Waziri Simbachawene maini unayokula si anayokula Mtanzania maskini

Waziri Simbachawene maini unayokula si anayokula Mtanzania maskini

Tengeneza Njia

Senior Member
Joined
Jul 29, 2022
Posts
121
Reaction score
205
Umetetea sana hoja ya tozo kuonyesha kuwa maisha yamebadilika bla bla bla!

Maini mnakula nyinyi tena ya gharama sana - maini hapa yanawakilisha tu mambo mengi ya anasa ambayo viongozi wetu mnapata na huku mtanzania maskini kabisa tena yule wa kijijini huko bado mnanyonya bila hata huruma. Maslai yenu mbele!

Mngekuja hapo na hoja na ma-report yanayoonyesha Serikali mnafanya nini kupunguza matumizi yasiyo na tija, sio ripoti za kina bashungwa na ndalichako za kutimiza wajibu.

Mngekaa hapo mkatuambia sababu gani mmechagua kufanya miradi mingi ambayo mmetuonesha na pesa za miradi hiyo hazipo mpaka mmefikia huku kwenye kodi? yale masifa sifa mengi na kongore kwa mama na maneno kuwaambia wananchi sisi watanzania ni matajiri na tupo uchumi wa kati huku leo mmekiri hali ni ngumu na swali la mhandishi aliyegusia jambo hili. Mh. Mwigulu amejing'ata ng'ata tu na kuja na mifano yake isiyo na kichwa wala miguu ya vipapatio vya kuku na kwao kuzaliwa 11.

Dah, inasikitisha!
 
Mimi nimemuelewa Sana mzee Simbachawene sema tuu hajaweka wazi Ni wapi tutapata mbadala wa kupunguza hizi too[emoji848]
 
Umetetea sana hoja ya tozo kuonyesha kuwa maisha yamebadilika bla bla bla!

Maini mnakula nyinyi tena ya gharama sana - maini hapa yanawakilisha tu mambo mengi ya anasa ambayo viongozi wetu mnapata na huku mtanzania maskini kabisa tena yule wa kijijini huko bado mnanyonya bila hata huruma. Maslai yenu mbele!

Mngekuja hapo na hoja na ma-report yanayoonyesha Serikali mnafanya nini kupunguza matumizi yasiyo na tija, sio ripoti za kina bashungwa na ndalichako za kutimiza wajibu.

Mngekaa hapo mkatuambia sababu gani mmechagua kufanya miradi mingi ambayo mmetuonesha na pesa za miradi hiyo hazipo mpaka mmefikia huku kwenye kodi? yale masifa sifa mengi na kongore kwa mama na maneno kuwaambia wananchi sisi watanzania ni matajiri na tupo uchumi wa kati huku leo mmekiri hali ni ngumu na swali la mhandishi aliyegusia jambo hili. Mh. Mwigulu amejing'ata ng'ata tu na kuja na mifano yake isiyo na kichwa wala miguu ya vipapatio vya kuku na kwao kuzaliwa 11.

Dah, inasikitisha!

Kuna na haya mambo yao:

IMG_20220901_085859_867.jpg


Bila kusahau mishahara na marupurupu yao ambayo kwa hakika si kingine bali kufuru.
 
Back
Top Bottom