Waziri na Wizara ya Mambo ya Nje wanashindwa majukumu yao: tit fot tat na Kenya

Waziri na Wizara ya Mambo ya Nje wanashindwa majukumu yao: tit fot tat na Kenya

Mkuu Air Tanzania ina routes z Kenya?Tuanzie hapo.Kama hakuna wanajisemesha nini sasaa.Hawa kuwadharau Tz hatupeleki hata Mgambo,tunafanya Ujirani mwema na Alshabaab kwa wiki moja tu inatosha.Tz tushapigana sana saa hivi tunajenga Nchi.Uhuru wao Kenya wenyewe kuna Voice ya Tanzania.
Sasa mkuu ndege imeshindwa kuja bongo kisa hali ya hewa unataka wizara ya mambo ya nje ifanye nini? Kuna diplomasia ya kutuliza hali ya hewa? Au kenya kuzuia watanzania kufika kwao kisa corona ni swala la kiafya hilo na wako sahihi tu, ili tusiambukizane corona yafaa kila mtu abakie nchini kwao. Sasa kuna diplomasia gani hapo inahitajika katika corona na muingiliano wa watu?

Ndege kuzuiwa kufika ni swala la wizara ya uchukuzi hilo. Na hiyo ni hatua kulingana na janga hili la corona. Kenya ipo corona sana sasa waje huku watuletee corona? Au watoke na corona huku? Na pia kwa nini imekataza vibali vya ndege zetu kutua kwao wakati zao zinakuja kwetu? Hili mamlaka za usafiri wa anga wamalizane wenyewe.
 
Hilo swala lingekua handled timely na Membe enzi zake
 
Jidu La Mabambasi,

Hiyo ndege iliyokuja na ujumbe ipokuja na na kurudia angani haikuwa na nia ya kutua Tanzania bali walitaka kuonyesha tu kuwa walijaribu kuja kwenye mazishi. Haya mengine ni sheria ya reciprocity ndiyo itakayofuata, Ningekuwa Magufuli labda ningeweka ngumu sana kwa Uhuru.

Uganda na Rwanda nazo nadhani ziko njia ileile ila Uhuru ndiye aliyekuwa vocal sana. Nakubaliana naye kuwa nchi zetu zina korona, na ni lazima tushirikiane kuiondoa, lakini sikubaliani naye kwenye approach za kutumia lugha za kejeli na matendo ya kudanganya watu wazima.
 
Mkuu Air Tanzania ina routes z Kenya?Tuanzie hapo.Kama hakuna wanajisemesha nini sasaa.Hawa kuwadharau Tz hatupeleki hata Mgambo,tunafanya Ujirani mwema na Alshabaab kwa wiki moja tu inatosha.Tz tushapigana sana saa hivi tunajenga Nchi.Uhuru wao Kenya wenyewe kuna Voice ya Tanzania.
Precision Air ina route za Nairobi na Mombasa na ni WaTZ
 
Jidu La Mabambasi,

Retaliation ni kitu kizuri lakini kudharau(Ignoring) ni kitu kizuri zaidi.

Actually tunawapenda Wakenya si kwa sababu ni watu wazuri sana hapana:

-Ni kwa sb ni majirani tunaowategemeza chakula-Ni soko la lazima kwetu. Tukilikosa je, substitution yake ni ya faida zaidi au hasara?

-Hiki ni kichochoro cha mabeberu kwa sb wanaambatana nao sn-hapa kuna au kupiga mke kiukweli au mmoja kupiga kupiga mke huku mwingine akipiga ngozi.

Picha kubwa-Ndoa iliyodumu ni ile ya mume kuweka maji mdomoni!

German inayo Diplomasia ya kuigwa na Dunia, ebu tuibe hapo kitu!

Actually tungewaacha wakatua kwetu lakini tukahangaika na Malori tena tungeacha hata wiki Tatu nne hivi wajisahau halafu tunawafinya kwenye nyama laini!

Jicho la Tatu.
 
Mkuu Kenya tupende tusipende hatuwezi kuikwepa kibiashara.
Kenha ndio nchi ya pili kwa ukubwa wa biashara na Tanzania.
Hivyo tuyalee mahusiano hayo.
Hii ndio naisikia leo! Nina hakika utakuwa unadanganya.

Mkuu 'Jidu La Mabambasi', unao ushahidi wa kuonyesha kwamba "Kenya ndio nchi ya pili kwa ukubwa wa biashara na Tanzania"?

Kenya wakiuza sana hapa kwetu sio zaidi ya $600 milioni kwa mwaka. Biskuti, Icecream, maziwa, na mara moja moja mali za viwandani kama madawa havijawahi kupandisha biashara kuwa kubwa sana toka kwao. Sisi hatununui maua, mbogamboga toka huko.

Sisi hata hiyo $300 milioni haijawahi tokea. Mahindi yetu, vitunguu, maharage - hatuuzi dhahabu huko, na wala hatupati watalii wengi tokea pande hizo.

Sasa sijui ukubwa upi wa uchumi kati ya hizi nchi mbili unaouzungumzia!
 
Kunatafutwa njia ya kutuharibia uchaguzi wetu tu bure.

Mambo haya yakiendelea hivi, Magufuli atafaidika sana na mtafaruku huu.
 
Kiufupi mgogoro wa kiuchumi kati ya Kenya na Tanzania ni wa muda mrefu sana japo wamekuwa wakijitahidi kuufukia ila unaibuka tena, kibaya zaidi Wakenya wanahofu sana juu ya Tanzania kuwavuta nyuma ki uchumi na Tanzania kuwa mbele ya Kenya na hapa ndipo ukweli umelala. Yote tisa la kumi wahakikishe hii migogoro inafutika, kwani sote kuna kiasi tunategemeana.
 
Hao tusiwaendekeze.twende nao hivi hivi.

Sasa mtu unamkataza asiingie kwa ndege wakati mipakani mtu anaweza kupita hata kwa MIGUU. Kwahyo ndege zisiende kenya ila magari ruksa sasa umekataza nini?

Ni ujinga wa Kenya

Sent from my SM-G928F using JamiiForums mobile app
 
Tuikwepe tusiikwepe haitusaidii kitu WATULIZE AKILI WAACHE MAWENGE.

Hauwezi ukazuia ndege zisiingie kenya wakati hapo kenya Watanzania hata kwa miguu wana ingia.

Kama ni corona kati yao na sisi wapi kuna corona?
Mkuu Kenya tupende tusipende hatuwezi kuikwepa kibiashara.

Kenha ndio nchi ya pili kwa ukubwa wa biashara na Tanzania.

Hivyo tuyalee mahusiano hayo.

Sent from my SM-G928F using JamiiForums mobile app
 
Yanayoendelea katika mahusiano kati ya Kenya na Tanzania kwa sasa hivi hanasikitisha.
Kenya nijirani yetu na jirani ni ndugu.

Hivyo basi matukio matatu ya haraka haraka yaliyotokea yanatushangaza.
Kwanza ndege ya ujumbe wa Kenya ili rudi au kurudishwa Nairobi hivi majuzi.
Ndege hii ilikuwa na ujumbe wa viongozi waliokuwa wanakuja kuaga na kuhani msiba wa mzee Mkapa.
Pili kenya iliondoa ukaribisho kwa Watanzania, kati ya nchi nyingi, kwenda Kenya ati kutokana na janga la Korona.
Tatu leo Tanzania kwa kulipiza kisasi imeondoa ruksa ya ndege za Kenya, KA kutua Tanzania toka tarehe 1 Agosti, yaani kesho.

Sasa hapa napata wasi wasi juu ya ukaribu na mfululizo wa matukio haya.

Je hakuna hotline kati ya wizara za Nje kati ya Kenya na Tanzania?
Kweli watu wanafanya kazi zao kwa weledi hadi mambo yatokee hadharani na kuzivunjia heshima nchi zote mbili?

Mimi nayachukulia maswala haya kama failure in Diplomacy, na watu inabidi wawajibishwe.
Soon utasikia Kabudi akisema na kusifia kuwa jambo lililotendeka ni jambo la kishujaa huku mate mate yakimtoka
 
Back
Top Bottom