Mwendokasi washafeli
Kwanza kwa style yao ya ukataji ticket
Watakosa sana hela
Niulize kwanini?
Ova
Hiyo alienda kuangalia kama inataka kuwaka.[emoji23]LEO NIMEPANDA MOJA
DEREVA ANASHUKA ANAENDA KUCHOCHEA KULE NYUMA NDO INACHANGANYA
Hakuna kitu ambacho serikali ya CCM imewahi fanikiwa na hii tabia ya kufanya biashara italeta hasara daily
Mwendo kasi inaendeshwa kwa hasara alisema bro kindamba mtu mzito apo sababu ya politics issues
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo amefanya ziara ya kushtukiza kituo cha mwendokasi eneo la gerezani na kukuta mfumo wa kusoma tiketi haufanyi kazi, mtendaji mkuu alisema mfumo haufanyi kazi baada ya kutokea mgogoro kati ya supplier na alieununua. Meneja huyo amesema mfumo mpya unajengwa na waziri mkuu kumuhoji inatumia miaka mingapi kukamilika?
Majaliwa amesema wanaibiwa mapato kwani wao wanatumia mtambo na wengine wanatumia mtambo mwingine na hawana namna ya ku-check.
Pia Meneja amehojiwa tangu aingie amenunua mabasi mangapi baada ya serikali kununua mabasi 140 huku mabasi yanayokadiriwa kuwa barabarani ni wastani wa 100.
Mtoa huduma ya mwendokasi aliagiza mabasi 70 ambayo yamekwama kuingia barabarani kutokana na mgogoro na waziri mkuu akasema anaenda kuyaona. Majaliwa amesema wananchi wanalalamika mabasi hayatoshi akitolea mfano Kimara watu wanaingilia dirishani na kuhoji mapato wanayokusanya wanapeleka wapi kama wanashindwa kununua mabasi.
Pia waziri mkuu amepita karakana ya Jangwani na sasa anaelekea Ubungo kuangalia mabasi yenye mgogoro
==========
UBUNGO: Kinachoendelea waziri mkuu anauliza hatua zinazoweza kuchukuliwa kwa mabasi yaliyokwama ambapo mtu TRA anasema sheria inamruhusu kamishna kuya-donate au kuyaharibu na waziri mkuu amesema hawezi kupewa Shabiby kwasababu hayamfai kwenda Dodoma kwani ni kwaajili ya barabara za mwendokasi na sasa anauliziwa mwanasheria
Pia waziri mkuu anawaambia forodha waendelee kufanya minada ya mizigo iliyokaa kupita kiasi mara kwa mara ili kusafisha nafasi ya kuagiza mizigo mingine na kuwataka wabadilike kwani baadhi ya wateja wanalalamika process zinachukua muda mrefu
Kassim Majaliwa anasema pesa zilizotumika zimekopwa world bank na zinalipwa na mabasi yameletwa na mjasiriamali laiki ameshindwa ku-comply na sheria na sheria zimechukua mkondo wake tangu 2018 na kutaka kesho wakae waamue
Majaliwa amesema serikali inao uwezo wa kununua mabasi lakini tatizo ni usimamizi na hawawezi kumsimamia msimamizi ambae hawezi na leo amemuweka pembeni mkurugenzi wa fedha na mwingine anamuachia Rais kwani yuko kwenye mamlaka yake.
HongeraSina shida ya kuongoza udart or any govt ofis.
Bajaji zangu ninazosimamia zinatosha.
Tatizo humu jamvini kuna raia mnajiona mnajua everything but they don't know everything! Inaamaana wazir mkuu amekurupuka? Hujasikia akiwalaumu kua wameshindwa hata kununua magari mengine na kampuni inaenda kufa? Kasome vzr maneno ya prime minister ndo urud hapa. Kwamba unamaanisha hata wazir hajui kama wana mkopo??Hujui kama jamaa wana mkopo mkubwa....
usirukie vitu usivyojua utapasuka msamba
Utumbuaji wa hivi haufuati waraka wa utumishi wa umma.Amefanya sahihi. Kuhojo hadharani ni sahihi kabisa ila wananchi wajue kinachoendelea.
Kutumbua ndio inapaswa kufuata taratibu za kiutumishi.
Mradi kama huu unaendeshwa kwa mafanikio sana Latin Amerika. Nao wanatumia mabasi sio treni.Mràdi ulikosewa tangu awali. Mràdi huo ulitakiwa utumie train za umeme za kuzunguka kwà kutumia barabara hizo hizo. Matokeo yake wakaenda kumtoa mchina shida kwà kununua mabasi ya kichina.pia train ya umeme nauli ingekuwa kidogo, pia uharibifu ni kidogo, kuzitawala ni rahisi pia,
Hata SGR, kama inakamilika, yatakuwa ni haya haya tu.
Wapewe wachina waendeshe, maana hawatakuwa na dugu kwenye ujinga ujinga 😁!.Hata SGR, kama inakamilika, yatakuwa ni haya haya tu.
Tunarudi wapi wewe,mabasi yanajaa lakini hawanunui mapya,tiketi wanatoa kienyeji halafu unataka aulizwe sebuleni huku anakunywa fanta?Tunarudi kule kule. Haya mambo si ya kuulizana jukwaani. Angemwita yeye na viongozi wake ili wakae waone tatizo liko wapi. Kama ni uongozi lingeonekana tu.
Na kama ni serikali ingeonekana tu maana Meneja angeweza kusema kweli yake bila kuonekana kuwa anamdhalilisha WM hadharani. Inabidi viongozi wakuu wabadilike.
Amandla...
Hakuna kulemba ni kubomoa hapo hapoTunarudi kule kule. Haya mambo si ya kuulizana jukwaani. Angemwita yeye na viongozi wake ili wakae waone tatizo liko wapi. Kama ni uongozi lingeonekana tu.
Na kama ni serikali ingeonekana tu maana Meneja angeweza kusema kweli yake bila kuonekana kuwa anamdhalilisha WM hadharani. Inabidi viongozi wakuu wabadilike.
Amandla...