Waziri Mulamula: Watanzania walioko Ukraine wajitahidi waingie Poland. Wananchi msiwe na wasiwasi Serikali inafuatilia!

Waziri Mulamula: Watanzania walioko Ukraine wajitahidi waingie Poland. Wananchi msiwe na wasiwasi Serikali inafuatilia!

Unawaza kama mimi mkuu! Tena ubalozi upo kabisa pale salenda na kwa mujibu wa taarifa nilizonazo kati ya hao waTz 300+ waliopo UKRAINE 297 wapo mji wa mpakani na Urusi unaitwa Summy. Sasa kwanini wasivuke boda tu tena kwa miguu waende wakachukuliwe na ATCL Moscow?
Wizara inafanyia kazi mawazo yako.
 
Waziri wa Mambo ya nje Mh Mulamula amewataka watanzania takribani 300 walioko Ukraine wajitahidi waweze kuingia Poland ambako uratibu unafanyika.

Mulamula amesema ameona ubaguzi unaoendelea Ukraine kupitia mitandaoni na amesikitishwa sana lakini wananchi wasiwe na wasiwasi kwa sababu serikali inafuatilia kwa karibu sana.

Chanzo: ITV habari

Maendeleo hayana vyama!

Alichokiongea waziri Mulamula hakina maana wala msaada
Heri angekaa kimya tuu

Mungu wanusuru binadamu wasio na hatia

Mungu watembelee rais wa Russia na Ukraine ukawape moyo wa suluhu badala ya kumwaga damu zisizo na hatia
 
How ?
Wameshaongea na Poland ili kuwapokea hao watu mia tatu ?
Wakati kama huu ndio Ubalozi inabidi ufanye kazi yake..., sio tu kufanya photo shoot...
 
How ?
Wameshaongea na Poland ili kuwapokea hao watu mia tatu ?
Wakati kama huu ndio Ubalozi inabidi ufanye kazi yake..., sio tu kufanya photo shoot...
Balozi ni Dr Slaa......oooh sorry kumbe amestaafu.

Balozi yuko Sweden.
 
Hili neno' tunafuatilia kwa karibu' huwa silielewi kabisa..
 
Wacha mbaguliwe sababu hamjitambui kama binadamu, kila siku kulia Lia kwa hao wazungu wawasaidie.
 
Waziri wa Mambo ya nje Mh Mulamula amewataka watanzania takribani 300 walioko Ukraine wajitahidi waweze kuingia Poland ambako uratibu unafanyika.

Mulamula amesema ameona ubaguzi unaoendelea Ukraine kupitia mitandaoni na amesikitishwa sana lakini wananchi wasiwe na wasiwasi kwa sababu serikali inafuatilia kwa karibu sana.

Chanzo: ITV habari

Maendeleo hayana vyama!
Inafuatilia huku yupo Dar kwenye kiyoyozi
 
Waingie Poland kwa usafiri gani.

Hivi ukimwambia mtu aliyeko mtwara aingie Kenya bila msaada wa kumuwezesha kufika Namanga again ataingia kweli Kenya?

Watawezaje kufika huko na watakuwa wanakula nini?
Kwa ungo wa Sumbawanga labda, CCM wanadharau sn
 
Waziri anaangalia TV tu na kusema yale aliyosema. Imani yake ni walio nje wote ni watoto wa matajiri.
 
Msiwasumbue ccm sana kwani wanaweza wakasema bwana eeeee kwani sisi tuliwapeleka huko maana Hawa watu hawajui kile wakiongeacho
 
Waziri wa Mambo ya nje Mh Mulamula amewataka watanzania takribani 300 walioko Ukraine wajitahidi waweze kuingia Poland ambako uratibu unafanyika.

Mulamula amesema ameona ubaguzi unaoendelea Ukraine kupitia mitandaoni na amesikitishwa sana lakini wananchi wasiwe na wasiwasi kwa sababu serikali inafuatilia kwa karibu sana.

Chanzo: ITV habari

Maendeleo hayana vyama!
Kwa nini wasiende Urusi ambako ni karibu?
 
Et wana nchi wasiwe na wasiwasi.

CCM huwa hamjiongezi , Watu wameanza kuwatoa RAIA wao wiki kadhaa kabla ya Vita hiyo.

Nyie mnastuka saizi tena baada ya Raia kuhoji .

Sasa mipakani tu huko Ukraine, Waafrika wanabaguliwa ,hamna kuondoka , sisi wazungu kwanza ndo tunasepa .

Acha utoto. CCM ndo nini. Wale watoto walioko kule wamepelekwa na CCM. Unaingiza Siasa kwa mambo serious. Umejiuliza kwanini wazazi hawakuwatoa watoto wao mapema? Kusoma Ukraine [emoji1255] Nchi maskini lazima mzazi ajiweze. Je Tanzania Ina Ubalozi Ukraine au inategemea Huyu wa Ujerumani? Mambo haya sio rahisi sana. Wengi wanaenda nje bila kujisajiri kwenye Balozi husika au kujitambulisha tu. Shida ikitokea ndo Serikali mnaikumbuka. Ikifanya jambo lazima mtafute lawama. Umeambiwa Sasa wanafanya utaratibu wao wafike tu Poland. Unakuja na Vyama. Wewe chama gani mkuu. Fanya tofauti.
 
Acha utoto. CCM ndo nini. Wale watoto walioko kule wamepelekwa na CCM. Unaingiza Siasa kwa mambo serious. Umejiuliza kwanini wazazi hawakuwatoa watoto wao mapema? Kusoma Ukraine [emoji1255] Nchi maskini lazima mzazi ajiweze. Je Tanzania Ina Ubalozi Ukraine au inategemea Huyu wa Ujerumani? Mambo haya sio rahisi sana. Wengi wanaenda nje bila kujisajiri kwenye Balozi husika au kujitambulisha tu. Shida ikitokea ndo Serikali mnaikumbuka. Ikifanya jambo lazima mtafute lawama. Umeambiwa Sasa wanafanya utaratibu wao wafike tu Poland. Unakuja na Vyama. Wewe chama gani mkuu. Fanya tofauti.
Acha kujifanya msemaji wa serikali, walienda rasmi na serikali inalijua hilo.
 
Back
Top Bottom