi kama atashinda uchaguzi wa 2020. Ni mgumu sana hapa Hai mwaka huu.

Na sababu ni moja tuu, Uongozi wote wa Kata, Tarafa na vijiji karibu vyote jimbo la Hai ni CCM na 90% ya Viongozi wote walikuwa wana chama wa Chadema.

Wanaogombea mwaka huu Hai ni Chadema na Chadema walioasi ambao wamejiunga na wana CCM kutaka kuchukua Jimbo. Kuna mtifuano. Tusubiri tuone.
 
Mbowe arudi kwenye kazi yake ya udj.
"kwaheri Mbowe,,,kwaheri Mbowe"
 
Wanafaidika vp kwa kumkubali Mbowe au ndio yaleyale ya ushabiki wa vyama tu kama tunavyoshabikia simba na yanga? Au ndio kuwakomoa ccm?

Yani siasa za bongo Mtu unaweza ukawa na uhakika wa kuchaguliwa kila uchaguzi hata kama hufanyi maendeleo yeyote kwenye jimbo lako.
Ccm imefanya maendeleo gani kwa miaka karibia 60 ??
 
Ccm imefanya maendeleo gani kwa miaka karibia 60 ??
Sizungumzii vyama,hata ccm wapo watu ambao kila uchaguzi wanapita ila hakuna ambacho wananchi wanafaidika katika maendeleo,ndio maana nikahoji pia kwa Mbowe hao watu wanaomkubali ni kipi wananchofaidika?
 
Waziri Mkuu Kasim Kajaliwa amebomoa Ngome ya Mwenyekiti wa Chadema Taifa na Mbunge anaye maliza muda wake Freeman Mbowe kwa kusema hai ilikosa Mbunge kwa muda wa miaka kumi na tano.

Ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa kampeni za mgombea ubunge wa jimbo la hai pamoja na kumwombea Kura Mgombea Urais wa CCM john Pombe Magufuli kura za ndio kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa jamuhuri wa muungano wa Tanzania kwa miaka mitano tena.

Majaliwa amewaambia wananchi wa hai waache ushabiki wa kuchagua viongozi wasio na uwezo Bali wachague mtu mwenye uwezo wa kutatua matatizo yao na kuwasikiliza wapiga kura wake na atakaye kaa jimboni.

Waziri Mkuu Majaliwa amesema hai imekosa maendeleo ya haraka kwa sababu mwakilishi wake akuwa na mipango ya kuleta maendeleo ya chap chap kama wabunge wengine.

Majaliwa amewaomba wananchi wa jimbo la hai kumchagua mgombea ubunge wa Ccm, Saasisha Elinikyo Mafuwe. ili aweze kuleta maendeleo hai kwani atapingana na serikali yake.

Amesema hai tumemtumia kijana msikivu Lengai Ole Sabaya kusimamia maendeleo kwa sababu Mbowe amekua akipinga kila kitu na kushindwa kuwa mwakilishi wa wananchi kwani mambo mengi wanapingana na serikali na kutoka nje ya bunge.

Kwa upande wake mgombea ubunge wa hai ameomba kura kwa kusema kwamba hatasimamia miradi yote ya maendeleo katika jimbo la hai ndani Siku mia moja ikiwemo miradi ya Maji Afya Elimu na miundo mbinu ya bara bara.

Amewaomba wananchi kumpa kura na kumpima kwa muda wa miaka mitano waone utendaji wake wa kuleta maendeleo kwa kushirikiana na madiwani wa halmashauri ya Hai.

Mgombea ubunge wa Siha Mollel amesema Mbowe hafai kuwa Mbunge tena kwa sababu amekuwa akitumia fedha za mfuko wa jimbo vibaya hivyo asichaguliwe na wananchi tena

Meya mstaafu wa jiji la Arusha kalisti Lazaro katika kampeni hizo amemwelezea mbowe kuwa ni kiongozi asiye jitambua hasa kupingana na serikali na kuwashawishi wabunge na madiwani wake kupinga maendeleo

Kalisti amesema alikua Chadema ameongoza baraza la madiwani kwa miaka mitano amekuwa akiambiwa apingane na serikali na hata muda mwingine avunje baraza iyo yote ni kuonyesha kupingana na serikali.

Kuna vichwa vingi ambavyo siyo vya wapiga kura

1599602396299.png
 
Back
Top Bottom