Waziri Nape ashangaa masuala ya mifumo nchini kutosomana

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648
Waziri Nape ameyasema hayo katika Kongamano la Jukwaa la Fikra kuhusu mabadiliko ya digitali leo tar 20 jijini Dar, akisema kuwa inauma kusikia mifumo ya Tanzania bado haiwezi kusomana.

Ametolea mfano kipindi alipoenda Hospitali ya Benjamin Mkapa na kufanya kipimo cha MRI ya mguu wake halafu alivyoenda Muhimbili MOI hawakuweza kupata taarifa hiyo na kumwambia afanye kipimo tena.

Kama waziri anashangazwa na kuumia, sisi wengine tufanye nini?
 
Aaah ndo wale madalali ya mifumo ya wahindi wameanza kampeni mdogo mdogo
 
Anashangaa nini wakati mifumo yenyewe ya kupewa kutoka nje? Aingie mitamboni aisomanishe mwenyewe
 
Yatakiwa hospital zote za serikali ziwe na mfumo mmoja ila hospital nyingine haiwezi ona hadi iombe hospital husika.
NHIF yatakiwa mfumo wake upokee matibabu yote hivyo mtu akienda hospital nyingine mfumo umkatae kuwa keshatibiwa hospital fulani
 
Yeye hashangai alivyotembea juu ya wanawake kule Lindi?!
 
Daktari A kutumia vipimo vya Daktari B tena hospital tofauti huwa ngumu kweli kweli.
 
Huyu mbwa atazeeka vibaya sana uzee wake.
 
Suluhisho la hili ni kutafuta MWEKEZAJI !!!!
Tukisema tutafute mwekezaji kwenye kila kitu ili kupata ubora, tutajikuta hata vibanda vyetu vya samaki tunatafuta mwekezaji.
 
Ulishawahi kumuelewa Nape?

Aendelee kukanyaga migongo ya wamama huko Mtama, ataisoma 2025
 
Kama hadi waziri anashangaa sisis wananchi ndio tumeduwaa kabisa hatuelewi
 
Wapewe Akina Habib kitengo uone kama mifumo haitasomana
 
Ujinga wake

Kwann hakuchukua vile vipimo kutoka BM national hospitol
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…