Waziri Mkuu Majaliwa na uhalali wa maamuzi hadharani

Waziri Mkuu Majaliwa na uhalali wa maamuzi hadharani

"ndugu wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM......katika serikali yangu Kuna watu wanalegalega.....hawaendi na kasi yangu......naomba Kibali chenu nikaipange serikali yangu" Hii ni kauli ya Samia Suluhu Hassan katika mkutano mkuu wa CCM Dodoma.

Nadhani kauli hii imemtia wenge Waziri Mkuu, ameanza kuzunguka ili "ajiokoe". Kwa kufanya hivyo, anaandaa matukio, halafu anafanya anavyofanya

Majaliwa ni msanii sana !
 
Utapangua safu na Safu Ila Kama Hakuna system zinazofanya kazi Ni kazi bure..

Ufisadi aliuibua PM kwa taarifa yenu uliofanywa chini ya Mwendazake na Wala sio mgeni na umejulikana toka kitambo Ila Hakuna Cha kufanya maana DED wa Sumbawanga mfano Ni ndugu wa Magufuli na Ni nyoka....
Makosa ya kiserikali,na kuteua makada wa chama kuwapa nafasi za kiutendaji imedhoofisha ufanisi wa taasisi zinazosimamia hizi Mamlaka za Serikali.

Taarifa za ndani za Serikali zinajadiliwa mbele ya kamera,hii ni kuidhofisha Serikali mbele ya wananchi bila kujua.

Viongozi wafanyiwe mafunzo ya kiutawala na uendeshaji na maadili, bila kuzingatia na kurekebisha haya siku ya uchaguzi huru na haki hakuna atayechaguliwa sio mfanya kiki wala chama.
 
Lazima ajikite kwa watu wa chini kwa sababu huku ndiko Kuna miradi ambayo watu wa kawaida wanaiona na pia ndiko anaweza kukutana naonkwa kiki n...
Sawa. Ila yeye kwa cheo chake alitakiwa awabane hao wa juu ili kuleta Uwajibikaji kwa wale wa chini. Tanzania ni nchi kubwa sana.

Hata afanyeje hataweza kugusa kila mahali. Kama siyo kutafuta kiki basi ajikite kwenye report ya CAG atuonyeshe huo uchapakazi wake. Madudu yanayoibuliwa na CAG pia yana audit report.
 
Leadership style hii ya kutumbua majipu hadharani, iltamalaki kipindi cha Serikali ya awamu ya tano.

-Waziri Mkuu ni zao la Serikali ya awamu ya tano,kwa hiyo anaendeleza leadership style ya awamu iliyopita.
-Leadership style hii haikuwa fair wakati ule na sasa hivi.

-Sina uhakika Kama watumishi wote walioadhirika na leadership style hii wamepata relief baada ya kufanya uchunguzi na kuonekana hawana hatia. -watendaji wetu,wawe Wazalendo,na watumie rasilimali chake tulizo nazo.

-wanaotumbuliwa ni wachache tu , asilimia kubwa ya watendaji wa Serikalini na mashirika ya umma siyo wasafi.

-Waziri Mkuu anachofanya,mara nyingi,ni kuwasimamisha kazi watuhumiwa,ili kupisha uchunguzi,kwa mfano leo,amewasimamisha kazi Mhasibu na Mkurugenzi huko Sumbawanga, baada ya wahusika kutuhumiwa kwa kuungua nyaraka nyeti za mradi katika mazingira ya kutatanisha.

Ushauri
1. Serikali iweke mifumo sahihi na endelevu wa kufanya kazi.

2. Mawaziri wa kisekta watimize majukumu yao kuondoa muhali.

3. Mahakama ifanye kazi kwa weledi,itoe haki bila upendeleo.

4. Vyombo vya uchunguzi vifanye kazi kwa weledi na kwa muda mfupi.

5. Watuhumiwa wawekwe pembeni kupisha uchunguzi.Lakini ifanyike kwa wahalifu wote,pasiwe na double standard.

6. Serikali na vyombo vyake vya uchunguzi ,viwe vinawasafisha watuhumiwa wote, ambao wamebainika hawana makosa,kwa maana kuna waadhirika wengi wa maamuzi haya ambao hawajui hatima yao toka awamu tano na wengine wamefariki

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Tumeshuhudia Waziri Mkuu Majaliwa, akikemea hadharani, watuhumiwa (Innocent Till Proved Guilty Under the court of law) Kwa Mujibu wa Vyanzo vyake. Watuhumiwa Hao Wa makosa mbalimbali, Ni watendaji Wa Kada za Chini Na za kawaida, Hasa Tamisemi, Elimu. n.k.

Japo kukemea kunarekebisha Tabia, lakini Kuna tatizo lililojificha ndani ya tatizo.

Mosi, Waziri Mkuu Ni Mtendaji Mkuu Wa shughuli zote za kila siku za Serikali. Je, Yeye Kama Mkuu, anakuwa wapi kusimamia na kuhakikisha Kuna Udhibiti (checks & controls) ndani ya Serikali, mpaka tunayoaminishwa kuwa Ni madudu yanatokea?

Pili, Kama taarifa anazopata Ni sahihi, Je Hao wanaopaswa kukamata, kushitaki Na kutoa haki wanakuwa wapi, mpaka wasubirie aje yeye amtaje mtuhumiwa, ambaye bado hajafikishwa mahakamani, kuwa Ni mkosaji?

Je, hizi Sio staged events (matukio ya kupangwa) ili kutuhadaa Sisi wananchi?

Je, mahakama ikimkuta mtuhumiwa Hana hatia, Waziri Mkuu atarudi Tena kutupa taarifa kuwa yule mtuhumiwa niliyemhukumu hadharani Hana hatia. Je pernality damage anayoifanya Kwa mtuhumiwa itafidiwa namna gani?

Je, Mamlaka ya Waziri Mkuu, ya kuwajibishana ndani Kwa ndani yamekuwa hafifu namna hiyo mpaka yapewe nguvu Na vyombo vya habari?

Je, Kuna muunganiko Mzuri kweli Kati ya Mamlaka ya Waziri Mkuu Na Mawaziri, Manaibu Waziri, Makatibu Wakuu Na Manaibu Makatibu Wakuu Wa Wizara husika? Wao wanakuwa wapi kukemea hayo, au wanamuacha aje atengeneze Jina Kwa wananchi?

Je, hizi ni kampeni za kuniaminisha kwa wananchi kuwa ni mchapakazi?

Nawasilisha.
Tatizo la wabongo lipo palepale,hamtaki waovu,walarushwa washughurikiwe.Wasiposhughurikiwa mnakuja hoo serikali hii chovu sana.Hamueleweki.
 
Tumeshuhudia Waziri Mkuu Majaliwa, akikemea hadharani, watuhumiwa (Innocent Till Proved Guilty Under the court of law) Kwa Mujibu wa Vyanzo vyake. Watuhumiwa Hao Wa makosa mbalimbali, Ni watendaji Wa Kada za Chini Na za kawaida, Hasa Tamisemi, Elimu. n.k.

Japo kukemea kunarekebisha Tabia, lakini Kuna tatizo lililojificha ndani ya tatizo.

Mosi, Waziri Mkuu Ni Mtendaji Mkuu Wa shughuli zote za kila siku za Serikali. Je, Yeye Kama Mkuu, anakuwa wapi kusimamia na kuhakikisha Kuna Udhibiti (checks & controls) ndani ya Serikali, mpaka tunayoaminishwa kuwa Ni madudu yanatokea?

Pili, Kama taarifa anazopata Ni sahihi, Je Hao wanaopaswa kukamata, kushitaki Na kutoa haki wanakuwa wapi, mpaka wasubirie aje yeye amtaje mtuhumiwa, ambaye bado hajafikishwa mahakamani, kuwa Ni mkosaji?

Je, hizi Sio staged events (matukio ya kupangwa) ili kutuhadaa Sisi wananchi?

Je, mahakama ikimkuta mtuhumiwa Hana hatia, Waziri Mkuu atarudi Tena kutupa taarifa kuwa yule mtuhumiwa niliyemhukumu hadharani Hana hatia. Je pernality damage anayoifanya Kwa mtuhumiwa itafidiwa namna gani?

Je, Mamlaka ya Waziri Mkuu, ya kuwajibishana ndani Kwa ndani yamekuwa hafifu namna hiyo mpaka yapewe nguvu Na vyombo vya habari?

Je, Kuna muunganiko Mzuri kweli Kati ya Mamlaka ya Waziri Mkuu Na Mawaziri, Manaibu Waziri, Makatibu Wakuu Na Manaibu Makatibu Wakuu Wa Wizara husika? Wao wanakuwa wapi kukemea hayo, au wanamuacha aje atengeneze Jina Kwa wananchi?

Je, hizi ni kampeni za kuniaminisha kwa wananchi kuwa ni mchapakazi?

Nawasilisha.
Wcha ufisadi utafungwa

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
"ndugu wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM......katika serikali yangu Kuna watu wanalegalega, hawaendi na kasi yangu. Naomba Kibali chenu nikaipange serikali yangu" Hii ni kauli ya Samia Suluhu Hassan katika mkutano mkuu wa CCM Dodoma.

Nadhani kauli hii imemtia wenge Waziri Mkuu, ameanza kuzunguka ili "ajiokoe". Kwa kufanya hivyo, anaandaa matukio, halafu anafanya anavyofanya
Acheni kumnanga majaliwa ni bora mara mia huyu majLiwa kuliko

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Kwa Mamlaka ya Waziri Mkuu, anayo nguvu kubwa kuwawajibisha watendaji ndani Kwa ndani bila kupiga makelele. Uchunguzi unafanyika, ushahidi unapatikana, mtu anakamatwa, anafunguliwa kesi, anahukumiwa Na mahakama Kwa haki, anatumikia kifungo.

Hapo Sasa hata akienda Hadharani kumtaja mhusika ambaye tayari kahukumiwa inakuwa Na mshiko. Hii ya kutangaza mtuhumiwa ambaye bado hajathihitishwa Na mahakama kuwa Ni mkosaji, tenahadharani, Kisha unatoa Amri akamatwe, Kuna kasoro ndani ya Nia Thabiti.

Na Tena unakuwa umejibebesha Mamlaka ya Mahakama YA kuhukumu mtuhumiwa, ambaye endapo atathibitika Hana hatia, Basi unakuwa umesababisha personality damage kubwa, at the expense ya kujibebea umaarufu.
Kuwataja kuna faida zake pia,inakuwa ni alert kwa wengine kujua kwamba ufuatiliaji upo na hatua zinachukuliwa hivyo wengine kuogopa kufanya matendo hayo
 
Hii Nchi ina mfumo ukiofeli maana unategemea uadilifu binafsi wa mtu Sasa kwenye jamii hao waadilifu Ni wachache wanazidiwa na waovh wengi kwa msingi huo muadikifu 1 ataonekana Ni kikwazo kwa wengi Majizi..

Bila kuweka syastem zinazofanya kazi na hapa Katiba itoe Nguvu Wananchi wamchague Mkuu wa Mkoa na wawe na nguvu ya kumuondoa pindi Mambo yakiharibika Tena bila mlolongo Ni just petition kadhaa Basi, Mkurugenzi tunuajiri sie wenyewe asiletwe na Tamisemi maana Madiwani hawana nguvu yeyote kwake.

Lakini huu upuuzi wa kutegemea watu wakupe taarifa ndio uje kujiongelesha na kuwataka wakuchunguza wafanhe kazi Yao haina tija yeyote..

Kwa hili Serikali ya CCM inatukosea sana.
Mama yako anaupiga mwingi endelea kukenua meno yote,acha ukigeugeu
 
Kuna udhalilishaji na kiki, nchi nyingi haziongozwi namna hii (kudhalilisha,kufokea hadharani),na inawezekana Wanakosea lakini hamna mtu wa kuwarekebisha viongozi wavunjao sheria za kiutumishi.

Wengi wafanyao hivi walimuiga mwendazake,ukifuatilia awamu zilizopita viongozi walikuwa hawaingilii majukumu ya watendaji,wala kuwadhalilisha watumishi walio chini yao mbele ya kamera.

Kwani viongozi hawana utaratibu wa kufanya kazi mpaka wasubiri kamera ma vyombo vya habari ili kuonyesha mapungufu ya kiutendaji yaliyopo Serikalini?

Viongozi wamesahau agenda za kuwahudumia na kuwapa majibu ya matatizo yanayowakabili wananchi (ukosefu wa huduma ya maji, barabara,kupanda bei bidhaa mbalimbali bila udhibiti,) badala yake wanafanya maigizo hadharani.

Viongozi wajue yote haya yafanyayo hadharani wananchi wanawachora tu (Viongozi badala ya kutoa majibu ya kero za wananchi,kiongozi anaenda kutoa matamko,kufokea watumishi walio chini yake mbele ya kamera huku akijua anavunja sheria,kanuni na taratibu za nchi),na kusahau wajibu wa nafasi walizopewa.
Kwahiyo mnafurahia watu wanapora mali ya umma kisha wanachoma nyaraka?[emoji706][emoji706]
 
At least yeye kaonesha njia ya kufanya watu kuwajibika na hawawezi kujisahau. Kukosea kupo tuu, Magufuli alisema acha tukosee tutarekebisha mbele kwa mbele
 
Utapangua safu na Safu Ila Kama Hakuna system zinazofanya kazi Ni kazi bure.

Ufisadi aliuibua PM kwa taarifa yenu uliofanywa chini ya Mwendazake na Wala sio mgeni na umejulikana toka kitambo Ila Hakuna Cha kufanya maana DED wa Sumbawanga mfano ni ndugu wa Magufuli na Ni nyoka..

Kuweka maafisa usalama wa vyeo vya Juu kwenye Ngazi za maamuzi ni upuuzi maana wakipiga Pesa huna Cha kuwafanya hao hao ndio unategemea taarifa kutoka kwao.

Mfano wa mwisho DED wa Kahama alinunua Shangingi kwa makusanyo ya Halmashauri mil.450 na Mwendazake hakuwa na Cha kufanya zaidi ya kijisemesha ooh ameongza makusanyo na blaa blaa za kipumbavu kisa Ni manyoka hao wakipiga Hakuna wa kuwagusa.
Huyu mwamba usipomtaja account yako haisomi?[emoji706][emoji706]
 
Maswali yako nimeyapenda. Unachosema ni kweli kabisa Nami pia nilishawaza hilo.

Kwa kweli kinachoendelea ni WM kujitafutia uwanja wa kujionyesha kuwa ni mchapa kazi. Kama ni kweli kwa nini amejikita kwa watu wadogo wadogo wa ngazi za chini.

Angeaminika zaidi pale atakapowaibua wale Wateule wanakula kwa urefu wa kamba zao.
Wengine ni wateule wa mkubwa wake,anachofanya ni kumpa taarifa na kumshauri,hilo linabaki kwa anayeupiga mwingi,kuubeba ushauri au kuupotezea
 
SIO KWA LICHAMA CCM ! Majizi Hayo hayataki udhibiti ! Hakuna mwana ccm hata mmoja asiye mwizi! Japokua na wale wa vyama vingine wanaweza kua wezi pia maana pia ni wa TZ
Wabongo wezi ila CCM nayo ni majizi yaliyokubuhu. Yametunyonya sana watanzania
 
Huyu mwamba usipomtaja account yako haisomi?[emoji706][emoji706]
Hawezi kwepa haya ya ufisadi maana Miaka 6 amekuwepo Madarakani na hii miradi mingi aliiacha.
Hakuna mradi hata mmja ambao pm kakagua huko Rukwa ambao Umeanza awamu hii,na hiyo miradi Pesa zilikuwa na haikukamilika..

Zama za Mwendazake aliyeaminisha watu kwamba Serikali take hainaufisadi Hakuna mtu angethubutu kusema Kuna ufisadi ili amuaibishe bwana mkubwa.
 
Back
Top Bottom