Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ni msafi kisiasa; Hana kashfa ya rushwa; anaaminika zaidi na wananchi/dola. Je, tupo tayari kuona mafisadi wanamstafisha?

Ni muongo wa kuzaliwa, congenital liar. Alisema Rais yuko busy anapiga kazi, mnataka mumuone wapi, Magomeni Mwembechai sokoni?

Kumbe Rais kashanyooka. Tena kaongopea msikitini, Astakafullulillah ladhim!
We ulitaka atoe taarifa kuwa Rais kafariki msikitini. Kumbuka katiba ya JMT inamruhusu makamu wa Rais kufanya hivo. Be positive Brother.

Sent from my STK-L21 using JamiiForums mobile app
 
Mengine yote uliyoyataja ni kweli kabisa sifa hizo zote na nyingine ambazo hukuzitaja.

Lakini moja tu hana. HANA UWEZO NI MUOGA MNO HADI AGONGWE KONZI KIDOGO AU APAPASWE NDIO ANASTUKA aaahhooo kumbe mimi ni waziri mkuu ndio sasa anaact. Vinginevyo ni hana uwezo kabisa kabisa
 
Ni muongo wa kuzaliwa, congenital liar. Alisema Rais yuko busy anapiga kazi, mnataka mumuone wapi, Magomeni Mwembechai sokoni?

Kumbe Rais kashanyooka. Tena kaongopea msikitini, Astakafullulillah ladhim!
Intelijensia ilimlazimu aseme Rais yu hai Ili kulitayarisha Taifa.Mbona hata Mkapa alichelewesha demice ya Mwalimu?Ni kweli PM hajasikika ni fisadi kama alivyo Tundu Lisu wa CDM
 
Mtu muongo muongo mbabaishaji Hana nafasi.
Niwakumbushe kidogo tuuu. Hivi aliyeshirikisns na yule Mhaya kuuza shule za wazazi na kujinufausha siyo yeye? Hivi aliyemwambia mtumishi wa TPA kurudishia mita gage ya mafuta wakati wa ziara ya Gahafla ya magufuri bandarini akimwambai " Rudisha kama zamani , mweu anakuja hukoa' bahati mbaya akakamatika akirudishia na kufukuzwa kazi sio yeye kweli?
 
Hujui kitu au umeamua kujitia upofu. Kwa ufupi ujue tu kuwa ndani ya uongozi wa CCM na Serikali, hakuna msafi hata mmoja. Wanazidiana tu kwa viwango wa uovu.

Huyo unayemsema, nenda Dodoma alikojengewa ghorofa na mfanyabiashara wa kiarabu. Halafu utuambie, huyo aliyemjengea hilo ghorofa lake, yeye anamlipa nini?
 
Muongo hawezi kuaminika tena uongo mwingine anautolea kwenye mimbar za Msikiti wa Ijumaa.

Huo ukiazi.
 
Anaaminika na dola!!?neno kubwa hilo yaani dola inamwamini si ndio!?

Au dola ndio imemwambia agombee URAIS 2025!!?

Au ndio huyo FDR!!?anaetajwa tajwa humu tunaemsubiri!!?

Ngoja tuone!
 
Tafuta ripoti ya Bashiru Ally juu ya uhakiki wa mali za CCM ndiyo utajuwa uchafu wa Majaliwa Majaliwa Kassim. Isingekuwa busara za Mkapa (RIP), Magufuli alikuwa anamvua u-PM mapema mwaka 2017
 
Nilifikiri ni Tanzania, kumbe ni Yazania.......bila shaka anafaa kuwa rais wa Yazania.
 
Mbona mnatuchanganya makada wa ccm?Tusimame na mama au majaliwa
 
Nukuu:
"Ikiwa haya unayosema ni sahihi unadhani kwanini 2020 alipita bila kupingwa huku wagombea wangine wa Ruangwa wakitekwa ?"


Thanks Quote Reply
 
Ni mwongo balaa, yaani ni professional Liar.
 
Aliyeongopa siyo KASSIM Majaliwa, aliyeongopa alikuwa Waziri Mkuu katika kutekeleza majukumu yake ya kazi.

Hapa tunamjadili Mwalimu Kasim Majaliwa
Kama Yuko tayari kuongopa sababu ya Cheo, atatufaa nini?
 
Yuko makini sana nafuraishwa na utendaji wake, anafaa kuwa Rais wa nchi.Hababaishwi, hajivuni, anajua anachofanya.Kutoka kwa Magu kwenda kwa Samia tungesikia mengi lkn yeye kimyaa utadhani hakukwazika, kifua chake ni kipana sana.
 
Anaifaa Tanzania 2025, ana uthubutu,makini na Hana mchezo na wabadhirifu. Huyu angekuwa na full power Watanzania msingejuta kama sasa hivi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…