mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,309
- 4,798
Majaliwa ameyasema leo Ijumaa Mei 6, 2022 wakati akizindua mradi wa Afya yangu unaofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Marekani (USAID).
Amesema kazi ya maandalizi ya sensa ya watu na makazi inaendelea nchini ambayo inaenda sambamba na anwani za makazi.
Majaliwa amewataka Watanzania kushiriki katika sensa ya watu na makazi na kwamba haitakuwa faida kwa Watanzania tu pekee bali na taasisi zote zinazofanya kazi na Serikali ya Tanzania.
Amesema kazi hiyo inaendelea na imefikia asilimia 86 katika kuikamilisha uwekaji wa anwani za makazi na kwamba kazi iliyobaki ni kuchomeka vibao kuonyesha mitaa.
“Ingawa vibao vingine vimeandikwa kimakosa lakini najua yatarekebishwa. Juzi nilikuwa natembea nikaona bango moja limeandikwa Mahakama load badala ya Road (barabara) imeandikwa load,”amesema.
Majaliwa amewataka makatibu tawala kuangalia usahihi wa majina ya mitaa hiyo.
“Wanapoandika majina haya mhakiki mara mbili mbili. Msikubali kwenda kubandika kibao kikiwa kimekosewa. Yapo majina ya watu yahakikiwe vizuri,”amesema.
Amesema kuna bango moja limeandikwa kimakosa Feed Force badala ya Field Force na lingine lilikuwa likiandikwa jina lake lakini limekosewa pia.
Chanzo: Mwananchi