Waziri Ummy kufanya mabadiliko kwa Watendaji wa Mamlaka za Serikali

Waziri Ummy kufanya mabadiliko kwa Watendaji wa Mamlaka za Serikali

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Ummy Mwalimu ameahidi kufanya mabadiliko makubwa kwa watendaji wa mamlaka za serikali za mitaa kutokana na kutoridhishwa na utendaji kazi wa baadhi ya watumishi na Wakuu wa Idara katika mamlaka hizo.

Waziri Ummy ametoa kauli hiyo jijini Dodoma wakati akifunga kikao kazi cha wakuu wa idara za utawala na rasilimali watu katika utumishi wa umma, ambapo amebainisha kuwa baadhi yao wamekuwa wakitengeneza madaraja kati yao na watumishi wanaowasimamia.

Aidha, Mhe. Ummy amesema ofisi yake inakusudia kufanya mabadiliko ya utaratibu wa watumishi na watendaji katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ikiwemo kuondoa mamlaka za nidhamu kutoka kwenye Baraza la Madiwani.

Chanzo: ITV
 
Ukaimu kaimu umezidi halmashauri

Pia watu wenye sifa wapo kibao hawapewi Ofisi waliopewa wanakaimu

Kila idara hata wakuu wa vitengo ni mwendo wa kukaimu tu

Sasa hapo ndio utajua local government is local
 
Hii ya madiwani kuwa mamlaka ya nidhamu ibaki tu. Sema kamati za uchunguzi isipangwe na waajiri maana anawapangia mpaka cha kuandika kwenye ripoti.
 
Hivi mwl alikuwa hajapandishwa daraja kwa miaka takribani 10, anapopandishwa kwa nini asivushwe lile alilokosa akapata sawa na wenzake, pia inakuwaje mel kaajiriwa 1999 akawa na daraja G na wa 1990 akawa F, hii inatokana na nini? Na hao wote wamejiendeleza kufikia degree
 
Ukaimu kaimu umezidi halmashauri
Pia watu wenye sifa wapo kibao hawapewi Ofisi waliopewa wanakaimu
Kila idara hata wakuu wa vitengo ni mwendo wa kukaimu tu
Sasa hapo ndio utajua local government is local
Weacha tu, hovyo kahisa! Afu kila mtu msimamizi
 
Hii ya madiwani kuwa mamlaka ya nidhamu ibaki tu. Sema kamati za uchunguzi isipangwe na waajiri maana anawapangia mpaka cha kuandika kwenye ripoti.
Wacha itoke mzee, unakuta diwani ni la saba anapewa laki tu kuwa mtumishi fulani ashuguulikiwe, aisee utashambuliwa kama nyuki, na unapewa adhabu isiyo na msingi.

Wacha yaondolewe
 
Ondoa wakuu wa idara wafuatao ili upate amani,wamekuwa miungu watu na ni walamba Rushwa wakubwa, DT geita TC, DT kahama manispaa, DT songwe, Afisautumishi Ilala, afisaelimu secondary Halmashauri ya Meru, Ilemela, Arusha Jiji, afisaelimu msingi Halmashauri za Korogwe, Moshi manispaa kule Kilimanjaro. Geita vijijini
 
Wacha itoke mzee, unakuta diwani ni la saba anapewa laki tu kuwa mtumishi fulani ashuguulikiwe, aisee utashambuliwa kama nyuki, na unapewa adhabu isiyo na msingi.

Wacha yaondolewe
Lakini mkuu, madiwani si wanajadili ripoti ya kamati ya uchunguzi ambayo inafanywa na wataalamu wenye elimu na vyeo kumzidi mtumishi mtuhumiwa? Mchawi wa kila kitu ni maoni ya ripoti ya kamati uchunguzi, na huko ndiko Mkurugenzi anakowapanga hao wana kamati ili waandike ripoti ya atakavyo yeye kwa kuwa kamati yenyewe anaiunda huyohuyo Mkurugenzi..sasa hii ndio inapaswa kubadilishwa, Kamati iwe Huru ikiwezekana iwe fixed kabisa kwa mwaka au miaka miwili, wajumbe wajulikane na sio kuteua kila tuhuma zinapoibuliwa
 
Ondoa wakuu wa idara wafuatao ili upate amani,wamekuwa miungu watu na ni walamba Rushwa wakubwa, DT geita TC, DT kahama manispaa, DT songwe, Afisautumishi Ilala, afisaelimu secondary Halmashauri ya Meru, Ilemela, Arusha Jiji, afisaelimu msingi Halmashauri za Korogwe, Moshi manispaa kule Kilimanjaro. Geita vijijini
DT kahama ndio nini mkuu?
 
Ondoa wakuu wa idara wafuatao ili upate amani,wamekuwa miungu watu na ni walamba Rushwa wakubwa, DT geita TC, DT kahama manispaa, DT songwe, Afisautumishi Ilala, afisaelimu secondary Halmashauri ya Meru, Ilemela, Arusha Jiji, afisaelimu msingi Halmashauri za Korogwe, Moshi manispaa kule Kilimanjaro. Geita vijijini
huu ushauri unatoa kwenye serikali ipi, we si kutwa unainanga serikali ya Sasa kuwa ni rubbish
 
huu ushauri unatoa kwenye serikali ipi, we si kutwa unainanga serikali ya Sasa kuwa ni rubbish

E0NhMwdXIAAW0HL (1).jpeg
 
Hawabadilishi Sheria za recategorization zinazosumbua kila kukicha.

Mh. Ummy Mwalimu hapa wasomi tunahitaji neno la matumaini kutoka kwako
 
Ukaimu kaimu umezidi halmashauri

Pia watu wenye sifa wapo kibao hawapewi Ofisi waliopewa wanakaimu

Kila idara hata wakuu wa vitengo ni mwendo wa kukaimu tu

Sasa hapo ndio utajua local government is local
Wana roho mbaya sana aiseh.. Utadhani wanakaa milele kwenye hizo nafasi. Afu sasa madiwani nao, nishawahi shuhudia kuna mtumishi mmoja alikuwa afisa mtendaji wa kata. Daah kisa tu kuna upigaji diwani alikuwa anafanya, sasa diwani akawa anaharibu na wawkuwajibishwa ni jamaa ambae ni mtendaji kata.. Jamaa akaona sio kweli maana kamwambia sana atumie akili haelewi, kalipiga pini... Diwani ndo chuki ikaanza hapo, mpaka kwenye balaza lao wakamshinikiza mkurugenzi.. Mkurugenzi akaona amuhamishe wahuni wadiwani kwa chuki zao bado hawakuridhika jamaa katolewa kazini ndo wakafurahi.. Jamaa akaendelea na life mtaani badae akaona sio kweli, huu ni uonevu kila akikataa rufaa kwenye mabalaza ya watumishi anashindwa .. Akaamua kuandika barua ikulu.. Ndo barua ikaelekezwa kwa katibu mkuu utumishi ikashuka wizarani mpaka halmashauri aliyopo ndo akarudi kazini.. Ila akashuka tena akawa mtendaji ngazi ya mtaa.. Kwahiyo mh Ummy mwalimu ameona kuna uonevu na nibora waondolewe kuwa mamlaka ya nidhamu...
 
Hii ya madiwani kuwa mamlaka ya nidhamu ibaki tu. Sema kamati za uchunguzi isipangwe na waajiri maana anawapangia mpaka cha kuandika kwenye ripoti.
Wewe itakuwa diwani kama sio basi ndugu yako, kama sio ndugu yako basi jamaa yako, haiwezekani MTU analipwa posho ya laki afu amsimamie MTU anaelipwa mshahara ambao mpaka wafanane hiyo posho iingie Mara 4, 5 au 10.. Kama sio kutengeneza fitna ni nini? Kamati ya nidhamu ya watumishi wa halmashauri iwe mkoa na katika halmshauri msimamizi wa watumishi wa serikali awe mkurugenzi tu, ilikuondoa kila MTU boss.. Inamfanya mtumishi ashindwe tekeleza wajibu wake ipasavyo
 
Ondoa wakuu wa idara wafuatao ili upate amani,wamekuwa miungu watu na ni walamba Rushwa wakubwa, DT geita TC, DT kahama manispaa, DT songwe, Afisautumishi Ilala, afisaelimu secondary Halmashauri ya Meru, Ilemela, Arusha Jiji, afisaelimu msingi Halmashauri za Korogwe, Moshi manispaa kule Kilimanjaro. Geita vijijini
Tt geita Tc mbona n mpya ana kama mwaka hivi nini shida
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Ummy Mwalimu ameahidi kufanya mabadiliko makubwa kwa watendaji wa mamlaka za serikali za mitaa kutokana na kutoridhishwa na utendaji kazi wa baadhi ya watumishi na Wakuu wa Idara katika mamlaka hizo.

Waziri Ummy ametoa kauli hiyo jijini Dodoma wakati akifunga kikao kazi cha wakuu wa idara za utawala na rasilimali watu katika utumishi wa umma, ambapo amebainisha kuwa baadhi yao wamekuwa wakitengeneza madaraja kati yao na watumishi wanaowasimamia.

Aidha, Mhe. Ummy amesema ofisi yake inakusudia kufanya mabadiliko ya utaratibu wa watumishi na watendaji katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ikiwemo kuondoa mamlaka za nidhamu kutoka kwenye Baraza la Madiwani.

Chanzo: ITV
Atafanya mabadiliko atawapeleka wapi? watabaki halmashauri kama siku zote
 
Wewe itakuwa diwani kama sio basi ndugu yako, kama sio ndugu yako basi jamaa yako, haiwezekani MTU analipwa posho ya laki afu amsimamie MTU anaelipwa mshahara ambao mpaka wafanane hiyo posho iingie Mara 4, 5 au 10.. Kama sio kutengeneza fitna ni nini? Kamati ya nidhamu ya watumishi wa halmashauri iwe mkoa na katika halmshauri msimamizi wa watumishi wa serikali awe mkurugenzi tu, ilikuondoa kila MTU boss.. Inamfanya mtumishi ashindwe tekeleza wajibu wake ipasavyo
Well said maana madiwani wa CCM ni wahuni sn wanaonea watumishi
 
Back
Top Bottom