Waziri Mkuu na Bunge wanataka kutafakari nini wakati walipitisha kwa 100%

Waziri Mkuu na Bunge wanataka kutafakari nini wakati walipitisha kwa 100%

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
22,227
Reaction score
49,628
Nimemsikia Mbunge Lucy Mayenga akiwaomba wabunge wenzake watafakari upya kuhusu mkataba wa DP World.

Wakati huo huo Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa amesema hawatapuuza maoni ya wananchi wanayotoa kuhusu huo mkataba.

Hii tafsiri yake nini, ni kuwa Wabunge na WM wamegundua kosa lao, kuwa hawakutafakari kabla ya kuupitisha na walidharau maoni ya wananchi, kwanini hawakutafakari na kwa nini walidharau kelele za wananchi, sababu kuna baadhi ya watu kwa propaganda zao na maslahi yao wametumika kuupotosha Umma na kulipotosha Bunge.

Hebu fikiria Mb kama Musukuma asiye na uelewa wowote wa mikataba ya kimataifa, na mwandishi wa habari kama Kitenge kwa vile tu walitembelea ofisi za DP World na kukuta komputa zimepangwa vizuri wakadhani ndio ufanisi wenyewe, watu kama hawa wana faida gani kwa bunge na taifa.

Ifikie mahali watu wa aina hii wakiwemo Wabunge, waandishi wa habari au mtu yeyote anayeeneza habari za kupotosha Umma kwenye jambo kubwa kama hili na kuiingiza nchi kwenye hasara kubwa wahesabiwe kama WAHAINI, hawaisaidii nchi hawamsaidii rais, wakati wowote wanaweza kununuliwa na mataifa ya nje kwa tamaa zao na kufanya propaganda za uongo na kiliingiza taifa kwenye machafuko makubwa.

Hongera Waziri Mkuu na Bunge kuanza kutambua kuwa kuna watu wanafanya propaganda za uongo kwenye huu mkataba, nilijua kukaa kwako kimya ulikuwa hupendezwi na watu wa aina hiyo.

Nakutakia wewe binafsi na Bunge muwe na tafakuri njema kwa maslahi mapana ya Taifa letu.
 
ukiona mtu anijitamba ajasoma alafu kuwakebei wenzake walio soma.
muogope sana sawa na mjinga kuwaona wajanja ni wajinga.
 
Nimemsikia Mbunge Lucy Mayenga akiwaomba wabunge wenzake watafakari upya kuhusu mkataba wa DP World.

Wakati huo huo Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa amesema hawatapuuza maoni ya wananchi wanayotoa kuhusu huo mkataba.
Naona wewe ni mgeni na usanii wa kitz
 
Hebu fikiria Mb kama Musukuma asiye na uelewa wowote wa mikataba ya kimataifa, na mwandishi wa habari kama Kitenge kwa vile tu walitembelea ofisi za DP World na kukuta komputa zimepangwa vizuri wakadhani ndio ufanisi wenyewe, watu kama hawa wana faida gani kwa bunge na taifa.
😂😂😂
 
DP World na wao wamekurupuka hawakuisoma Tz vizuri kisiasa ipo unstable sana na hilo ni kosa kubwa katika uwekezaji, baada ya wananchi kuanza kupiga kelele mpaka huko twitter ndipo wanapata picha halisi tofauti na viongozi wachache walivyowaaminisha, hili linawapa mashaka na navyohisi DPW imezungumza na serikali kuhusu ushirikishwaji wa wananchi, haya makampuni ya kigeni yanajua nguvu ya umma, nachoweza kusema DPW was misinformed, DPW itakuwa wanafuatilia maoni ya wananchi, wanasiasa, wanasheria n.k na wamegundua kuna jambo halipo sawa.
 
Nimemsikia Mbunge Lucy Mayenga akiwaomba wabunge wenzake watafakari upya kuhusu mkataba wa DP World.

Wakati huo huo Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa amesema hawatapuuza maoni ya wananchi wanayotoa kuhusu huo mkataba.

Hii tafsiri yake nini, ni kuwa Wabunge na WM wamegundua kosa lao, kuwa hawakutafakari kabla ya kuupitisha na walidharau maoni ya wananchi, kwanini hawakutafakari na kwa nini walidharau kelele za wananchi, sababu kuna baadhi ya watu kwa propaganda zao na maslahi yao wametumika kuupotosha Umma na kulipotosha Bunge.

Hebu fikiria Mb kama Musukuma asiye na uelewa wowote wa mikataba ya kimataifa, na mwandishi wa habari kama Kitenge kwa vile tu walitembelea ofisi za DP World na kukuta komputa zimepangwa vizuri wakadhani ndio ufanisi wenyewe, watu kama hawa wana faida gani kwa bunge na taifa.

Ifikie mahali watu wa aina hii wakiwemo Wabunge, waandishi wa habari au mtu yeyote anayeeneza habari za kupotosha Umma kwenye jambo kubwa kama hili na kuiingiza nchi kwenye hasara kubwa wahesabiwe kama WAHAINI, hawaisaidii nchi hawamsaidii rais, wakati wowote wanaweza kununuliwa na mataifa ya nje kwa tamaa zao na kufanya propaganda za uongo na kiliingiza taifa kwenye machafuko makubwa.

Hongera Waziri Mkuu na Bunge kuanza kutambua kuwa kuna watu wanafanya propaganda za uongo kwenye huu mkataba, nilijua kukaa kwako kimya ulikuwa hupendezwi na watu wa aina hiyo.

Nakutakia wewe binafsi na Bunge muwe na tafakuri njema kwa maslahi mapana ya Taifa letu.
PM yeye ni opportunist TU,Huwa hajulikani yupo upande Gani,yeye anacheki maslahi yake TU,karama Moja aliyonayo ni "state man"anamzidi hata Makamu mpango na Samia,
Majaliwa awe Raisi,rose migiro Waziri mkuu,CAG Abbas,nchi ingefika mbali,
Badala ya ccm kututafutia ajira,yanauza bandari zetu,
 

Attachments

  • 20230621_084555.jpg
    20230621_084555.jpg
    782 KB · Views: 4
DP World na wao wamekurupuka hawakuisoma Tz vizuri kisiasa ipo unstable sana na hilo ni kosa kubwa katika uwekezaji, baada ya wananchi kuanza kupiga kelele mpaka huko twitter ndipo wanapata picha halisi tofauti na viongozi wachache walivyowaaminisha, hili linawapa mashaka na navyohisi DPW imezungumza na serikali kuhusu ushirikishwaji wa wananchi, haya makampuni ya kigeni yanajua nguvu ya umma, nachoweza kusema DPW was misinformed, DPW itakuwa wanafuatilia maoni ya wananchi, wanasiasa, wanasheria n.k na wamegundua kuna jambo halipo sawa.
Shirika kubwa kama DP World ambalo linamilikiwa na serikali, haliwezi kufanya uwekezaji mkubwa kama huu bila kufanya upembuzi yakinifu kuhusu hatari ambazo zinaweza kuukumba uwekezaji wao (Contingent and Risk Assessment). Hata wakoloni kabla ya kuanza kuiba huku Afrika walianza kutuma wapelelezi na wamishonari kutengeneza mazingira, kitu ambacho DP World wamekifanya sana.

Mambo ambayo waarabu wamekuwa wakiyafanya kabla ya kuja kuwekeza hapa Tanganyika, hayana utofauti wowote ule, na yale mambo wakoloni walifanya kabla ya kuja kutawala Afrika kinyemela. Walitumia wapelelezi (Explores), wamishionari na dini (Missionaries and Religion), na wafanyabiashara (Traders/Business Men). Baada ya miaka zaidi ya 200, hakuna kilichobadilika kabisa, mbinu hizi zinatumiwa na wachina, wahindi, wamarekani na sasa waarabu. Ubaya ni kwamba hakuna anayestuka kabisa, mijitu inauza nchi kwa kukenua meno.

Au unadhani ni Tanganyika tu ndiyo tunawalalamikia DP World ? Hapana. Kule Marekani DP World walikataliwa kabisa na bunge la Marekani kumilikishwa bandari za Marekani kwasababu za kiusalama, hivyo likatengenezwa shirika ambalo linashirikiana na DP World ila linaendeshwa na Wamarekani. Kule Uingereza nako DP World inalalamikiwa kwa kuumiza maelfu ya wafanyakazi ambao wa shirika la bandari, P & O Ferries ambalo lilinunuliwa na DP World katika uwekezaji wake.

Wafanyakazi wa kizungu wameamka tu, wakakuta vibarua vimeota nyasi bila sababu yoyote ile na mwarabu hajatoa maelezo. Kule Uingereza wana sheria kali mno ambazo zinalinda ajira za wafanyakazi, lakini bado wakafukuzwa, sembuse wale watanganyika wanaofanya pale bandarini kwa kupelekwa kupitia vimemo vya mama na mjomba ilhali hawana uwezo! Unadhani watapona kweli ?

Tukirudi hapo Djibouti. DP World waliingia ubia (Joint-Venture) na serikali ya Djibouti ili kuendeleza bandari na maeneo maalum ya kibiashara (Special Economic Zones). Wakasainishwa mkataba kama huu wa kwetu, tena wa ulikuwa una afadhali kwasababu wenyewe walitengeneza kampuni binafsi ambalo liliifanya serikali ya Djibouti imilikia hisa asilimia 64% kwenye ule ubia.

Siku zilivyoenda mwaraba wa DP World hakuendesha bandari ya Doraleh kwa kasi ambayo ilitegemewa, hivyo Djibouti ikalipa kampuni la Uchina, China Merchants ruhusa ya kutengeneza eneo maalamu la biashara (Special Economic Zones) na kuendeleza bandari ya Doraleh. Bwanaa, bwanaa, mwarabu ilhali hajaendeleza chochote kwenye ule ukanda akaamua kufungua kesi kwenye mahakama za Hong-Kong akiwashitaki Djibouti na China Merchants, akitaka alipwe fidia ya dola za Kimarekani milioni 200.

Moja ya sababu ni kwamba, Uchina ametumia rushwa kuwalaghai Djibouti ili apewe fursa ya uwekezaji. Huku sababu nyingine ikiwa ni uvunjifu wa haki ya DP World kumiliki fukwe zote za Djibouti bila kuingiliwa (Breach of Exclusive Right of DP World to own all ports and economic zones of Djibouti). Katika maana nyingine ni kwamba DP World wakisaini mkataba na wewe hawakuruhusu kabisa kukaribisha mwekezaji mwingine. Kama kuna fursa basi inabidi uwape wao kwanza, na hata kama hawatafanya chochote kila huwezi kuwafanya chochote.

Kila siku nilikuwa najiuliza ni kwanini wakomunisti wa Urusi (Bolsheviks) waliamua kuingia mtaani na kumuua mfalme Nicholas Ramanov na familia yake yote kikatili, huku wakipiga risasi na kuwanyonga maelfu ya watawala wa nchi ile pamoja na viongozi wa dini. Nilisoma lakini sikuwahi kuelewa kwanini mwanadamu anaweza kufanya ukatili wa namna ile. Nimefika umri huu sasa naanza kupata picha kwamba mwanadamu anaweza kuwekwa kwenye mazingira fulani, halafu akageuka kuwa mnyama.

Wabunge wa Tanganyika walichokifanya dhidi ya watu wao ni dhambi kubwa ambayo haiwezi kusameheka hata kidogo. Wametuhadaa na kutudharau sisi raia wao kwa kuhongwa tende na halua za waarabu. Nchi za watu wenye akili timamu, leo hii bunge la Tulia Ackson lingeshakuwa A Pile of Dust.
 
Back
Top Bottom