Waziri Mwigulu: Mfumuko wa bei hausababishwi na Sera wala Uzembe. Fedha ya COVID 19 imeongeza mzunguko Vijijini na Deni la taifa ni himilivu

Waziri Mwigulu: Mfumuko wa bei hausababishwi na Sera wala Uzembe. Fedha ya COVID 19 imeongeza mzunguko Vijijini na Deni la taifa ni himilivu

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Waziri wa fedha Dr Mwigulu Nchemba amesema mfumuko wa bei unaolalamikiwa hausababishwi na sera zetu wala uzembe.

Kadhalika, fedha ya mkopo wa COVID 19 kutoka IMF imesaidia kuongeza mzunguko wa fedha mitaani na hasa katika maeneo yote ya vijijini ambako fedha hizi bado zinazunguka.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha amesema deni la taifa ni himilivu na mambo yanaenda kama yalivyopangwa.

===

Waziri wa Fedha na Mipango Mh. Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mfumuko wa bei na kupanda kwa gharama za maisha kwa wananchi hakusababishwi na tatizo la kisera wala uzembe bali unatokana na uwepo wa majanga yanayoendelea kuikumba dunia.

Dkt. Mwigulu ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na wahariri wa vyombo vya Habari akieleza utendaji na mafanikio ya serikali ya awamu ya sita katika kipindi cha mwaka mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan.


Chanzo: ITV habari
 
Fedha ya Covid si ilitumika kujengea madarasa? au kuna chenchi zilibaki ndio zikapelekwa kwenye huo mzunguko usioonekana?
 
Fedha ya Covid si ilitumika kujengea madarasa? au kuna chenchi zilibaki ndio zikapelekwa kwenye huo mzunguko usioonekana?
Simple logic: pesa za uviko zimeongeza fedha kwenye mzunguko.

Uwepo wa fedha kwenye mzunguko, umesababisha bidhaa kupanda.

Supply ya fedha imeongeza demand ya mahitaji, demand imeongeza bei.
 
Simple logic: pesa za uviko zimeongeza fedha kwenye mzunguko.

Uwepo wa fedha kwenye mzunguko, umesababisha bidhaa kupanda.

Supply ya fedha imeongeza demand ya mahitaji, demand imeongeza bei.
Ulaya na Marekani ambako kuna fedha nyingi na demand kubwa ya mahitaji hakuna mfumuko wa bei mkubwa kiasi hiki.
 
Nimeuliza leo nondo ya 16 mm ni 45,000 pcs 1.
Nyati cement 42.5 ni 15,000
Na viwanda vipo vingi tu.
Samia kazi unayo
 
Back
Top Bottom