Waziri Simbachawene acha kuingiza raia kwenye ulinzi. Polisi wako wanafanya nini?

Waziri Simbachawene acha kuingiza raia kwenye ulinzi. Polisi wako wanafanya nini?

Badala ya kutumia wananchi ambao nao wanakabiliwa na majukumu mengine asubuhi watajikuta wanasinzia maofisini au kwenye vibarua vyao.

Jukumu la ulinzi ni la Polis, Si la raia.Hata Mwendazake alipiga vita walinzi shirikishi.Walijigeuza kuwa vikundi vya uhalifu vya kunyanyasa raia na kupokea rushwa.

Serikali ijipange,,Polisi mchana wawe wachache usiku wamwagwe wenge mitaani.

Polis iachane na kulinda mabenki au taasisi mbali mbali na badala yakezilindwe na suma jkt.

hao askari wasambazwe mitaani badala ya kulinda taasisi.

Ikiwa hawatoshi kuna migambo hawana kazi. Wachukuliwe hao wapelekwe nchi nzima.
 
kuna advantage kiasi flani ya kutumia ulinzi shirikishi..
kwanza hawa jamaa wanawajua wezi wa mtaani so inakua rahisi kuwadhibiti..
pili inasolve swala la ajira kwa kiasi chake

nadhani swala la malipo ndo inabidi lifanyiwe kazi kuwe na kiwango sawa cha malipo kwa kaya zote na mahala popote nchini.

Sent from my SM-G570F using JamiiForums mobile app
ULINZI SHIRIKISHI SIO CHANZO CHA AJIRA.
 
Mi mwenyewe mtaani nipo kwenye kikundi Cha ulinzi shirikishi na kwakua hatuna posho usiku tukikukamata tunakusachi tunakunyang'anya kila kitu tumekua vibaka wenye vibali
 
Mi mwenyewe mtaani nipo kwenye kikundi Cha ulinzi shirikishi na kwakua hatuna posho usiku tukikukamata tunakusachi tunakunyang'anya kila kitu tumekua vibaka wenye vibali
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
nalipwa mshahara laki 2 kodiya pango elfu 80 ushuru wa taka elfu 10 ulinzi shirikishi elfu 10 malipo ya maji elfu 10 umeme elfu 20. kweli nitaishi na elfu 70 chakula na matumizi yangu madogomadogo bado tozo miamala na vocha bado usafiri wa dalala. serikali iache kuomba wananchi michango. nchi nyingi ulimwenguni takataka juu ya serikali ulinzi juu ya serikali umeme bei chini majibbei chini
Kuliko kuja hapa jukwaani na kutoa ushauri kwa lugha ya kejeli dhidi ya Waziri ni vema mkae kama jamii mpeane rate ambayo kila mtu ataimudu.

Watanzania tubadilike tuache mambo ya kihuni huni, mtu anakuwa na idea nzuri lakini lugha anayoandika hata Waziri akiiona ataona ni upuuzi tu.
 
Badala ya kutumia wananchi ambao nao wanakabiliwa na majukumu mengine asubuhi watajikuta wanasinzia maofisini au kwenye vibarua vyao.

Jukumu la ulinzi ni la Polis, Si la raia.Hata Mwendazake alipiga vita walinzi shirikishi.Walijigeuza kuwa vikundi vya uhalifu vya kunyanyasa raia na kupokea rushwa.

Serikali ijipange,,Polisi mchana wawe wachache usiku wamwagwe wenge mitaani.

Polis iachane na kulinda mabenki au taasisi mbali mbali na badala yakezilindwe na suma jkt.

hao askari wasambazwe mitaani badala ya kulinda taasisi.

Ikiwa hawatoshi kuna migambo hawana kazi. Wachukuliwe hao wapelekwe nchi nzima.
Polisi waache kulinda bank walinde suma jkt?!! Hiv mkuu unajiskiliza unavyoongea lakin? Hawa suma wanaotumia pump action kulinda ndo uwakabidhi bank? Mtu akienda hata na bastola yenye risas 10 anavamia bank na anapiga tukio na kusepa
 
Polisi waache kulinda bank walinde suma jkt?!! Hiv mkuu unajiskiliza unavyoongea lakin? Hawa suma wanaotumia pump action kulinda ndo uwakabidhi bank? Mtu akienda hata na bastola yenye risas 10 anavamia bank na anapiga tukio na kusepa
Suma jkt wamepitia mafunzo yote ya kijeshi

Wanauwezo wa kutumia silaha za kila aina

Hao mafunzo yao ni zaidi ya polisi

Hao mafunzo yao ni sawa na jwtz.
 
Hivi sasa kuna migogoro kila mahala juu ya kuwepo kwa ulinzi shirikishi. Mfano mtaani kwangu mwenyekiti wa mtaa ambaye ni wa CCM kawa mwizi kabisa maana analazimisha kila mkazi wa kitongoji mwenye nyumba alipe Tshs.10,000 kwa mwezi suala ambalo analibeba kama vile ni kesi.

Sasa hivi anatishia kupeleka watu polisi nikiwemo mimi. Tshs.10,000 kwa mwezi ni nyingi sana. Halafu hana walinzi wawili tu. Huyu mzee ni mwizi. Kama kilivyochama chake. Nimefanya utafiti sehemu nyingi wanalipa Tshs.3000.

Leo nimemsikia Waziri wa Mapolisi George Simbachawene akitoa maelekezo juu ya kuimarisha ulinzi kupitia ulinzi shirikishi. Waziri ajiulize mbona kipindi cha kudhibiti Wapinzani aombi ulinzi shirikishi?

Tanzania ina jeshi kubwa sana la polisi ambalo linafanya kazi kijinga mno. Hawa maarufu Tigo wapo busy na bodaboda mchana usiku wamelala sasa nchi ngani inaogopa kulinda Wananchi wake Usiku?

Hii nchi ina mambo ya hovyo sana. Waziri mjipange hata kuimarisha doria usiku, ili suala la ulinzi na kuanza mtaa uajiri Walinzi ni kuleta sokomoko mitaani.

Toeni ama zungumzeni na TAMISEMI waweke walinzi hata hawa SUMA JKT kila ofisi za serikali za mitaa italeta tija kuliko kuliacha kwa kila mjumbe ajipangei malipo yake. Na hili linawapata watu kugomea mambo ya ulinzi kutokana na kuchezea CHAGUZI zetu.
Ulinzi shirikishi ni jukumu letu sote

tulilinda enzi za Nyerere, Mwinyi na mkapa

vijana mmekua mlenda sana
 
Suma jkt wamepitia mafunzo yote ya kijeshi

Wanauwezo wa kutumia silaha za kila aina

Hao mafunzo yao ni zaidi ya polisi

Hao mafunzo yao ni sawa na jwtz.
Suma jkt hana mafunzo yoyote ya kumzidi polisi jkt kule ni kilimo na kulindia virungu na kuchezea SR tu alaf ile ni kampuni ya ulinz tu iliyo chin ya jkt huwez kumpa SMG mtu wa kwenye kampuni ya ulinzi
 
Bila police Jamii police hawezi Kazi.Police Jamii ndie anaewajua vibaka na wezi wote mitaani,ukiibiwa tafuta police jamii mpe hela mwizi akipatikana atakurejeshea gharama.
Kuibiwa ni faida niliibiwa tv na radio vyote jumla milioni 1.Nilimpata mwizi wangu na mnunuzi nikamwambia chagua miaka 30 jela robbery au unipe pesa hapa unapanga kiwango utakacho kama ni milioni 10 au zaidi unaangalia ulichoibiwa kimezaa mara ngapi.
 
Hivi ukilipa ikatokea ukaibiwa Huyo Mwenyekiti analipa au inakuaje?
Wanakwambiya wana uhakika gani kama ni kwl ulikuwa na vitu hivyo unavyodai vimeibiwa?

Na havipo sasa,,

Watathibitishaje kama ulikuwa navyo na kwl vimeibiwa usiku huo.?
 
Nijuavyo mm walinzi shirikishi ni sehemu ya askari.

Hivyo wanapaswa kulipwa na serikali sio RAIA.

Tanzania kuna mambo ya hovyo sana.
Kila siku kuwatwisha wanainchi mzigo wa maisha magumu
Tanzania hiyo ambayo walinzi shirikishi ni sehemu ya askari hivyo walipwe na serikali?!!!hakuna kitu kama hicho, askari wao ni kama waratibu tu, lakini ulinzi ni wa jamii husika ya mtaa, mkisema kila kitu mtegemee polisi mufwaaa!!!
 
Tanzania hiyo ambayo walinzi shirikishi ni sehemu ya askari hivyo walipwe na serikali?!!!hakuna kitu kama hicho, askari wao ni kama waratibu tu, lakini ulinzi ni wa jamii husika ya mtaa, mkisema kila kitu mtegemee polisi mufwaaa!!!
Kuna wale Mgambo au walinzi shirikishi vituo vya police wanalipwa na nani?

Waache kuzidi kutupa mzigo wanainchi..
 
Back
Top Bottom