Waziri Mkuu Kassim Majaliwa: Rais Magufuli ni mzima na anachapa kazi. Wanataka atoke, atoke aende wapi? Kariakoo au Magomeni?

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa: Rais Magufuli ni mzima na anachapa kazi. Wanataka atoke, atoke aende wapi? Kariakoo au Magomeni?

Jana usiku mama Suluhu Hassan alitangaza msiba kwa masikitiko makubwa na kuueleza umma kuwa Mh. Alilazwa tangu tar.6 ila mh. Majaliwa aliuambia umma tar 12 kuwa Mh. yupo ofisini anachapa kazi.

Wakati mwingine tunashindwa kuaminiana kwa maneno yanayotolewa na viongozi wetu.

It's time to wakeup
So mlitaka awaambie Raus anaumwa.Sio sawa kuna taratibu.
 
BASI VEMA KAMA NI HIVYO, lakini msiwe kama katelefoni.....
Sema ketelefoni alikuwa anatekeleza yake ambayo bosi wake alitaka iwe hivyo. Unakumbuka Dkt JK alipokuwa na tezi dume alitaka isiwe issue ya public akiwa waziri wa Dkt JK, mwisho DKT JK akasema niwajulishe tu watanzania
 
Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa, amewataka watanzania wawapuuze Wapotoshaji wa mitandaoni wanaotaka kuleta taharuki juu ya Afya ya Rais Magufuli "Rais ana shughuli nyingi, Wanataka atoke aende wapi, Kariakoo au Magomeni tangu lini?"

Leo asubuhi wakati nakuja huku nimeongea naye kwa simu na ameniagiza niwaambie wana Njombe kuwa anawapenda sana na anawashukuru sana kwa kura nyingi mlizompigia

Kuna wenzetu hawaishi hapa nchini, wao kazi yao ni kutuombea mabaya tu, kupandikiza chuki tu. Sasa unamuombea mwenzako kufa hiyo ni akili kweli? Nawatoa hofu watanzania, Rais wenu yuko imara anafanya kazi zake kama kawaida za ofisini.

Tuhakikishe tunamuabudu Mungu, tunamuomba Mungu katika kila jambo, tunamtegemea Mungu katika kila jambo, hata asubuhi nilivyokuwa natoka Dodoma nimempigia kumjulisha ratiba yangu, hata juzi alikuwa anajua ninakuja akanituma, wasalimie wana Njombe na nilitoa Salamu.

Naomba nirudie, kwa salam alizotupa leo kweli wana Njombe, mheshimiwa Rais anawasalimia sana wana Njombe, mheshimiwa Rais anawashukuru wana Njombe.

Hii huwa inanikumbusha kama "meme".
 
Back
Top Bottom