DOKEZO Waziri wa Elimu, huu mtindo wa Kubakiza watoto shuleni wakati wa likizo ni Sahihi?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kumuacha shule ndo kumpambania.hapo unapambania watoto wa walimu sio wakwako.Nenda hapo shuleni kwao utakuta wamebaki walimu wawili wengine wako makwao kufanya mambo yao.watoto nikupiga makelele nakupewa na maasignment yasiyona kichwa wala miguu.
Ile tu kuwa kwenye mazingira ya shule, inampa utayari kwa mtihani; akija nyumbani na kukaa muda mrefu halafu arudi shule, inaweza kumchukua muda kuwa na ule utayari wa kufanya mtihani
 
[emoji28][emoji28][emoji28]Eti watoto wako bize wanatafuta thamani ya X,
Ila kweli watoto wanatakiwa wajue kazi ndogo ndogo kwa kadri ya umri wao
 
Kumuacha shule ndo kumpambania.hapo unapambania watoto wa walimu sio wakwako.Nenda hapo shuleni kwao utakuta wamebaki walimu wawili wengine wako makwao kufanya mambo yao.watoto nikupiga makelele nakupewa na maasignment yasiyona kichwa wala miguu.
Ni kweli kabisa
 
Nature ya mitihani imekaaje?Ninyi walimu si ndio mnatakiwa kushauri aina ya mitihani na nature yake iweje?
Na suala la kubakiza watoto linapaswa liwe shirikishi sio shule kuamua tu,sasa hapo mwalimu utaacha kulaumiwa?

Tunataka mtoto ajifunze na mambo mengine sio kufualu mitihani tu
 
Ina maana uelewi kazi ya serikali?.Au mzazi mmoja mmoja atawezaje kubadilisha jambo linalofanywa kwenye jamii ya wengi.Walioweka serikali hawakua wajinga.
Huyo jamaa anaongea utadhani hajui wajibu wa serikali kwa maananchi wake
 
Huyo ni mnufaika.
Mbona sisi tulisoma kwa masaa 5:20 kwa siku 194 na syllabus tulimaliza

Hawa ni wapigaji tu
 
Wazazi WA Siku hizi sio walezi wanajua kuzaa TU ndo maana maadli yanashuka tunasingia Ulaya,Lea mwanao mwenyewe Kaa nae likizo msome Mtoto ujue tabia zake
Mnataka walimu wawaleee na housemade from January to December,Hivi hamuoni haya na Hilo suala Hapo ukute Kuna mzazi kaliunga mkono la watoto kubaki shule
Katoto ka std 4 kanabaki kufanya Nini?!!lini wazazi tutajua watoto wety tabia zao?uwezo wao?madhaifu Yao?!
Yaani tunakoelekea ni mtihani Sana Mungu atulinde...!!!
 
Waziri mwenyewe kairuki hapitagi mtandaoni
Waziri wa Elimu ni Prof. Mkenda na huu ujumbe tayari jana alishafikishiwa na Uongozi wa JF na alisema Wizara Itatoa Kauli.
 
Mitaala na ratiba za muhula wote ziko wazi. Ila uvivu wa walimu wanatumia kipindi cha likizo na weekend kutafuta kipato haramu.
Pia linalosikitisha zaidi ni kwamba madarasa ya mtihani kuwekwa busy maana yake tanzania tunasomea mtihani tu
Yeah Tanzania miaka ya hivi karibuni kumegeuka na kikundi cha shule na wazazi wakitaka watu wafaulu tu
 
Sasa hao wanafunzi watakaa muda gani wakati mnataka mpige pesa za tuition?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…