Waziri Tabia Mwita Amshukuru Dkt. Mwinyi kwa Kombe la CECAFA U15 Kutua Zanzibar

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

WAZIRI TABIA MWITA AMSHUKURU DKT. MWINYI KWA KOMBE LA CECAFA U15 KUTUA ZANZIBAR

Mabingwa wa CECAFA U15, Karume Boys wametua nyumbani Zanzibar wakitokea nchini Uganda na ubingwa wao walioupata kwenye michuano ya CECAFA U15 Boys Championship.

Karume Boys wamepokelewa na Makamu wa Pili wa Rais, Mhe. Hemed Suleiman, Waziri wa Michezo, Mhe. Tabia Mwita, Mkuu wa Mkoa, Mhe Idrisa, viongozi mbalimbali, Wazazi na wadau wa soka visiwani Zanzibar.

Makamu wa Pili wa Rais, Mhe Hemed Suleiman, Waziri wa Michezo, Mhe Tabia Mwita, Mkuu wa Mkoa, Mhe. Idrisa wamepata bahati ya kuwa viongozi wa kwanza kubeba kikombe cha ubingwa wa CECAFA U15 kilicholetwa na vijana wa Karume Boys.

Karume Boys wameletwa na Ndege maalum iliyotolewa na Mhe. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi ambayo imewafikisha vijana wa Karume Boys nchini wakitokea Entebbe, Uganda.
 

Attachments

  • F_JZBGPWIAAr7tw.jpg
    126.2 KB · Views: 7
  • F_JaNeVWQAAvksn.jpg
    183.2 KB · Views: 7
  • F_JaOSwWsAAgiOn.jpg
    157.2 KB · Views: 5
  • F_JaN37XAAAok60.jpg
    144.8 KB · Views: 6
  • F_JaOuHWcAALm2g.jpg
    172.4 KB · Views: 7
  • F_JcpXRXEAA11WQ.jpg
    147.1 KB · Views: 7
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…