Waziri Ummy: Kigezo kikubwa ambacho tutakitumia kuajiri walimu ni wale wanaojitolea. Alalamikia barua feki

Waziri Ummy: Kigezo kikubwa ambacho tutakitumia kuajiri walimu ni wale wanaojitolea. Alalamikia barua feki

wewe ndiye huelewi- duniani kuna internship
internship



noun

the position of a student or trainee who works in an organization, sometimes without pay, in order to gain work experience or satisfy requirements for a qualification.

"they encouraged students to apply for newspaper internships"
mkuu internship inaenda sanjari na allowances kama busfare, meals and accomodation na ipo kisheria kwa taaluma kama utabibu, unesi, maabara na mafamasia kwa ngazi ya shahada hapa nchini. Vipi hawa walimu mliwatangazia lini wajitolee na ajira zao zinatolewa kwa mfumo huo tangu lini? nani alikuwa anawalipa pesa za kujikimu? na vipi kuhusu taasisi za uma zilizokataa kupokea vijana wa kujitolea?
 
Tatizo ni kubwa kuliko hata ajira zenyewe, boresheni sekta binafsi wau wajiajiri
Kila mmoja anataka aaijiriwe serikalini. Hao walioomba serikalini asilimia kubwa wana ajira tayari shule binafsi na wanalipwa vizuri lakini hawazithami.
 
Hii habari ya Wanaojitolea nayo ni kichaka kingine. Wanaojitolea wenyewe wamepewa nafasi hizo za kujitokea kwa kujuana, then hao hao ndio watakaopewa kipaumbele kwenye kuajiriwa! Hawa masikini wenye hali tete na walioshindwa kujitolea kwa sababu ya kukosa namna ya kujikimu wawapo majitoleoni, itakuaje kwa upande wao?

TAMISEMI wawe fair katika hili. Watumie vigezo vinavyokubalika kwa mujibu wa sheria.
 
wewe ndiye huelewi- duniani kuna internship
internship



noun

the position of a student or trainee who works in an organization, sometimes without pay, in order to gain work experience or satisfy requirements for a qualification.

"they encouraged students to apply for newspaper internships"
Wewe unadhani ni asilimia ngapi ya wahitimu wanamudu hali ya kujikimu wenyewe pindi wawapo majitoleoni?
 
Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu amesema yapo malalamiko kuwa baadhi ya Walimu wanaojitolea wanawasilisha barua feki zinazosema wanafanya hivyo wakati hawajitolei.

Ametoa kauli hiyo leo Mei 25, 2021 Bungeni Dodoma wakati akimjibu Mbunge wa Longido Kiruswa aliyehoji ni kwanini Seikali isiajiri Walimu ambao wanajitolea. Amesema hata Wanaojitolea watafanyiwa uchambuzi ili kuona kama ni kweli wanafanya hivyo.

Amesema kigezo kikubwa kitakachotumika ni hicho akiongeza kuwa, suala hilo ni tete ambapo nafasi ni 6,949 ilihali mpaka Mei 23, 2021 walioomba ni 89,958. Ameomba Serikali iaminiwe akisisitiza Haki itatendeka.

========

Waziri wa TAMISEMI, Ummy Mwalimu akibu swali la mbunge Kiruswa lililouliza 'Kwanini wasiajiri walimu ambao wanajitolea?' kwenye ajira za ualimu zilizotangazwa karibuni, amesema kigezo kikubwa ambacho watakitumia katika kuangalia wenye vigezo ni wale ambao wanajitolea.

Waziri Ummy amesema kwa sasa ipo changamoto kwa wengine kuleta bara feki kwamba wanajitolea na suala hilo ni tete kwani nafasi zipo 6,949 lakini walioomba wameshafika 89,958 na kumuomba spika aiamini serikali itatenda haki.

Amesema pia upo mtazamo ndani ya wazira labda waajiri ambao wamemaliza muda mrefu lakini hawajaajiriwa akitolea mfano waliomaliza 2012 kwani muda wao wa kuajiriwa serikalini nao unapungua ambapo wanatakiwa kuajiriwa kabla ya kufikisha umri wa miaka 45.


Huu Ni unyanyasaji unatumiaje kujitolea kuwa kigezo Cha kumwajili mwalim? Sio sawa kabisa . Mtu ajitolee wakat hakuna nauli,hela ya malaz au fedha kwa ajili ya matumiz mengine,anawezaje? Ataishije? Hiki kigezo kinafaa kifutiliwe mbali kabsa
 
Vigezo vifuatavyo vitasaidia kuondoa malumbano ambavyo ni;

1. Waliokaa muda mrefu bila ajira mfano aliyemaliza 2015 apewe kwanza kabla ya alomaliza 2019 maana hata kukaa mtaani tu uzoefu.

2. Ufaulu wa GPA waweke benchmark ya 3.8
Mkuu GPA ya 3.8 ST JOSEPH ni sawa na 3.8 MZUMBE? Kwa wewe unavyodhania?
 
Wengi humu wanaangalia solution ya muda mfupi, wakati bado vyuo vinatema.

Hili tatizo limetengenezwa na hao Wizara ya elimu na TCU yao.

Mtu anaenda kusoma education kwasababu
1. Apate mkopo
2. Programme nyingine zimemtema ualimu ndio kapu la kubeba walioshindwa kwenda labda health programmes.

Lazima watu wajazane wawe wengi sanaa kwenye hiyo fani na wakose pakwenda.

Nashauri
1. TCU iweke vigezo vikali kwenye programmes za ualimu tupate walimu kweli, wenye kupenda ualimu na sio igeuke ni kimbilio la mwisho kwa wanaojiunga na elimu ya juu.
Hii iende sambamba na kuboresha maslahi ya walimu iwe taaluma inayoheshimika.
UKWELI MCHUNGU UKIONA KAZI YAKO WAFANYAKAZI MLIOPO NCHI NZIMA NI WENGI KUANZIA ELFU 20 BASI MSHAHARA WENU LAZIMA UWE MDOGO.
 
Wewe unadhani ni asilimia ngapi ya wahitimu wanamudu hali ya kujikimu wenyewe pindi wawapo majitoleoni?
Mkuu ukijitolea kijijini kwenu ulikozaliwa au kwenye shule ya mtaani kwenu unagharamika nini- mbona mkiitwa na Mbowe kwenye maandamano mnaenda na kudai hamulipwi kitu wala kusombwa kama wale wa CCM- unakera sana wewe na kijilizaliza kwako.
 
mkuu internship inaenda sanjari na allowances kama busfare, meals and accomodation na ipo kisheria kwa taaluma kama utabibu, unesi, maabara na mafamasia kwa ngazi ya shahada hapa nchini. Vipi hawa walimu mliwatangazia lini wajitolee na ajira zao zinatolewa kwa mfumo huo tangu lini? nani alikuwa anawalipa pesa za kujikimu? na vipi kuhusu taasisi za uma zilizokataa kupokea vijana wa kujitolea?
Mkuu ukishatangaziwa hiyo ni ajira sasa- kujitolea unajipeleka
 
Mkuu ukijitolea kijijini kwenu ulikozaliwa au kwenye shule ya mtaani kwenu unagharamika nini- mbona mkiitwa na Mbowe kwenye maandamano mnaenda na kudai hamulipwi kitu wala kusombwa kama wale wa CCM- unakera sana wewe na kijilizaliza kwako.
Huna akili
 
Sometimes kusoma sana au kutosoma hakudetermine GPA kubwa.

Huko "Private" vyuo vingi wanapeana miGPA mikubwa mikubwa tu wakati vyuo vingi serikalini wanafunzi wana kazi ya kuoneshana umwamba na ma-lecturerers.
Ooh yes!!!.Umeongea vyema kabisa.

Naona suala la GPA vyuoni ni changamoto sana hasa ukizingatia kuwa kuna baadhi ya vyuo hasa private universities GPA zinatolewa kama njugu.

Next time nitaleta hapa JF special uzi tu jinsi gani kuwe na uwiano wa utoaji wa hizi GPA vyuoni. Je should there be a regulatory body kusimamia hili la GPA, je mitihani ya universities zote isahihishwe na taasisi moja? ....n.k
 
Back
Top Bottom