The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Deogratius Ndejembi, ameipa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni siku mbili kuvunja ukuta wa kiwanja namba P18618, eneo la Kigogo, baada ya mmiliki wake kushindwa kuwasilisha nyaraka za uhalali wa umiliki.
Akizungumza na wananchi leo, Februari 15, 2025, Mhe. Ndejembi amesema kampuni ya Nizar Food ilipewa muda kuwasilisha nyaraka hizo tangu Januari 21 mwaka huu lakini imeshindwa kufanya hivyo.
Uchunguzi wa Kamishna wa Ardhi ulibaini kuwa viwanja hivyo viliongezwa kinyemela, hivyo ameagiza ukuta huo ubomolewe mara moja.
Akizungumza na wananchi leo, Februari 15, 2025, Mhe. Ndejembi amesema kampuni ya Nizar Food ilipewa muda kuwasilisha nyaraka hizo tangu Januari 21 mwaka huu lakini imeshindwa kufanya hivyo.
Uchunguzi wa Kamishna wa Ardhi ulibaini kuwa viwanja hivyo viliongezwa kinyemela, hivyo ameagiza ukuta huo ubomolewe mara moja.