Waziri Mkuu Majaliwa na uhalali wa maamuzi hadharani

Lazima ajikite kwa watu wa chini kwa sababu huku ndiko Kuna miradi ambayo watu wa kawaida wanaiona na pia ndiko anaweza kukutana naonkwa kiki nk...
Ni kwa nini katika ziara zake viongozi wa kisiasa hawaguswi hata wakiwa na madudu? Wakuu wa wilaya za Nsimbo Katavi na Kalambo Rukwa wamehusika wazi wazi kuhujumu miradi ya hospitali za wilaya/vituo vya afya katika maeneo yao.

Lakini hakuna waliposimamishwa kudhalilishwa. Kituo cha afya Nkomolo wikaya ya Nkasi hakuna kiongozi amepekekwa pale tangu kilipofanyiwa ukarabati 2017 na Takukuru na Usalama wanajua nani walifanya nini pale.

Juzi waziri mkuu katoka huko lakini hata kupitishwa njia ya karibu na Kituo hicho hakupita. RIP Kanumba, umesaidia watanzania wote kuwa wasanii.
 
Sasa hayo maswali yako mawili ndo umeuliza nn??

Embu tumpongeze Majaaliwa hata Kwa hiki kidogo anachoonesha.
 
Inawezekana anawataja Hadharani wale wasio wateule Wa Rais, ambao yeye anawatuhumu, Na Sio Uthibitisho Wa kimahakama.
 
Sasa hayo maswali yako mawili ndo umeuliza nn??

Embu tumpongeze Majaaliwa hata Kwa hiki kidogo anachoonesha.
Tunampongeza. Swali la kujiuliza, Ni Je Yeye Kama mtendaji Mkuu Wa Serikali, amekuwa wapi kusimamia hayo ndani Kwa ndani yasitokee, anapilalamika kwenye Kamera Kama mwananchi Wa kawaida, anatuchanganya. Kumbuka kufeli Kwa internal Control ya Serikali, Ni kufeli kwake pia. Yeye Ni Mtendaji. Na vpi ikithibitika mahakamani kuwa anawataja hawana hatia. Atawasafisha?
 
Mchakato Wa kumuondoa PM Ni ule ule Kama Wa kumuweka madarakani. Vipi Kama Bunge likagoma, kumuondoa Kwa Kura?

Sent from my CPH2159 using JamiiForums mobile app
 
Hizi ni drama tu za kuzugia wadanganyika!

Pm anjaribu kutumia mbinu za mwendazake kutafuta cheap popularity ili kumblackmail Rais Samia!

Serikali haiwezi kuendeshwa kienyeji namna hiyo. This is a recipe for future troubles.
 
Hizi ni drama tu za kuzugia wadanganyika!

Pm anjaribu kutumia mbinu za mwendazake kutafuta cheap popularity ili kumblackmail Rais Samia!

Serikali haiwezi kuendeshwa kienyeji namna hiyo. This is a recipe for future troubles.
Mbinu ya kumtaja mtuhumiwa Hadharani Kama mkosaji, inaharibu Sana Sifa yake. Kama Ni kweli kafanya Ni Sawa, lakini Kama bado Ni tuhuma, Basi ikithibitika mahakamani kuwa hakuwa Na kosa, inakuwa imemharibia Sifa Na hakuna mtu ataenda Hadharani Tena kumsafisha.

Nadhani mifumo ya ndani ya uwajibishanaji, ingetiliwa mkazo, uchunguzi ufanyike, mtu afunguliwe mashtaka, na akihukumiwa mahakamani Basi atangazwe. Vinginevyo Ni maigizo.
 
Kujigeuza mahakama Hadharani, haijakaa vizuri. Imagine Kama Rais anamnanga PM Hadharani, itakuwaje?
 
nchi nyingi PM ndio kiongozi wa serikali, anateua mawaziri na makatibu wa wizara....... yeye ndio anawajibika kwa kila kitu kuhusu uongozi wa serikali

yeye (PM) ndio anateuliwa na Raisi, nchi za Asia zimefanikiwa sana kwa njia hii......

anyway, sijui nataka kusema nini, ....ila ni hivi nchi hii raisi ana mamlaka makubwa mno alafu mara nyingi huwa tunachagua maraisi ambao ni wepesi,
 
Kwani Wabunge Wanaotoka Kusini Ni Wangapi
Hata Wasipokuwepo Bunge Litaendelea
Nitapiga Shangazi Zake
 
Mamlaka ya uteuzi haihitaji kura za Bunge kumuondoa, Bunge Wana uwezo wa kupiga kura za kutokuwa na imani kwa PM
Mamlaka ya Uteuzi ikikasirika, haina haja ya kupeleka Bungeni Sio?
Lakini Bunge linaweza kumkataa PM bila idhini ya Rais, vp Rais akigoma?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…