Waziri Ummy : Wagonjwa wasitozwe gharama za posho ya dereva wala muuguzi ambao usindikiza mgonjwa na ambulance

Waziri Ummy : Wagonjwa wasitozwe gharama za posho ya dereva wala muuguzi ambao usindikiza mgonjwa na ambulance

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Snapinsta.app_452969009_18291073693203109_8574163368861664726_n_1080.jpg

Snapinsta.app_453003734_18291073753203109_673806947906266105_n_1080.jpg
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amekemea na kuwaonya viongozi wa Hospitali nchini ambazo zina magari ya kubebea wagonjwa (ambulance) wenye tabia ya kutoza wagonjwa au ndugu zao malipo ya posho ya dereva pamoja na mtaalamu ambaye uhusika katika safari.

Amesema kwamba ni marufuku kwa hospitali zote nchini ambazo zipo chini ya Serikali kuwatoza kuwatoza wananchi pesa ya posho ya dereva wala mtaalamu ambao uhusika kusindikiza mgonjwa na ambulance.
Snapinsta.app_453000813_18291073711203109_2974442295477406524_n_1080.jpg
"Marufuku kwa Hospitali zote nchini kuwatoza wananchi pesa ya posho ya dereva wala muuguzi anayesindikiza mgonjwa na badala yake mwananchi anatakiwa kuchangia gharama za mafuta tu," amesema Ummy.

Waziri Ummy ameyasema hayo Julai 28, 2024 akiwa mkoani Tanga wakati akikabidhi gari la kubebea wagonjwa kwa uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa huo, ikiwa gari hiyo kati ya magari 736 yanayodaiwa kununuluwa na Serikali.

Sanjari na hilo Waziri Ummy amesisitiza umuhimu wa matumizi stahiki ya magari hayo huku akionya yasitumike katika shughuli nyingine tofauti ili yaweze kudumu kwa muda mrefu.
 
hakika amewasaidia watanzania masikini.

landcruiser inatumia lau dizeli 1lt/6km. tutegemee ratio ya scania 113 kwa hesabu ya 1lt/2km
 
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amekemea na kuwaonya viongozi wa Hospitali nchini ambazo zina magari ya kubebea wagonjwa (ambulance) wenye tabia ya kutoza wagonjwa au ndugu zao malipo ya posho ya dereva pamoja na mtaalamu ambaye uhusika katika safari.

Amesema kwamba ni marufuku kwa hospitali zote nchini ambazo zipo chini ya Serikali kuwatoza kuwatoza wananchi pesa ya posho ya dereva wala mtaalamu ambao uhusika kusindikiza mgonjwa na ambulance.
"Marufuku kwa Hospitali zote nchini kuwatoza wananchi pesa ya posho ya dereva wala muuguzi anayesindikiza mgonjwa na badala yake mwananchi anatakiwa kuchangia gharama za mafuta tu," amesema Ummy.

Waziri Ummy ameyasema hayo Julai 28, 2024 akiwa mkoani Tanga wakati akikabidhi gari la kubebea wagonjwa kwa uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa huo, ikiwa gari hiyo kati ya magari 736 yanayodaiwa kununuluwa na Serikali.

Sanjari na hilo Waziri Ummy amesisitiza umuhimu wa matumizi stahiki ya magari hayo huku akionya yasitumike katika shughuli nyingine tofauti ili yaweze kudumu kwa muda mrefu.
Neno la Wsziri siyo sheria.
Neno la Rais ndilo sheria.

Ummy ajifunze kufuata taratibu badala ya kutoa matamko anayojua kabisaa kuwa hayana legitimacy kisheria
 
Back
Top Bottom