Waziri Mkuu Kassim Majaliwa: Rais Magufuli ni mzima na anachapa kazi. Wanataka atoke, atoke aende wapi? Kariakoo au Magomeni?

Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa, amewataka watanzania wawapuuze Wapotoshaji wa mitandaoni wanaotaka kuleta taharuki juu ya Afya ya Rais Magufuli "Rais ana shughuli nyingi, Wanataka atoke aende wapi, Kariakoo au Magomeni tangu lini?"

Leo asubuhi wakati nakuja huku nimeongea naye kwa simu na ameniagiza niwaambie wana Njombe kuwa anawapenda sana na anawashukuru sana kwa kura nyingi mlizompigia

Kuna wenzetu hawaishi hapa nchini, wao kazi yao ni kutuombea mabaya tu, kupandikiza chuki tu. Sasa unamuombea mwenzako kufa hiyo ni akili kweli? Nawatoa hofu watanzania, Rais wenu yuko imara anafanya kazi zake kama kawaida za ofisini.

Tuhakikishe tunamuabudu Mungu, tunamuomba Mungu katika kila jambo, tunamtegemea Mungu katika kila jambo, hata asubuhi nilivyokuwa natoka Dodoma nimempigia kumjulisha ratiba yangu, hata juzi alikuwa anajua ninakuja akanituma, wasalimie wana Njombe na nilitoa Salamu.

Naomba nirudie, kwa salam alizotupa leo kweli wana Njombe, mheshimiwa Rais anawasalimia sana wana Njombe, mheshimiwa Rais anawashukuru wana Njombe.

 
Ila kwa uhalisia kama Rais angekuwa katika hali kama hiyo inayosemwa ni dhahiri kungekuwa na taharuki na isingewezekana kamwe kwa waziri Mkuu kuendelea na ziara kama hizo.

I BET THE PRESIDENT IS FULLY FIT AND FINE
Umepata funzo gani mkuu??
 
Tatizo poor security unit ya jpm MTU anapelekwa mhimbili kudungwa sindano hawashituki
 
 
Kumbe mtu alikuwa kwenye -20oC
 
Tatizo poor security unit ya jpm MTU anapelekwa mhimbili kudungwa sindano hawashituki
Jamaa alijiamini sana, kumbe alikuwa amezungukwa na mazimwi wala watu. Kwa nje walikuwa wanacheka na kufurahi ila mioyoni walimsagia meno.
 
Mfuno wa nchi unafikia pahala unamdanya hadi Makamu wa Rais na Waziri Mkuu - hii nchi tuna matatizo mengi. Mimi kwa kauli hii simlaumu Waziri Mkuu.

Makamo wa Rais na yeye akapewa safari ili asiwe karibu na eneo la tukio - Bongo aiseee !!
 
Mfuno wa nchi unafikia pahala unamdanya hadi Makamu wa Rais na Waziri Mkuu - hii nchi tuna matatizo mengi. Mimi kwa kauli hii simlaumu Waziri Mkuu.

Makamo wa Rais na yeye akapewa safari ili asiwe karibu na eneo la tukio - Bongo aiseee !!
FUSO, hivi hapa unataka kusema nini hasa? Nani alimdanganya nani hapa? Waziri Mkuu unadhani hapa aliongea na nani? Muongo hapa ni yupi?

Namnukuu Waziri Mkuu, "Leo asubuhi wakati nakuja huku nimeongea naye kwa simu na ameniagiza niwaambie wana Njombe kuwa anawapenda sana na anawashukuru sana kwa kura nyingi mlizompigia"
 
I BET THE PRESIDENT IS FULLY FIT AND FINE
Mnaona? Hivyo hivyo CCM wana bet na maisha yetu Watanzania. Wakati hatuna maji, hatuna umeme bila shaka wao huko wana bet we are fully fit and fine!

Na sisi kama kondoo, tunajipiga vifua tukiisifia serikali huku tukipelekeshwa machinjoni!.
 
alipewa maelekeza aseme hivyo...same as ni nani alimpangia mama ziara wakati mzee yupo hoi kitandani na yeye akasema hivyo hivyo kwamba mwili lazima ujicheki cheki vijihoma vya hapa na pale.
 
alipewa maelekeza aseme hivyo...same as ni nani alimpangia mama ziara wakati mzee yupo hoi kitandani na yeye akasema hivyo hivyo kwamba mwili lazima ujicheki cheki vijihoma vya hapa na pale.
Kumbuka Waziri Mkuu hakusema amepata/amepewa taarifa, hapana, alisema ameongea naye (Magufuli?) kwa simu. Hakuna utetezi hapa, kama hakuongea na Magufuli, yeye ni muongo, period! Amewadanganya wananchi.
 
Kiswaswadu muongo sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…