Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa: Tunaboresha maslahi ya Wafanyakazi, sio lazima tuseme hadharani

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa: Tunaboresha maslahi ya Wafanyakazi, sio lazima tuseme hadharani

Aidha, Waziri Mkuu ameeleza kuwa maslahi ya wafanyakazi hayapo kwenye mishahara tu bali pia kwa kuwapandisha daraja na kupunguza kiwango cha kodi.
Ndo maana waalimu wengi unasikia tunakubadilishià cheo cha muundo ila sio daraja la mshahara yaaani haya kuna jamaa hawana huruma kabisa.
 
Wameshafeli kwenye hili
Kwa muda mrefu tangu mwaka 2016, nimekuwa nafuatilia nafuatilia kauli za PM kuhusu hiyo mishahara ya wafanyakazi, mara utamsikia akisema hivi sasa serikali imetengeneza mfumo wa kielekroniki wa lawson, ni mfumo unaobainisha wenyewe watumishi wanaostahili kupandishwa madaraja, hivyo tatizo hilo limepatiwa ufumbuzi wa kudumu! Haya ilipofika 2018, akaja na kauli mpya OOH! Serikali imeunda Tume ya kupitia upya viwango vya mishahara na kwa tunasubiri ikamilishe kazi na kutoa mapendekezo! Tume hiyo mpaka leo kimyaa! Na sasa leo bado anasema serikali ikipandisha mishahara gharama nyingine zitaongezeka! Hapa serikali iache uvivu!

Hivi si hiyohiyo serikali ndio inayotoa bei elekezi ya huduma?

Kwani wakiwapandishia wafanyakazi mishahara alafu wakatoa bei elekezia za nauli za mabasi na huduma nyingine ni nani atapinga???
Ikumbukwe kwamba ongezeko la mishahara kwa wafanyakazi lina mchango sana katika kuchangamsha mzunguko wa fedha na ukuwaji wa uchumi kwa ujumla!

Ukipandisha mishahara na madaraja kwa watumishi utawezesha watumishi hawa kukopa mamilioni kwenye mabenk, Ni haohao watumishi watalipa fedha hizo kufanya manununuzi, kulipia huduma na mambo mbali mbali, humo mote serikali itakusanya kodi na kutunisha mfuko, uchumi unapaa, Lakini kuendelea kuzuia mishahara isipande kunadumaza mzunguko wa fedha na ucumi kwa ujumla.
Nashauri serikali ishirikishe wataalam wake wa masuala uchumi kupata ushauri muafaka kwenye jambo hili, lakini tukiendelea kulibeba kisiasa tutaendelea kuimiza nchi yetu kiuchumi.
 
Kwahiyo wakitangaza mshahara kupanda, bei za huduma zinapanda, mbona wakijenga barabara na miundombinu mingine bei hazipandi kwakuwa hiyo miundombinu watu wameiona na kusikia?
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali imejifunza kuwa inapotangaza hadharani kuhusu kupandishwa mishahara, kumekuwa kunatengeneza gharama kubwa na kusababisha ugumu wa maisha ya wengine.

Ameeleza hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Konde (ACT-Wazalendo) Khatib Haji aliyehoji ni lini Wafanyakazi wa Tanzania watapandishiwa mishahara na kuboreshewa maslahi.

Waziri Mkuu amesema, "Eneo la Wafanyakazi peke yake ukitangaza hadharani kwamba tumepandisha mishahara kwenye masoko, vituo vya mabasi na huduma nyingine zote zinapanda".

Amekiri ni kweli wafanyakazi wengi wanasubiri kusikia kupanda kwa mishahara akisema hilo likifanyika linatengeneza ugumu wa maisha, hivyo bado Serikali inaendelea kutafuta njia nzuri ya kuongeza maslahi ya mtumishi.

Aidha, Waziri Mkuu ameeleza kuwa maslahi ya wafanyakazi hayapo kwenye mishahara tu bali pia kwa kuwapandisha daraja na kupunguza kiwango cha kodi.
Subuutuuu. Waongeze mishahara wasitangaze???!!!!
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali imejifunza kuwa inapotangaza hadharani kuhusu kupandishwa mishahara, kumekuwa kunatengeneza gharama kubwa na kusababisha ugumu wa maisha ya wengine.

Ameeleza hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Konde (ACT-Wazalendo) Khatib Haji aliyehoji ni lini Wafanyakazi wa Tanzania watapandishiwa mishahara na kuboreshewa maslahi.

Waziri Mkuu amesema, "Eneo la Wafanyakazi peke yake ukitangaza hadharani kwamba tumepandisha mishahara kwenye masoko, vituo vya mabasi na huduma nyingine zote zinapanda".

Amekiri ni kweli wafanyakazi wengi wanasubiri kusikia kupanda kwa mishahara akisema hilo likifanyika linatengeneza ugumu wa maisha, hivyo bado Serikali inaendelea kutafuta njia nzuri ya kuongeza maslahi ya mtumishi.

Aidha, Waziri Mkuu ameeleza kuwa maslahi ya wafanyakazi hayapo kwenye mishahara tu bali pia kwa kuwapandisha daraja na kupunguza kiwango cha kodi.
Mimi ninachowasihi Serikali katika hili, baada ya kufanya nyongeza kimya kimya na kitu ambacho ni kizuri sana, wazisisitize taasisi husika kuhakikisha kuwa zinawapa wafanyakazi wake barua zinazoelekeza nyongeza hizo, na taasisi zitakazokiuka hili basi zichukuliwe hatua.

Kuna baadhi ya HR wana tabia ya kuonyesha ongezeko la mshahara kwenye SALARY SLIP tu, huku mtu husika akiwa hajapewa barua yoyote ile. All of a sudden mtu anakuja kugundua kuwa ni kweli mshahara umeongezeka ila kiasi anacholipwa kumbe ni cha ngazi D wakati yeye yuko ngazi E. Kumbe hata alipokuwa yuko ngazi D, alikuwa analipwa mshahara wa ngazi C. Hiki kitu kinashangaza sana, kwamba mtu ana mshahara wake halafu bado kuna mtu mwingine mahali anakaa analazimisha kukaa anakula mshahara wa mtu mwingine, halafu huyo tena eti ndiyo HR?

Wasipofanya hivyo, wataongeza mishara halafu mishahara hiyo itaishia kuliwa na wenye meno. Kuna baadhi ya watu wachcahe sana nchi hii, wana meno na matumbo, halafu wengine hawana
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali imejifunza kuwa inapotangaza hadharani kuhusu kupandishwa mishahara, kumekuwa kunatengeneza gharama kubwa na kusababisha ugumu wa maisha ya wengine.

Ameeleza hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Konde (ACT-Wazalendo) Khatib Haji aliyehoji ni lini Wafanyakazi wa Tanzania watapandishiwa mishahara na kuboreshewa maslahi.

Waziri Mkuu amesema, "Eneo la Wafanyakazi peke yake ukitangaza hadharani kwamba tumepandisha mishahara kwenye masoko, vituo vya mabasi na huduma nyingine zote zinapanda".

Amekiri ni kweli wafanyakazi wengi wanasubiri kusikia kupanda kwa mishahara akisema hilo likifanyika linatengeneza ugumu wa maisha, hivyo bado Serikali inaendelea kutafuta njia nzuri ya kuongeza maslahi ya mtumishi.

Aidha, Waziri Mkuu ameeleza kuwa maslahi ya wafanyakazi hayapo kwenye mishahara tu bali pia kwa kuwapandisha daraja na kupunguza kiwango cha kodi.
Well articulated Hon. PM
 
Wenyewe waongeze kupanda kwa gharama za maisha hilo Ni Jambo jingine hata mshahara usipopada maisha hayarudi nyuma! Kuna watumishi wanakufa wengine wanastafu wataongezwa lini?
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali imejifunza kuwa inapotangaza hadharani kuhusu kupandishwa mishahara, kumekuwa kunatengeneza gharama kubwa na kusababisha ugumu wa maisha ya wengine.

Ameeleza hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Konde (ACT-Wazalendo) Khatib Haji aliyehoji ni lini Wafanyakazi wa Tanzania watapandishiwa mishahara na kuboreshewa maslahi.

Waziri Mkuu amesema, "Eneo la Wafanyakazi peke yake ukitangaza hadharani kwamba tumepandisha mishahara kwenye masoko, vituo vya mabasi na huduma nyingine zote zinapanda".

Amekiri ni kweli wafanyakazi wengi wanasubiri kusikia kupanda kwa mishahara akisema hilo likifanyika linatengeneza ugumu wa maisha, hivyo bado Serikali inaendelea kutafuta njia nzuri ya kuongeza maslahi ya mtumishi.

Aidha, Waziri Mkuu ameeleza kuwa maslahi ya wafanyakazi hayapo kwenye mishahara tu bali pia kwa kuwapandisha daraja na kupunguza kiwango cha kodi.
Ila Katelephone ni mtu wa kamba sana
 
Back
Top Bottom