Pre GE2025 Waziri Slaa awataka wananchi kushiriki ujenzi wa mnara

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa, amewahamasisha wananchi wa Kijiji cha Idete, Kata ya Chanzuru, mkoani Morogoro, kuchangia nguvu kazi katika ujenzi wa mnara wa mawasiliano ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za mawasiliano, hasa vijijini.

Pia soma Pre GE2025 Miradi kuelekea Uchaguzi Mkuu: Mhandisi Kundo akagua mradi wa maji unaonufaisha zaidi ya wakazi 200,000 Chalinze

Waziri Silaa ameungana na wananchi hao kukagua utekelezaji wa ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano katika kijiji hicho, ikiwa ni sehemu ya juhudi za serikali kuboresha huduma za mawasiliano nchini.
 
Kuna kijiji kimoja kinaitwa Sanjaranda huko Itigi mkoani Singida nimekuta mnara wa Tigo(yas) unajengwa na mfuko wa mawasilano. Kijiji hicho na vijiji jirani kupata masafa ya redio hasa TBC na nyingine hazisikiki wananchi wanaishi hata hawajui nchi yao inaendaje. Pamoja na mawasiliano ya simu ni bora pia wakafunga mitambo ya kunasa masafa ya redio hapohapo mnarani na makampuni mengine ya simu nao wajenge minara yao hapo. Kuna maeneo mengi ya katikati ya nchi bado hayana mawasiliano ya simu na haya ya fm kwa redio. kupiga simu hadi uende kijiji cha mbali ukapande kichuguu au mti ndio upige simu, hiki ni kituko miaka hii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…