Mocumentary
JF-Expert Member
- Jul 31, 2017
- 806
- 2,049
Swali na majibu.SWALI: Sababu za Serikali kutumia Wakala wa Huduma za Ununuzi Serikalini (GPSA) ambaye ananunua Magari kwa gharama kubwa kuliko bei ya Soko la Dunia.
JIBU: Serikali inatazamia kuanza kuwakopesha Watumishi wenye sifa ili kuondoa mzigo wa Mafuta na Matengenezo Serikalini.
[emoji16]
Nachomaanisha, wakopeshwaji watakopa magari ya Bei himilivu watakayomudu matengenezo hivyo gharama na matumizi yayapungua.Serikali gari haiuzwi kwa bei ya kununulia.
Inashuka vibaya mno na inaweza kununuliwa kwa bei ya nyanya
Land cruizer mkonga mpya bei gani?Ukisoma btn the lines.
V8 zitabaki Kwa Rais na Pm bas, wengine watarudi kwenye Land cruiser mkonga.
Na kinachosikitisha, wanachukua hatua hizo Leo, Si kwamba wanasikiza wananchi no, ni kwamba madeni yamewaelemea.
Ukilinganisha na wanayotumia sasa,Land cruizer mkonga mpya bei gani?
Salary 3-4M kabla ya makato italipa hiyo gari kwa muda gani?
Na mafuta na matengenezo mtupe PuaSerikali iliwahi kusema inatumia Bil.550 Kwa mwaka Kuagiza magari, vipuri, mafuta na matengenezo Kila mwaka.
--
Akijibu swali la Mbunge Asia Abdulkarim Halamga aliyehoji sababu za Serikali kutumia Wakala wa Huduma za Ununuzi Serikalini (GPSA) ambaye ananunua Magari kwa gharama kubwa kuliko bei ya Soko la Dunia, Waziri wa Fedha, Dkt, Mwigulu Nchemba amesema Serikali inatazamia kuanza kuwakopesha Watumishi wenye sifa ili kuondoa mzigo wa Mafuta na Matengenezo Serikalini.
Kuhusu utaratibu wa kuagiza Magari moja kwa moja Viwandani badala ya kutumia Mawakala, Dkt. Mwigulu amesema "Kuna baadhi ya mazingira yanaruhusu Serikali kununua kwa mawakala, pia, baadhi ya Viwanda havipendi wanunuzi waende moja kwa moja Viwandani".
Kwa mujibu wa taarifa iliyowasilishwa na Wizara ya Fedha Bungeni mwaka 2022, Serikali ilikuwa na Magari 15,742, Pikipiki 14,047 na Mitambo 373 huku ikitumia zaidi ya Tsh. Bilioni 500 kila mwaka kwaajili ya Ununuzi wa Magari mapya, Mafuta, Vipuri na Matengenezo.
My Take
Naona Kuna kigugumizi Cha kuchukua maamuzi.
Toka mwaka juzi mnaongelea hili jambo na hamfiki Muafaka.
Semeni kama Serikali kwamba deadline itakuwa lini? Na Je Madereva mtaajiri wa Umma au Kila boss na dereva wake?
Kumbe haujui janja yao!! Gari la milioni 300 anauziwa kwa mkopo mfanyakazi kwa sh milioni 30 tu!! Halafu anapewa malipo ya milage kila mwezi!!Sasa gari ya milioni mia tatu huyo DED au DC atamaliza lini kulilipa?? AU atakuwa kwenye ajira only kununua gari?
Kwahiyo CCM ni chongo na Akina Chadema ndio Vipofu?kwenye Nchi Ya Vipofu Wote, Chongo Akiongoza Ana Nafuu Sana
By Julius Kambarage Nyerere
Basi mkopo haukuhusu!Hakuna mtumishi wa wilayani mwenye uwezo wa kuhudumia harrier sembuse kruza?
Yaani kwenye mbio za mwenge niingize kruza langu kufukuzana kukagua njua ya mwenge.? Never
Umeandika nini hiki mzee mgaya?Magari ya Watumishi wa Serikali wanaostahili kukopeshwa Lazima yatakuwa na Bei ya chini kutokana na ukweli magari hayo yanauzwa na Serikali yenyewe
Pili, Magari hayo yatatumiwa na Watumishi kwenye Shughuli za kila siku za Serikali
Sidhani kama Magari hayo yana kodi
Hivyo usidhani V8 ya tsh 400mil na mkopo wake utasomeka hivyo, yawezekana kabisa ikawa chini ya tsh 50mil
Jumaa Mubarak 😀
Mzee mgaya anazeeka vibayanimerudia kusoma mara 2 ila bado sijaelewa, mwenye ambaye ameelewa anisaidie tafadhali