Waziri Ummy Mwalimu: Wanaokata Bima ya Afya wakiwa wagonjwa wanatishia ustahamilivu wa Mfuko

Waziri Ummy Mwalimu: Wanaokata Bima ya Afya wakiwa wagonjwa wanatishia ustahamilivu wa Mfuko

Huyu mama aisee....

Bora hata asingejibu kabisa.... .. sasa ni wakati upi bima itajua huyu anaumwa na huyu haumwi?

Kwanini wasikiri tu kuwa , mfuko hauna fedha au modeling yao ni mbovu.

Watu wanachanga pesa kidogo ambazo haiziendani na gharama za matibabu, sio kujaribu ku victimize kila kitu na kila idea.

Kumchelewesha mteja kupata huduma for any reason whatsoever is just isn't right...
Aliyelalamika kuhusu watoto hajasema kama mtoto kakatiwa bima baada ya kuzaliwa. Bima za vifurushi vya hiari wameweka ianze kufanya kazi miezi mitatu makusudi kabisa, maana watu walikuwa wanakwenda kukata Bima huku wanayemkatia akiwa anapata matibabu sehemu fulani. Kukata bima ilikuwa ni kukimbia mzigo wa matibabu na kuibebe Bima ambayo mgonjwa tajwa hakuwa mwanachama wake. Huo ulikuwa wizi, na inakinzana na maana ya Bima. Ndio maana hata ukienda kukata bima ya gari ambayo ni comprehensive wanapiga picha gari, kujiridhisha kama kweli lina hali yenye thamani uliyotaja na liko salama. Huwezi kata bima ya afya wakati unaumwa, ukifanya hivyo mantiki yake inapotea.
 
Anamaanisha kifurushi cha wiki cha dakika unatakiwa uunge ukiwa huna shida ya kuwapigia watu huku muda unaenda tu.

Kuunga na kuwapigia watu ni hasara kwa mtandao.
 
We mbuzi huna akili
👇👇
IMG_20221108_203949.jpg
 
Waziri yupo sahihi. Nawapa mfano halisi kabisa:

Mwezi wa nne mwaka huu kuna dada alifika hospitalini akiwa anaumwa, tumbo lilikua limevimba kiasi na alikua anaskia maumivu makali wakati anapokua ktk siku zake. Umri ana miaka 35 na hakuwahi kushika mimba.

Tukafanya vipimo vingi ikiwemo ultrasound ambayo ilionyesha ana "pedunculated uterine myoma yenye 15cm by 20cm". Yani kwa kifupi alikua na fibroid kubwa kwa nje ya mji wa uzazi ambayo kimsingi ilibidi itolewe. Tukamshauri kuhusu upasuaji akasema sawa nitarudi.

Kumbe mwenzetu haraka akaenda kukata bima. Kama mnavyojua mchakato unachukua miezi mitatu kupata bima yako. Kwahyo akaja tena mwezi wa nane mwaka huu akiwa na bima yake huku ile hali aliyokua nayo mwanzo ikiwa imebadilika kabisa (yani alikuja akiwa hoi bin taabani). Tuliishia kutoa kizazi ili kumuokoa yule dada. Pengine angewahi matibabu haraka asingefikia hatua ile.
 
Huyu mama aisee....

Bora hata asingejibu kabisa.... .. sasa ni wakati upi bima itajua huyu anaumwa na huyu haumwi?

Kwanini wasikiri tu kuwa , mfuko hauna fedha au modeling yao ni mbovu.

Watu wanachanga pesa kidogo ambazo haiziendani na gharama za matibabu, sio kujaribu ku victimize kila kitu na kila idea.

Kumchelewesha mteja kupata huduma for any reason whatsoever is just isn't right...
Hapo sasa ndiyo ametumia akili yake ya kuunga unga ile halisi. Nyakati zingine anakuwa kalishwa madesa
 
Probability princpals ..ah ngoja nirudi zangu jukwaa la lngu pendwa la sports,..hapa naweza kua mabishana na Wana historia na sayansi ya jamii.
Inawezekana umesomea mambo hayo lakini umekariri vibaya. Yes, Waziri maybe anazungumzia issue ya "adverse selection" lakini majibu aliyotoa ni tofauti na hoja ya aliyejibiwa.

Miongoni mwa matatizo ya wasomi wetu ni kutotumia usomi kwenye kutekeleza majukumu yao. Ndio maana kuna uzi wa johnthebaptist anasema kuna kazi zinazofanywa na baadhi ya taasisi zinaweza kufanywa na lasaba B.

Tatizo lingine la wasomi wetu ni kutokuwa na uwezo wa kutambua kiini cha tatizo na suluhu yake na hili ni tatizo la kutoelewa dhana ya vitu kuhusiana na kusababishana (ignorance about correlation and causation). Matokeo yake decision zinazofanywa zimekuwa zikiumiza kundi kubwa la watu ambao hawahusiki.

Tatizo la tatu ni kutoelewa "operational models za taasisi au mambo mbalimbali na madhara yake au mabadiliko yake. Mfumo wa Bima ya Afya nadhani ni lazma kwa mtumishi wa umma (kama sijakosea), no matter kama mtumishi huyo na wanufaika wake wanajijua kama wana historia ya kuumwa umwa au hapana. Na kutokana na hilo NHIF imekuwa Taasisi hodhi ya Bima ya Afya nchini kwetu. Hii ni kutokana na kuangalia upande mmoja tu wa kupata pesa kutoka katika mapato ya mtumishi.

Kwa maoni yangu, huenda tatizo hilo lingeisha kama watumishi pamoja na ulazima wa kuwa na Bima ya Afya, lakini wangepewa chaguo la kujiunga na Bima ya Afya waitakayo. Kwa kufanya hivyo, tatizo analosema Waziri huenda lisiwepo au likapungua kwani mfuko wenye ushindani dhaifu ungeondoka sokoni na pia historia ya mgonjwa ingetumika katika kutambua package inayomfaa. Changamoto za afya zimeongezeka kutokana na kuongezeka kwa presha ya maisha, na pia idadi ya watumishi wa umma imekuwa ikiongezeka kwa kasi kiasi cha NHIF kuzidiwa.

Aidha, kutowaadhibu wasiohusika, kungekuwa na mfumo wa matibabu uliounganishwa (integrated health services, IHS) ambapo historia ya mgonjwa inaweza kuonekana wakati wowote na popote anapoenda kupata huduma za afya (na hivyo kupunguza athari za kuficha maradhi wakati wa kukata bima).
 
Inawezekana umesomea mambo hayo lakini umekariri vibaya. Yes, Waziri maybe anazungumzia issue ya "adverse selection" lakini majibu aliyotoa ni tofauti na hoja ya aliyejibiwa.

Miongoni mwa matatizo ya wasomi wetu ni kutotumia usomi kwenye kutekeleza majukumu yao. Ndio maana kuna uzi wa johnthebaptist anasema kuna kazi zinazofanywa na baadhi ya taasisi zinaweza kufanywa na lasaba B.

Tatizo lingine la wasomi wetu ni kutokuwa na uwezo wa kutambua kiini cha tatizo na suluhu yake na hili ni tatizo la kutoelewa dhana ya vitu kuhusiana na kusababishana (ignorance about correlation and causation). Matokeo yake decision zinazofanywa zimekuwa zikiumiza kundi kubwa la watu ambao hawahusiki.

Tatizo la tatu ni kutoelewa "operational models za taasisi au mambo mbalimbali na madhara yake au mabadiliko yake. Mfumo wa Bima ya Afya nadhani ni lazma kwa mtumishi wa umma (kama sijakosea), no matter kama mtumishi huyo na wanufaika wake wanajijua kama wana historia ya kuumwa umwa au hapana. Na kutokana na hilo NHIF imekuwa Taasisi hodhi ya Bima ya Afya nchini kwetu. Hii ni kutokana na kuangalia upande mmoja tu wa kupata pesa kutoka katika mapato ya mtumishi.

Kwa maoni yangu, huenda tatizo hilo lingeisha kama watumishi pamoja na ulazima wa kuwa na Bima ya Afya, lakini wangepewa chaguo la kujiunga na Bima ya Afya waitakayo. Kwa kufanya hivyo, tatizo analosema Waziri huenda lisiwepo au likapungua kwani mfuko wenye ushindani dhaifu ungeondoka sokoni na pia historia ya mgonjwa ingetumika katika kutambua package inayomfaa. Changamoto za afya zimeongezeka kutokana na kuongezeka kwa presha ya maisha, na pia idadi ya watumishi wa umma imekuwa ikiongezeka kwa kasi kiasi cha NHIF kuzidiwa.

Aidha, kutowaadhibu wasiohusika, kungekuwa na mfumo wa matibabu uliounganishwa (integrated health services, IHS) ambapo historia ya mgonjwa inaweza kuonekana wakati wowote na popote anapoenda kupata huduma za afya (na hivyo kupunguza athari za kuficha maradhi wakati wa kukata bima).
SAWASAWA....
👍 👍
 
Waziri yuko sahihi. Unakata Bima leo kesho unataka ukatibiwe. Mfuko lazima ufe.

Ijapokuwa kuna juhudi za lazima zifanyike kuwaeleimisha watu umuhimu wa kuwa na Bima Mapema kabla ya majanga.
 
View attachment 2444948
Mdau kwenye mtandao wa Twitter ametoa hoja yake kuhusu bima na kuwatag Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, Viongozi wa Taasisi ya NHIF na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wanawake na Makundi Maaalum, Dkt. Dorothy Gwajima.

Ameandika: “Kilio cha Wazazi wengi kwa Sasa ni Swala la Ku Apply Bima ya Afya kwa watoto kisha ikae Miezi 3 ndio waweze Kuitumia halijakaa sawa. Tunaomba mpitie Kipengele hiki cha muda wa Kusubiri Mkirekebishe.

Waziri Ummy Mwalimu akajibu: “Tatizo baadhi ya watu wanakata Bima ya Afya tayari wakiwa ni wagonjwa tena wengine wakiwa wodini. Hatua hii inatishia uhai na ustahamilivu wa Mfuko. Nitumie fursa hii kuhimiza wananchi kukata Bima ya Afya kabla ya kuugua.”
Hapa Tanzania tunakwenda kidhulma tu ninavyojuwa Mimi katika kuweka bima ya afya sio kwamba ile pesa uliyochangia ndiyo itakayokutibu isipokuwa wako wachaniaji wengine wala hawaumwi na wanachangia miaka kwa miaka sasa ukisema mtu akae miaka mitatu ndipo aweze kupata huduma huo ni wizi na ukatili wa serikali kwa raia wake au kwa nini usiseme kwa wale wanaochangia muda mrefu bila ya kuumwa basi warejeshewe michango yao,serikali mna jukumu la kuchangia pia katika mfuko huo kila mwaka.
 
Naona waziri yuko sahihi. Unaweza kukatia gari yako bima baada ya kupata ajali, na bima hiyo ikakufidia hiyo ajali ambayo wakati unakata bima ilishatokea? Kama kila mtu atangojea augue ndipo akate bima, huo mfumo utaweza kujiendesha?
Sinimpaka uwe na gari,kama hauna gari unaweza kuikatia bima? kwaiyo kukata bima baada ya kuwa mgonjwa ni sawa.
 
View attachment 2444948
Mdau kwenye mtandao wa Twitter ametoa hoja yake kuhusu bima na kuwatag Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, Viongozi wa Taasisi ya NHIF na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wanawake na Makundi Maaalum, Dkt. Dorothy Gwajima.

Ameandika: “Kilio cha Wazazi wengi kwa Sasa ni Swala la Ku Apply Bima ya Afya kwa watoto kisha ikae Miezi 3 ndio waweze Kuitumia halijakaa sawa. Tunaomba mpitie Kipengele hiki cha muda wa Kusubiri Mkirekebishe.

Waziri Ummy Mwalimu akajibu: “Tatizo baadhi ya watu wanakata Bima ya Afya tayari wakiwa ni wagonjwa tena wengine wakiwa wodini. Hatua hii inatishia uhai na ustahamilivu wa Mfuko. Nitumie fursa hii kuhimiza wananchi kukata Bima ya Afya kabla ya kuugua.”
Kwa hiyo kuna wenzetu huwa wanajua kuwa kesho ijayo nitaamwa ni bora nikate bima mapema! Huyu waziri hivi hajui kuwa hali ya maisha ya walala hoi? Mtu masikini atanunuaje bima ilhali hata hajua kesho atakula na kuwalisha wanawe? Atakataje bima na aondokane na pesa zake ilhali hata hajui kama kwa mwaka mzima ataumwa na kuhitaji matibabu hospitali? by thew way. to be hinest mfumo mzima wa Bima tanzania ni wa kushangaza anyway!
 
Waziri yupo sahihi. Nawapa mfano halisi kabisa:

Mwezi wa nne mwaka huu kuna dada alifika hospitalini akiwa anaumwa, tumbo lilikua limevimba kiasi na alikua anaskia maumivu makali wakati anapokua ktk siku zake. Umri ana miaka 35 na hakuwahi kushika mimba.

Tukafanya vipimo vingi ikiwemo ultrasound ambayo ilionyesha ana "pedunculated uterine myoma yenye 15cm by 20cm". Yani kwa kifupi alikua na fibroid kubwa kwa nje ya mji wa uzazi ambayo kimsingi ilibidi itolewe. Tukamshauri kuhusu upasuaji akasema sawa nitarudi.

Kumbe mwenzetu haraka akaenda kukata bima. Kama mnavyojua mchakato unachukua miezi mitatu kupata bima yako. Kwahyo akaja tena mwezi wa nane mwaka huu akiwa na bima yake huku ile hali aliyokua nayo mwanzo ikiwa imebadilika kabisa (yani alikuja akiwa hoi bin taabani). Tuliishia kutoa kizazi ili kumuokoa yule dada. Pengine angewahi matibabu haraka asingefikia hatua ile.
Huyu aliamua kuwa mjanja tu maana angeitumia Bima ndani ya siku 30 alizopewa ingegoma hivyo akaamua sogeza siku mbele.
 
Back
Top Bottom