msovero
JF-Expert Member
- Jun 30, 2019
- 863
- 1,534
Dada Ummy sina shaka na utendaji kazi wako lakini nakushauri upunguze kujieleza kwa sababu maelezo unayotoa yanakufunga.
Mtangulizi wako pamoja na kuwa na maneno mengi lilipokuwa linakuja suala nyeti la kitaifa alikuwa makini sana kuchunga kauli zake ili kuepusha maswali na mijadala isiyo ya lazima kwa watu.
Unachotakiwa utambue ni kuwa wizara uliyopewa ina changamoto nyingi kwakuwa inagusa karibia kila sekta kuanzia afya, elimu, miundombinu, wafanya biashara pamoja na ajira kwa vijana.
Kwahiyo ni wizara inayohitaji umakini na utulivu mkubwa kuiongoza kabla ya kuamua au kutamka jambo lolote unalotaka umma usikie vinginevyo utakuwa unajifunga kwa kauli zako kila wakati.
Mathalani nitolee mfano suala hili la ajira. Hapakuwepo haja ya kutaja idadi ya waombaji ikiwa bado maombi yanaendelea kwa sababu umeleta tension kubwa na hali ya kukata tamaa kwa waombaji.
Kadhalika suala la vigezo vya kuajiri lingebaki kuwa siri yenu wizarani ili waombaji wabaki na kazi moja tu ya kusubiria majina au pdf kama wengi wanavyopendelea kuita. Lakini kusema wizara inafikiria kutumia kigezo hiki na kile unazidi kuwajengea hofu waombaji na kujifunga pia endapo mambo yatakwenda tofauti na ulichokisema.
Nikupe mfano mwingine. Ukiwa bungeni leo umesema wizara itatoa kipaumbele kwa wahitimu wa miaka ya 2012 lakini kumbu kumbu zinaonyesha wahusika hao walishaajiriwa na hawapo. Katika kuthibitisha hili nimekuwekea viambatanisho vya matangazo ya ajira 2019 na 2020 ambayo yote yanaonyesha wahitimu waliopo ni kati ya 2014 na kuendelea..
Kiambatanisho 1: Tangazo la ajira za mwaka juzi likionyesha wahitimu wa kuanzia 2014-2017
Kiambatanisho 2: Tangazo la ajira la mwaka jana likionyesha wahitimu waliopo ni kuanzia 2014-2019
Lakini tangazo lako linasema kuna wahitimu hadi wa 2012 na 2013 na wewe mwenyewe umekiri kwamba mnafikiria kutoa priority kwa wahitimu hao ambao takwimu zinaonyesha tayari walishaajiriwa miaka ya nyuma huko pamoja na wahitimu wa 2014. Je, inakuaje tena uwape kipaumbele wahitimu hawa ambao serikali iliwaajiri miaka kadhaa iliyopita?? Kama waliacha kazi kwa hiari zao unahangaika nao wa nini dada ummy??
Mtangulizi wako pamoja na kuwa na maneno mengi lilipokuwa linakuja suala nyeti la kitaifa alikuwa makini sana kuchunga kauli zake ili kuepusha maswali na mijadala isiyo ya lazima kwa watu.
Unachotakiwa utambue ni kuwa wizara uliyopewa ina changamoto nyingi kwakuwa inagusa karibia kila sekta kuanzia afya, elimu, miundombinu, wafanya biashara pamoja na ajira kwa vijana.
Kwahiyo ni wizara inayohitaji umakini na utulivu mkubwa kuiongoza kabla ya kuamua au kutamka jambo lolote unalotaka umma usikie vinginevyo utakuwa unajifunga kwa kauli zako kila wakati.
Mathalani nitolee mfano suala hili la ajira. Hapakuwepo haja ya kutaja idadi ya waombaji ikiwa bado maombi yanaendelea kwa sababu umeleta tension kubwa na hali ya kukata tamaa kwa waombaji.
Kadhalika suala la vigezo vya kuajiri lingebaki kuwa siri yenu wizarani ili waombaji wabaki na kazi moja tu ya kusubiria majina au pdf kama wengi wanavyopendelea kuita. Lakini kusema wizara inafikiria kutumia kigezo hiki na kile unazidi kuwajengea hofu waombaji na kujifunga pia endapo mambo yatakwenda tofauti na ulichokisema.
Nikupe mfano mwingine. Ukiwa bungeni leo umesema wizara itatoa kipaumbele kwa wahitimu wa miaka ya 2012 lakini kumbu kumbu zinaonyesha wahusika hao walishaajiriwa na hawapo. Katika kuthibitisha hili nimekuwekea viambatanisho vya matangazo ya ajira 2019 na 2020 ambayo yote yanaonyesha wahitimu waliopo ni kati ya 2014 na kuendelea..
Kiambatanisho 1: Tangazo la ajira za mwaka juzi likionyesha wahitimu wa kuanzia 2014-2017
Kiambatanisho 2: Tangazo la ajira la mwaka jana likionyesha wahitimu waliopo ni kuanzia 2014-2019
Lakini tangazo lako linasema kuna wahitimu hadi wa 2012 na 2013 na wewe mwenyewe umekiri kwamba mnafikiria kutoa priority kwa wahitimu hao ambao takwimu zinaonyesha tayari walishaajiriwa miaka ya nyuma huko pamoja na wahitimu wa 2014. Je, inakuaje tena uwape kipaumbele wahitimu hawa ambao serikali iliwaajiri miaka kadhaa iliyopita?? Kama waliacha kazi kwa hiari zao unahangaika nao wa nini dada ummy??