Waziri Prof. Kabudi aufuta Uongozi wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBRC) kutokana na tuhuma mbalimbali

Waziri Prof. Kabudi aufuta Uongozi wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBRC) kutokana na tuhuma mbalimbali

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Screenshot 2025-03-06 145430.jpg
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi ameufuta Uongozi wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBRC) baada ya uchunguzi wa tuhuma mbalimbali zilizowasilishwa na wadau wa mchezo wa ngumi.

Taarifa kutoka Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imeeleza kuwa, mnamo tarehe 8, Mei 2024, Waziri aliunda Kamati Maalum ya uchunguzi yenye jukumu la kuchunguza malalamiko hayo na kubaini ukweli wake.

Baada ya kamati kukamilisha uchunguzi iliwasilisha taarifa ya yaliyobainika kulingana na tuhuma zilizowasilishwa. Kamati ilijidhihirisha pasi na shaka kuwa uongozi ulikuwa na mapungufu ya kiutendaji.

Mapungufu yaliyobainika ni matumizi mabaya ya madaraka kinyume na Sheria za nchi, Katiba ya Kamisheni ya ngumi za kulipwa Tanzania ya mwaka 2018 pamoja na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora na usimamizi wa rasilimali za kamisheni.

Matumizi mabaya ya fedha kinyume na Sheria za nchi, Katiba ya Kamisheni ya Ngumi za kulipwa Tanzania 2018 pamoja na kanuni za uwajibikaji na usimamizi wa rasilimali za kamisheni.

Kufuatia mapungufu hayo, Mheshimiwa Waziri ameelekeza hatua zaidi za kisheria zichukuliwe dhidi ya viongozi walioondolewa madarakani, ili kuweka fundisho kwa viongozi wengine wa vyama na mashirikisho na michezo nchini.

============================

Awali walivyosimamishwa
WhatsApp Image 2025-03-06 at 15.08.32_384890cb.jpg
 

Attachments

Bado hamjamuelewa Mwakinyo?
Bado mnasema anaringa? Bado mnasema ana maneno ya shombo?
 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi ameufuta Uongozi wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBRC) baada ya uchunguzi wa tuhuma mbalimbali zilizowasilishwa na wadau wa mchezo wa ngumi.

Taarifa kutoka Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imeeleza kuwa, mnamo tarehe 8, Mei 2024, Waziri aliunda Kamati Maalum ya uchunguzi yenye jukumu la kuchunguza malalamiko hayo na kubaini ukweli wake.

Baada ya kamati kukamilisha uchunguzi iliwasilisha taarifa ya yaliyobainika kulingana na tuhuma zilizowasilishwa. Kamati ilijidhihirisha pasi na shaka kuwa uongozi ulikuwa na mapungufu ya kiutendaji.

Mapungufu yaliyobainika ni matumizi mabaya ya madaraka kinyume na Sheria za nchi, Katiba ya Kamisheni ya ngumi za kulipwa Tanzania ya mwaka 2018 pamoja na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora na usimamizi wa rasilimali za kamisheni.

Matumizi mabaya ya fedha kinyume na Sheria za nchi, Katiba ya Kamisheni ya Ngumi za kulipwa Tanzania 2018 pamoja na kanuni za uwajibikaji na usimamizi wa rasilimali za kamisheni.

Kufuatia mapungufu hayo, Mheshimiwa Waziri ameelekeza hatua zaidi za kisheria zichukuliwe dhidi ya viongozi walioondolewa madarakani, ili kuweka fundisho kwa viongozi wengine wa vyama na mashirikisho na michezo nchini.

Chanzo: Mwanaspoti
Bado Tume / Kamisheni Olimpic.....yule Rais na Katibu wake hawafaiiii.....wameiba sanaaa
 
Back
Top Bottom