Waziri mpya wa Mawasiliano, anza kazi na Azam Media. Wamepanga kutupiga kwenye vifurushi vipya

Waziri mpya wa Mawasiliano, anza kazi na Azam Media. Wamepanga kutupiga kwenye vifurushi vipya

Ikiwezekana ifike hata 50k angalau kama watanganyika wataelekeza mawazo kwenye mambo ya msingi yanayoihusu nchi, hii Simba na yanga imewapumbaza sana watu wengi.
 
Ndugu Mteja, kuanzia 1/8/24 kutakuwa na mabadiliko ya bei. Kifurushi cha 25000 kuwa 28000; 17000 kuwa 19000; 10000 kuwa 12000; 6000 kuwa 7000 na 3000 kuwa 4000.

Azam decoder hawana Ubora kuzidi Dstv, Wanatumia kigezo cha kutuonyesha mipira Ili kuchaji gharama zaidi, ongezeko hilo ni kama blackmailing, hakuna media nyingine wanaowapa ushindani kwenye mpira kwa Sasa. Ongezeko hilo sio halisia na maisha ya wananchi, ajabu Mzawa mwenzetu anatunyonya kuliko wageni wawekezaji.

Mmesubiri home boy apigwe chini ndio mlete ongezeko! Waziri nakusihi, liangalie kwa jicho la wananchi wanyonge..


Azam Media wameanza uwizi wa wazi wazi, yaani wanapandisha vifurushi vyao kiholela tena bila hata barua ya TCRA, wala TCRA kupitia madai yao ya kupandisha bei vifurushi vyao, huu ni wizi, TCRA inafaa wasimamishe hizo bei mpya hadi waangalie kama kuna haja ya kuongeza bei..!!
 
Package ya mpira ongezeko ni 3000 wakati package zisizo na mpira wameongezwa 1000.sijawahi ona ongezeko kubwa kiasi hicho, kwenye maisha haya magumu ya Bei za vitu kuwa juu
Basi kama ongezeko ni package zote hiyo sababu ya kurusha ligi ya Spain ni sababu haina maana
 
Badala umwambie aje kuung'oa mzizi wa matapeli wa mitandaoni

Inazungumzia kuhuau vifurushi
 
Azam wameleta VAR sasa wamepanga kutupandishia vifurushi vya ving'amuzi!

Hii si sawa bora wapate mpinzanj kwenye kuonesha ligi za nyumbani ili wasitunyanyase!
 
Azama ni kampuni binafsi, acha uboya.
 
Hivi nchi za wenzetu,ivi vitu ni gharama namna hii?? Vp na internet bundle??sema levels za maisha kwa apa bongo ni tofauti ukiwaza ulipe kodi ya nyumba,ulipie bills za umeme+maji,na vifurushi vya king'amuzi navyo kulipia😂😂
 
Kwani Azam wanapata ruzuku serikalini? Hii ni biashara ya mtu binafsi na mfanya biashara yoyote lengo ni faida. Haya mambo hayamuhusu waziri wala serikali ni maamuzi ya kampuni binafsi hata sokoni tunaenda tunakutana na bei mpya lakini tunanunua. Kwa Azam kama huliwezi ni kuhamia sehemu unayoweza hakuna aliyelazimishwa kununua.

Nawashangaa wanaolalamika. At least ingekua ni tbc kweli.

Dawa yao ni kuacha kulipia, Wateja wote waweke mgomo baridi afu uone watavyomtesa bakhresa.
 
Azam Tv wanapandisha bei za vifurushi kiholela pasipo ongezeko la channels mpya.

Unapopandisha bei za vifurushi lazima kwanza uzingatie kuongeza channels mpya ambazo hazikuwepo ili kuweka uwiano kinyume na hapo wanatakiwa kudhibitiwa na Serikali.


Watakwambia wameongeza Cheka Plus TV, Azam Sports 4 na kununua laliga kwa bei kubwa.
 
Nawashangaa wanaolalamika. At least ingekua ni tbc kweli.

Dawa yao ni kuacha kulipia, Wateja wote waweke mgomo baridi afu uone watavyomtesa bakhresa.
Mgomo kwenye entertainment??ur kidding right? Vitu vya starehe kama ivi unajisumbua bure😂
 
Kumbe umetoa maoni ukiwa hujui chochote kuhusu hayo maongezeko
Kwa nn usingeanza utafiti ndio uje kutoa maoni?
Nahitaji kujiridhisha tu lakini ukweli upo wazi azam anatoa matangazo kwa bei rahisi sana kulinganisha satellite service provider wengine. Kwasasa East and central Africa ameshika soko.
Unadhani watu wengine hawapendi kushika hili soko? Tatizo uwezo hamna.
 
Nahitaji kujiridhisha tu lakini ukweli upo wazi azam anatoa matangazo kwa bei rahisi sana kulinganisha satellite service provider wengine. Kwasasa East and central Africa ameshika soko.
Kulinganisha na kina nani? Hapa naamini umefanya research h yo utakuwa na majibu
Anatoa bei rahisi kulinganisha na wengine kina nani?
 
Kulinganisha na kina nani? Hapa naamini umefanya research h yo utakuwa na majibu
Anatoa bei rahisi kulinganisha na wengine kina nani?
Kwa hapa ndani ana competitors kama dstv , startimes , zuku n.k .zaidi ya dstv hakuna service provider mwengine hapo anaeweza kuwa programs alizonazo azam mshindani mkuu wake ni dstv ambaye watanzania wengi wameshindwa afford service unataka watu waende wapi?
 
Back
Top Bottom